Majeruhi wa Ajali ya Wanafunzi 32 Arusha ,Doreen Mshana Aruhusiwa Kutoka Hospitalini Marekani..!!

Mtoto Doreen Mshana, manusura wa ajali ya Lucky Vincent, ameruhusiwa kutoka Hospitali na sasa ameungana na wenzake wawili katika nyumba maalum wanamoishi, Marekani, jimbo la Iowa.
Awali, wanafunzi wengine waliokuwa wakitibiwa katika Hospitali ya Mercy Hospital, Sioux City, Saidia Awadh na Wilson Tarimo, waliruhusiwa kutoka hospitali walimokuwa wakitibiwa.
Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu, ameandika katika ukurasa wake wa facebook na kueleza kuwa sasa Doreen, ameungana na wenzake baada ya hali yake kuimarika.
Doreen, alibaki hospitali hapo kutokana na majereha makubwa aliyopata na hivyo kulazimika kufanyiwa upasuaji mkubwa wa uti wa mgongo.
Wanafunzi hao walinusurika katika ajali ya basi la shule ya msingi ya Lucky Vincent, iliyoua wanafunzi 32, walimu wawili na dereva, Mei 6 mwaka huu, Karatu, Arusha.

from Blogger http://ift.tt/2s8CQh6
via IFTTT