TAMWA YATOA MAFUNZO KWA WANAHABARI KUHUSU UKATILI WA KIJINSIA

Picha ya pamoja na mgeni rasmi


 Mhariri Mtendaji wa Nipashe Jesse Kwayu akizingumzana waandishi wa hahabari walipata nafasi ya kuhudhulia mafunzo ya kuriporti habari za ukatili wa kijinzia yaliyotoleawa na Muungano wa waandishi waanawake katzania Tamwa jijini Mbeya Jana (Picha na Furaha Eliab, Mbeya).



Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Abbas Kandolo akizungumza na waandishi wa habari wakati akifungua mkutano wa mafunzo kwa waandishi wa habari kuhusiana na ukatili wa kijinisia yaliyotolewa na chama cha waandishi wanawake Tanzania (Tamwa).
 Masa Ngwila ambaye ni muwezeshaji wa semina kwa waandishi wa habari juu ya unyanyasaji wa kijinsia iliyotolewa kwa waandishi wa nyanda za juu kusini, Mbeya, Iringa Njombe Songea, Rukwa na Katavi


IMEBAINIKA kuwa bado kuna ukatrili mkubwa wa kijinsia katika familia za jamii ya kitanzania ambao unafanyika kimya kimya ambao huytokea ndani ya nyumba kati ya mume na mke.

Hayo yamebainishwa na Mkuu wa mkoa wa Mbeya Abbas Kandolo wakati wa ufunguzi wa Mafunzo kwa waandishi wa habari kuriporti matukio ya ukatili wa kijinsia ya siku nne kwa baadhi ya waandishi wa habari wa Nyanda za juu kusini yaliyo tolewa na chama cha wanahabari wanawake Tanzania Tamwa.

Alisema kuwa asilimia kubwa ya familia za kitanzania kuna ukatili mbali mbali wa kijinsia ambao umekuwa ukitokea kimya kimya.

Aliutaja ukatili huio kuwa ni ukatili wa Kingono, ubakaji, kipigo na ulazimishwaji wa mapezi kati ya wanandoa ambao umekuwa ukifanyika kisirisiri katika familia.

Kandolo alisema kuwa waandishi wa habari wanatakiwa kufanya utafiti wa ukatili wa aina hiyo na kuulipoti kisha kuielinisha jamii juu ya ukatili wa aina hiyo ambao umekuwa ukinyanyasa mtu mmoja mmoja katika familia.

Alisema kuwa ukatili huo pia umekuwa ukitokana na mila na destuli zilizopo katika jamii nyingi za kitanzania na waathilika wakuwa wakiwa ni watoto.

Aliongeza kuwa katika utafiti uliofanywa na watu mbalimbali kuhusiana na ukatili wa kijinsia unaofanywa katika ngazi ya familia umebaini kuwa asilimia kubwa umekuwa katika mkoa wa Dodoma asilimia 71 huku mkoa wenye ukatili kwa asilimia ndogo ni mkoa wa Tanga asilimia 16.

Kufuatia uwingi wa asilimia kubwa ya ukatili huo Serikali imetengeneza  mongozo wa kisera na mwongozo wa kutoa huduma kwa waathilika wa ukatili wa kijinsia hasa dhidi ya watoto.

Kwa upande wake muwezeshaji wa mafunzo hayo ambaye pia ni mhariri mtendaji wa Nipashe, Jesse Kwayu alisema kuwa waandishi kama wataelimisha jamii juu ya ukatili huo wananchi watajinasua katika ukatili huo.

Alisema kuwa kuwapo kwa ukatili na unyanyasaji wa kijinsia kunaikwamisha nchi kusonga mbele kimaendeleo kwa ni wanaotendewa ukatili ni wanawake kwa asilimia kubwa na wao ndio chachu ya maendeleo kwa taifa lolote duniani.

Kwayu alisema kuwa katika taifa ambalo hakuna ukatili wa kijinsia taifa hilo limesonga sana katika maendeleo yake.