Vijana wajiunga na al-Shabab Kenya

Polisi nchini Kenya wamewalaumu viongozi watatu wa kiislamu kwa kuwashawishi vijana wakiwemo wanafunzi wa vyuo vikuu kujiunga na kundi la kiislamu la al-Shabab.

Polisi wanadai kuwa viongozi hao wa kiislamu walivuka mpaka na kuingia nchini Somalia yalipo makao makuu ya al Shabab ambapo huwashawishi vijana hao kupitia kwa mitandao.
Vijana wajiunga na al-Shabab Kenya
Polisi wanadai kuwa viongozi huwahidi watu pesa nyingi ikiwa watajiunga na kundi hilo lenye mahusiano na mtandao wa al-Qaeda.
Vingozi hao hata hivyo hawajatamka lolote kufuatia madai hayo.