YAWA KAMA MBEYA
WAFANYABIASHARA wa Soko la Kariakoo jijini Dar es Salaam wamegoma kufungua maduka yao wakipinga bei kubwa ya mashine za Kielektroniki (EFD) na kutozwa asilimia 18 inayokatwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania(TRA) kwa kila bidhaa inayouzwa.
WAFANYABIASHARA wa Soko la Kariakoo jijini Dar es Salaam wamegoma kufungua maduka yao wakipinga bei kubwa ya mashine za Kielektroniki (EFD) na kutozwa asilimia 18 inayokatwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania(TRA) kwa kila bidhaa inayouzwa.
Wafanyabiashara
hao wamefikia hatua ya kugoma kwa maelezo kuwa serikali haikuwashirikisha
wakati wa kuziazisha matumizi ya mashine hizo.
“Tumegoma
kufungua maduka leo(jana) na hadi pale matatizo yetu yatakapotatuliwa na
kikubwa tulichogomea ni asilimia 18 inayokatwa na TRA kwa kila bidhaa
inayouzwa,” alisema Novaty Tarimo, muuzaji wa simu mtaa wa Narung’ombe na
Msimbazi.
Tarimo
aiambia Elimtaa kuwa , asilimia hiyo inayokatwa na mamlaka hiyo inauwa mitaji yao na wanawaomba wakae
chini na wafanyabiashara hao ili kujua changamoto wanazokabiliana nazo.
“Kero
za polisi na TRA kusimama barabarani kukamata mizigo, kuikagua na kuwaomba
rushwa kwa madai kuwa risiti haiendani na bei ya mizigo,” alisema mmoja wa
wafanyabiashara ya urembo, aliyejitambulisha kwa jina moja la Bonge.
Bonge
alisema, mashine hizo zimekuwa zikiuzwa bei kubwa ambayoinakaribia kuwa sawa na
mitaji yao.
Akizungumza
na waandishi wa habari jana, Mshauri wa
Jumuiya ya Wafanyabiasha hao, Jonson
Minja, alisema wafanyabiashara hao wamelalamikia kutoshirikishwa kwa mambo
mbalimbali yanayowahusu na kuona kama wanadharaulika.
