Mbunge Ataka Mawaziri Wafanyiwe ‘Interview’ Kabla ya Kuteuliwa

Dodoma. Mbunge wa Geita Vijijini (CCM), Joseph Kasheku maarufu kwa jina la Msukuma, ametaka mawaziri kufanyiwa usahili kabla ya kuteuliwa kushika nafasi hizo kutokana na baadhi yao kuwa na elimu ya juu, lakini wanashindwa kutekeleza majukumu yao kikamilifu.
Mbunge Msukuma
Akichangia katika hotuba ya Bajeti Kuu leo Alhamisi bungeni mjini hapa, Msukuma amesema walioaminiwa na kupewa nafasi hizo wamekuwa wakitajwa kwenye kashfa kubwa.
“Wengine wamegushi vyeti, tukiangalia wana madigrii huenda wengine wana uwezo mdogo wanazidiwa na makaratasi makubwa,”amesema.
 ASANTE KWA KUTEMBELEA MTANDAO WETU!!

from Blogger http://ift.tt/2se1Dhl
via IFTTT