Misaada yaanza kuwafikia waathiriwa Ufilipino

Misaada ya dharura iliyokuwa imesubiriwa kwa hamu imeanza kupelekwa katika eneo lililoathirika zaidi na kimbunga Haiyan nchini Ufilipino  na kuwafikia waathiriwa ambao wamekuwa wakiteseka kwa wiki sasa. Umoja wa Mataifa umekadiria kuwa watu waliowachwa bila makaazi imefikia takriban milioni mbili. 
Juhudi hizo za kusambaza misaada bado zimevurugika huku maafisa wakisema manusura wa kimbunga hicho wanaendelea kuhangaika na kusubiri chakula na maji . 
Ikiwa ni zaidi ya wiki moja baada ya Kimbunga Haiyan kuwauwa watu 3,633, mamia ya wafanyakazi wa kimataifa wa misaada wameweka hospitali za muda na kupeleka misaada. Mataifa kadhaa yakiongozwa na Marekani yanaendelea kuwasilisha misaada yao kwa wahanga wa janga hilo.

Related Posts