Wafanyabiashara wafunga maduka kwa siku nzima Njombe na Makambako

KWA siku nzima ya leo wafanyabiashara wamefunga maduka yao kwa kilekinacho daiwa kuwa ni kuwa katika siku ya kesi ya mwenyekiti wao wa taifa wa jumuia ya wafanyabiashara JWT, Taifa John Minja.

WAFANYABIASHARA mkoani Njombe na mji mdogo wa Makambako walifunga maduka kwa zaidi ya masaa 6 Siku ya juzi na kwenda mahakamani kusikiliza kesi ya mfanyabiashara mwenzao ambaye alipandisha mahakamani kwa mara ya kwanza Februari 6 mwaka huu na baadae kufanya mkutano wao.

Mfanyabiashara mwenzao Maxson Sanga alipandishwa katika mahakama ya hakimu mkazi Njombe Februari 6 mwaka huu na mamlaka ya mapato Tanzania (TRA) kwa kile lilichodaiwa kuwazuia kuwazuia kufanya kazi zake na kudai kuivunja sheria ya kodi namba 4 ya mwaka 2004.

Sanga alipandishwa mahakamani na wasimamizi wake wawili wa kampuni yake ya Mexons Investment Co. Ltd akiwemo Meneja wa Kampuni hiyo Emma Mgeni, na mkewe Happy kwa mashtaka ya kudaiwa kuwagomea maofisa wa mamlaka ya kukusanya mapato kanda ya Mbeya (TRA) waliofika katika eneo lake la biashara kwa lengo la kumkagua biashara yake.

Kesi hiyo iliyo wafanyawafanyabiashara kufunga maduka yao na kusababisha wakazi wa Mjini Njombe na baadhi ya wafanyabiashara kutoka makambako iliahilishwa kwa kuwa wakili upande wa TRA kuwa nje ya mji na kuifanya hakimu mkazi wa mahakama ya hakimu mkazi wa mahakama ya Njombe, Augustine Rwinzile kuiahilisha mpaka Aprili 8.

Katika mahakama ya hakimu mkazi Njombe polisi wa kutuliza ghasia (FFU) wakiwa na gari moja la polisi lenye namba za usajili PT 1864 na zaidi ya askari wasiopungua 18, walikuwepo mahakamani  hapo kwa lengo la kuangalia usalama huku wakiwa wamejiandaa kwa mabomu ya machozi huku wakiwa wamevalia mavazi ya kupambana na vurugu.

Baada ya kesi hiyo kuahilishwa kwa kesi hiyo wafanyabiashara wote waliondoka kwa umoja wao kuelekea katika ukumbi wa mikutano wa Turbo huku wakifiatiliwa nyuma na polisi hao na mkutano wao kulindwa na askali hao mwanzo mpaka mwisho kukiwa kumetawala amani ya kutosha katika ukumbi huo  na wafanyabiashara waliokuwa nje ya ukumbi kuambiwa waingie ndani na kupewa onyo na askali aliyekuwa amevaa mavazi ya kuraia.

Mkutano huo uliodumu kwa masaa zaidi ya manne ulifunguliwa na mwenyekiti wa korido ya wafanyabiashara wakubwa na wenye viwanda (TCCIA) mkoa wa Njombe Oraph Mhema ambaye aliwataka wafanyabiashara hao kuwa na umoja katika biashara zao na kupinga matendo mbalimbali ya rushwa na yanayo shawishi rushwa yanayo fanywa na TRA.
Alisema kuwa moja ya mambo ambayo wafanyabiashara wanatakiwa kuweka wazi ni pamoja na TRA kutumia madalali kukusanya kodi wakati wao wanalipwa mshahara kwaajili ya kukusanya kodi za watanzania.

“Wafanyabiashara ntatakiwa kuweka wazi na kutoa taarifa mapema mnapoona kuna dalili za kufanyiwa vitendo vya kuwashawishi kutoa rushwa, TRA wamekuwa wakiwatumia madalali kukusanya kodi na makufuli yao kufunga maduka yenu yakiwa na nembo za TRA, kitu hicho tunatakiwa kukipiga vita kwa sababu maofisa wanalipwa kwaajili ya kazi ya kukusanya kodi haiwezekani tukalipa kodi, madalali na maofisa,” alisema Mhema.

Aliongeza kuwa: "Kama hatutaungana wafanyabiashara kwa dhati, hakika hatutasonga mbele, meneja wa TRA mkoani Njombe tulizungumza nae kuhusu kesi inayomkabili mwenzetu Mexons alisema hana kosa, maofisa wa TRA walifanya oparesheni bila yeye kupata taarifa," alisema Mhema.

Mhema alisema kuwa hata hivyo kufuatia kesi inayomkabili mfanyabiashara huyo, Mexons ameombwa atoe shilingi laki mbili ili kesi hiyo ifutwe, jambo ambalo Mhema alisema wamepinga kutolewa fedha hizo na badala yake kumtaka aliyeifungua kesi hiyo ndiyo wanaopaswa kulipa fedha hizo.

Aidha katika hatua nyingine, Mhema alisema Kamishna Mkuu wa TRA nchini atakutana na wafanyabiashara wote mjini Makambako Machi 7 mwaka huu katika ukumbi wa Green City uliopo mjini Makambako kwa ajili ya kuzungumzia kupinga ongezeko la kodi la asilimia 100.

Naye Mwenyekiti wa Jumuia ya Wafanyabiashara mjini Makambako, Siphaely Msigala alisema katika kikao kitakachofanyika Machi 7 na Kamishana Mkuu wa TRA mjini Makambako, wafanyabiashara wote wametakiwa kufunga biashara zao kwa ajili ya kwenda kuzungumza na Kamishna huyo.

Alisema kuwa katika mkutano huo kutakuwa na Mkuu wa Mkoa Dk. Rehema Nchimbi, Mkuu wa Wilaya ya Njombe, Sarah Dumba, Wakurugenzi wa Halmashauri ya mji wa Makambako na Halmashauri ya Mji Njombe pamoja na kamanda wa polisi, Fulgence Ngonyani .


Alisema lenho la kuwaalika viongozi hao wa juu ni kuja kujua matatizo yao wakati wanawasilisha kwa kamishina wa TRA taifa.