Maalfu ya watu walijitokeza kwenye barabara
za mjini Moscow ili kufanya maandamano
makubwa ya kuupinga utawala wa Rais
Vladmir Putin.
Viongozi wa upinzani wamesema walioshiriki katika maandamano hayo walifikia watu laki moja, lakini polisi imesema walioshiriki walikuwa watu 20,000 Polisi waliopambana na waandamanaji waliompinga Putin mnamo mwezi wa Mei walikuwa katika hali ya tahadhari lakini hawachukua hatua yoyote safari hii.
Maandamano yalifanyika kwa muda wa saa sita na yalimalizika kwa amani . Maandamano hayo yamefanyika kwa mara ya kwanza tokea Rais Putin atie saini sheria mpya wiki iliyopita, ya kuwezesha kuwapa watu adhabu ya kulipa faini kubwa zaidi ikiwa wanashiriki au wanaandaa upinzani ambao haukuruhusiwa.
Viongozi wa upinzani wamesema walioshiriki katika maandamano hayo walifikia watu laki moja, lakini polisi imesema walioshiriki walikuwa watu 20,000 Polisi waliopambana na waandamanaji waliompinga Putin mnamo mwezi wa Mei walikuwa katika hali ya tahadhari lakini hawachukua hatua yoyote safari hii.
Maandamano yalifanyika kwa muda wa saa sita na yalimalizika kwa amani . Maandamano hayo yamefanyika kwa mara ya kwanza tokea Rais Putin atie saini sheria mpya wiki iliyopita, ya kuwezesha kuwapa watu adhabu ya kulipa faini kubwa zaidi ikiwa wanashiriki au wanaandaa upinzani ambao haukuruhusiwa.
