Mazungumzo ya Umoja wa Mataifa kuhusu mabadiliko ya tabia nchi
yamekamilika mjini Warsaw. Awali nchi mbili zinazotoa kiwango kikubwa cha
gesi zinazochafua mazingira, China na India zilipambana vikali na Marekani
pamoja nchi nyingine kuhusiana na ya kuyaandika mapendekezo yaliyokuwa
yakijadiliwa.
Lakini jana, wawakilishi kutoka takribani nchi 200 walikubaliana
kuhusu maamuzi hayo. Makubaliano hayo yanaruhusu mkataba mpya kuhusu
utoaji wa gesi ya kaboni kuidhinishwa mnamo mwaka wa 2015.
Kongamano
hilo pia liliujadili mpango wa kupunguza uharibifu wa misitu.
Ujumbe wa
Ujerumani katika mkutano huo ulisema maamuzi hayo yanaonyesha dalili
kubwa kwamba hata baada ya kutokea tofauti katika mazungumzo hayo, bado
wajumbe waliweza kulegeza misimamo yao na kufikia mapatano.
Habari na DW.DE
Subscribe to:
Post Comments (Atom)