Juhudi hizo za kusambaza misaada bado zimevurugika huku maafisa
wakisema manusura wa kimbunga hicho wanaendelea kuhangaika na kusubiri
chakula na maji . Ikiwa ni zaidi ya wiki moja baada ya Kimbunga Haiyan kuwauwa watu 3,633, mamia ya wafanyakazi wa kimataifa wa misaada wameweka hospitali za muda na kupeleka misaada. Mataifa kadhaa yakiongozwa na Marekani yanaendelea kuwasilisha misaada yao kwa wahanga wa janga hilo.
