Showing posts with label June 18. Show all posts
Showing posts with label June 18. Show all posts
JE ni Kweli Pesa za Kale Zina Nguvu za Kichawi?

JE ni Kweli Pesa za Kale Zina Nguvu za Kichawi?

Moja kwa moja utawaza kuhusu rupia(rupee ya mjerumani) na pesa nyingine za kale na yale yanayosemwa kuzihusu hasa kwenye habari nzima za kichawi
Watu wamezinguka na kuzinguliwa hasa watu wametapeliwa na wengine kufa wakitafuta hivi vitu vinavyotajwa kuwa na thamani kubwa
Ukweli huu hapa na si pesa tu bali na vitu vingine vya kale
1. Aina ya malighafi iliyotumika
Wakati huo vilitengenezwa vitu imara sana kutokana na upatikanaji wa malighafi ya kutosha …vitu kama vyombo vya bati na chuma urembo kama bangili mikufu pete nk leo hii ukivipata na kuviyeyusha kila kimoja unaweza kutengeneza kumi kupitia hicho kimoja
2. Uhifadhi
Wajerumani kwa hapa kwetu walikuta malighafi vito na madini ya kutosha sana! Kutokana na uhifadhi hafifu wakati huo vingi ya hivi vitu viliwekwa tu majumbani mwao wakiviandaa kuvidafirisha kwao
Vita ya pili ya 1939-45 iliwachanganya mno na walipoelekea kushindwa waliamua kuficha mali yote kwenye mashimo makubwa mashambani misituni kwenye mahandaki na milimani kusikofikika kwa urahisi kisha wakawaua watu karibia wote walioshiriki na wanaojua yale maficho wakasepa
Huku kote mali hizo zilihifadhiwa kwenye vyumba imara vilivyojengwa kwa zege gumu hasa ili iwe ngumu kuchimbua ama kuvunja na kama ni mapangoni yalikuwa mapango ya mbali hasa milimani na misituni
3. Dhana ya majoka na viumbe wa ajabu
Huko kwenye hayo maficho kuna baadhi ya watu walisalimika hivyo wakasimulia vizazi vilivyofuata
Kizazi cha kusaka utajiri wa haraka kikaona fursa na kuamua kuchangamkia dili. ..Wajerumani hawakuweka ulinzi wowote wa majoka! Hao ni viumbe tu walijitwalia makazi huko ambako ndio maisha yao yaliko
Watu walioenda bila tahadhari waliumwa na hayo madubwana na kupoteza maisha! Waliosalimika walitimua mbio na kuunda stories za kufikirika
4. Dhana ya uchawi na majini
Kwa wale waliosaka kwenye mahandaki na mashimo marefu yenye vyumba vilivyojengwa kwa zege , baada ya kufanikiwa kuvunja hayo mazege na kutaka kuingia ndani nao walikutana na mauzauza ya kila aina
Unajua ni kwa nini? Sehemu yoyote yenye mfumo wa nyumba ama chumba isiyokaliwa na binadamu roho zinazotangatanga na mapepo hufanya makazi yao kumbuka ile mada ya kutakasa makazi! Hivyo ukiingia huko lazima ukutane na vitu vya ajabu…Mjerumani hahusiki kabisa!
5. Uamuzi wa kufanya kafara ama tambiko kabla ya kuchimba ama kuingia pangoni
Wengi walitafuta waganga wa kienyeji kwenye hili na hawakufanikiwa. ..waliofanikiwa walifanikiwa kwa ujanja tuu….ukienda kwenye pango misituni ukachinja mnyama ukapiga manyanga automatically mkiondoka ile nyama italiwa na kuna wakati manyanga huleta kelele na kufukuza mnyama yoyote aliyeko pangoni…ndio maana baada ya kafara hamuingii siku hiyo hiyo bali kesho yake nk
Wale wa kwenye mashimo NA mahandaki ni ibada tu ya kuziomba roho ziondoke ama kuzifukuza kwa kutumia mitishamba na harufu wasizozipenda….mkikutana na roho korofi mtachezea kichapo mpaka muache kila kitu na kutimua mbio kali sana
6. Ukweli hasa ni UPI?
Baada ya vita ya pili kukoma na baadae Uhuru wajerumani walishindwa kurudi kwa ubabe hivyo wakatumia njia za kijanja kurudi
Unajua waliondoka na ramani zote kule mali zilikofichwa hivyo walirudi kuzichukua kwa njia ya kununua yale maeneo na kuyaendeleza kwa kujenga shule vyuo hospital nk ama miradi ya barabara ufugaji na kilimo
Kwa njia hii walichukua vyao kiulaini mno
7. Thamani na umaarufu wake ni UPI?
Vitu vya kale kwa wenzetu vina thamani kubwa sana….wenzetu wana utaratibu wa kuweka vituo vya antiques na kuchaji watalii pesa ndefu kuviangalia . kila kimoja kinakuwa kimeandikiwa historia yake. Kwa hiyo wakija huku kuvitafuta wengi huenda kuviuza kwenye hayo maduka kwa bei kali mno
8. Nguvu ya utajiri
Biashara imevamiwa , vitu vya kale haviwezi kukupa utajiri wa miujiza ..havina huo uwezo bali kuna baadhi kutokana na malighafi iliyotumika kuvitengeneza vina mvuto kwenye ulimwengu wa giza kama mabangili ya shaba
9. Usumbufu
Kuna watu wanawachezea wenzao shere na kuwasumbua bila sababu.. Miaka hiyo pesa ilitengenezwa kwa mpango maalum(nadhani hata sasa) na zilitengenezwa kwa miaka… Kuna miaka pesa hazikutengenezwa. Sasa mtu anakupa dili na kukuahidi kukupa pesa ndefu ukimletea rupee ya mwaka fulani Rupie_robo_DOA_1913.JPG
10. Hitimisho
Kuna baadhi ya sehemu kulikofichwa hizo mali wafichaji walinuizia ama kufanya mambo ya giza ili atakayejaribu kuchukua ama apate madhara au asizione kabisa…lakini kwa sehemu kubwa ni habari zilizotiwa chumvi nyingi

from Blogger http://ift.tt/2th6YV7
via IFTTT


JE ni Kweli Pesa za Kale Zina Nguvu za Kichawi?

JE ni Kweli Pesa za Kale Zina Nguvu za Kichawi?

Moja kwa moja utawaza kuhusu rupia(rupee ya mjerumani) na pesa nyingine za kale na yale yanayosemwa kuzihusu hasa kwenye habari nzima za kichawi
Watu wamezinguka na kuzinguliwa hasa watu wametapeliwa na wengine kufa wakitafuta hivi vitu vinavyotajwa kuwa na thamani kubwa
Ukweli huu hapa na si pesa tu bali na vitu vingine vya kale
1. Aina ya malighafi iliyotumika
Wakati huo vilitengenezwa vitu imara sana kutokana na upatikanaji wa malighafi ya kutosha …vitu kama vyombo vya bati na chuma urembo kama bangili mikufu pete nk leo hii ukivipata na kuviyeyusha kila kimoja unaweza kutengeneza kumi kupitia hicho kimoja
2. Uhifadhi
Wajerumani kwa hapa kwetu walikuta malighafi vito na madini ya kutosha sana! Kutokana na uhifadhi hafifu wakati huo vingi ya hivi vitu viliwekwa tu majumbani mwao wakiviandaa kuvidafirisha kwao
Vita ya pili ya 1939-45 iliwachanganya mno na walipoelekea kushindwa waliamua kuficha mali yote kwenye mashimo makubwa mashambani misituni kwenye mahandaki na milimani kusikofikika kwa urahisi kisha wakawaua watu karibia wote walioshiriki na wanaojua yale maficho wakasepa
Huku kote mali hizo zilihifadhiwa kwenye vyumba imara vilivyojengwa kwa zege gumu hasa ili iwe ngumu kuchimbua ama kuvunja na kama ni mapangoni yalikuwa mapango ya mbali hasa milimani na misituni
3. Dhana ya majoka na viumbe wa ajabu
Huko kwenye hayo maficho kuna baadhi ya watu walisalimika hivyo wakasimulia vizazi vilivyofuata
Kizazi cha kusaka utajiri wa haraka kikaona fursa na kuamua kuchangamkia dili. ..Wajerumani hawakuweka ulinzi wowote wa majoka! Hao ni viumbe tu walijitwalia makazi huko ambako ndio maisha yao yaliko
Watu walioenda bila tahadhari waliumwa na hayo madubwana na kupoteza maisha! Waliosalimika walitimua mbio na kuunda stories za kufikirika
4. Dhana ya uchawi na majini
Kwa wale waliosaka kwenye mahandaki na mashimo marefu yenye vyumba vilivyojengwa kwa zege , baada ya kufanikiwa kuvunja hayo mazege na kutaka kuingia ndani nao walikutana na mauzauza ya kila aina
Unajua ni kwa nini? Sehemu yoyote yenye mfumo wa nyumba ama chumba isiyokaliwa na binadamu roho zinazotangatanga na mapepo hufanya makazi yao kumbuka ile mada ya kutakasa makazi! Hivyo ukiingia huko lazima ukutane na vitu vya ajabu…Mjerumani hahusiki kabisa!
5. Uamuzi wa kufanya kafara ama tambiko kabla ya kuchimba ama kuingia pangoni
Wengi walitafuta waganga wa kienyeji kwenye hili na hawakufanikiwa. ..waliofanikiwa walifanikiwa kwa ujanja tuu….ukienda kwenye pango misituni ukachinja mnyama ukapiga manyanga automatically mkiondoka ile nyama italiwa na kuna wakati manyanga huleta kelele na kufukuza mnyama yoyote aliyeko pangoni…ndio maana baada ya kafara hamuingii siku hiyo hiyo bali kesho yake nk
Wale wa kwenye mashimo NA mahandaki ni ibada tu ya kuziomba roho ziondoke ama kuzifukuza kwa kutumia mitishamba na harufu wasizozipenda….mkikutana na roho korofi mtachezea kichapo mpaka muache kila kitu na kutimua mbio kali sana
6. Ukweli hasa ni UPI?
Baada ya vita ya pili kukoma na baadae Uhuru wajerumani walishindwa kurudi kwa ubabe hivyo wakatumia njia za kijanja kurudi
Unajua waliondoka na ramani zote kule mali zilikofichwa hivyo walirudi kuzichukua kwa njia ya kununua yale maeneo na kuyaendeleza kwa kujenga shule vyuo hospital nk ama miradi ya barabara ufugaji na kilimo
Kwa njia hii walichukua vyao kiulaini mno
7. Thamani na umaarufu wake ni UPI?
Vitu vya kale kwa wenzetu vina thamani kubwa sana….wenzetu wana utaratibu wa kuweka vituo vya antiques na kuchaji watalii pesa ndefu kuviangalia . kila kimoja kinakuwa kimeandikiwa historia yake. Kwa hiyo wakija huku kuvitafuta wengi huenda kuviuza kwenye hayo maduka kwa bei kali mno
8. Nguvu ya utajiri
Biashara imevamiwa , vitu vya kale haviwezi kukupa utajiri wa miujiza ..havina huo uwezo bali kuna baadhi kutokana na malighafi iliyotumika kuvitengeneza vina mvuto kwenye ulimwengu wa giza kama mabangili ya shaba
9. Usumbufu
Kuna watu wanawachezea wenzao shere na kuwasumbua bila sababu.. Miaka hiyo pesa ilitengenezwa kwa mpango maalum(nadhani hata sasa) na zilitengenezwa kwa miaka… Kuna miaka pesa hazikutengenezwa. Sasa mtu anakupa dili na kukuahidi kukupa pesa ndefu ukimletea rupee ya mwaka fulani Rupie_robo_DOA_1913.JPG
10. Hitimisho
Kuna baadhi ya sehemu kulikofichwa hizo mali wafichaji walinuizia ama kufanya mambo ya giza ili atakayejaribu kuchukua ama apate madhara au asizione kabisa…lakini kwa sehemu kubwa ni habari zilizotiwa chumvi nyingi

from Blogger http://ift.tt/2sEsFk3
via IFTTT


WASIFU WA RAIS WA TANZANIA, DKT JOHN POMBE MAGUFULI

WASIFU WA RAIS WA TANZANIA, DKT JOHN POMBE MAGUFULI

Maisha ya utotoni.
Jina lake kamili ni John Pombe Joseph Magufuli, kwa kabila yeye ni Msukuma na dini yake ni Mkristo. Alizaliwa Oktoba 29, 1959 Wilayani Chato Mkoa wa Kagera ambayo hivi sasa ipo Mkoa wa Geita.
Elimu
John Pombe Joseph Magufuli alianza elimu yake ya msingi katika Shule ya Msingi Chato kuanzia mwaka 1967 na kuhitimu mwaka 1974. Baada ya hapo alijiunga na Seminari ya Katoke iliyopo Biharamulo kwa ajili ya elimu yake ya sekondari iliyoanza mwaka 1975 hadi 1977 na baadae akahamia Shule ya Sekondari Lake mwaka 1977 na kuhitimu 1978.
John Magufuli alijiunga na Shule la Sekondari Mkwawa iliyopo mkoani Iringa kwa ajili ya masomo ya kidato cha tano na sita tangu mwaka 1979 na kuhitimu mwaka 1981 na mwaka huo aliohitimu akajiunga na Chuo cha Ualimu cha Mkwawa akasoma Diploma ya Ualimu katika masomo ya Chemistry na Hisabati.
John Pombe Joseph Magufuli (sasa Dkt na Rais wa #Tanzania), Shule ya Seminari Katoke, 1970s.
Mwaka 1988, John Magufuli alitunukiwa Shahada yake ya kwanza ya Ualimu akiwa amesomea masomo ya Chemistry na Hisabati kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) baada ya kuwa alijiunga chuoni hapo mwaka 1985. Mwaka 1994 John Magufuli alitunukiwa Shahada ya Uzamivu (Masters Degree) na mwaka 2009 akatunukiwa Shahada ya Umahiri (PhD) zote katika somo la Chemistry kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).
Rais John Pombe Magufuli akiwa mwanafunzi wa Shahada ya Umahiri ya Kemia (Masters Degree) katika Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam miaka ya mwanzo ya 1990.
Siasa na kazi
John Magufuli alijiingiza kwenye siasa kati ya mwaka 1982 na 1983 baada ya kuwa amefundisha kwa muda mfupi katika Shule ya Sekondari Sengerema mkoani Mwanza. Baadae aliacha Ualimu na kuajiriwa katika Chama cha Ushirika Nyanza kama Mkemia wa Chama hicho. Alifanya kazi hiyo kuanzia 1989 hadi mwaka 1995 alipochaguliwa kuwa Mbunge wa Jimbo la Chato kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM) ukiwa ndio uchaguzi wa kwanza tangu kuanzishwa mfumo wa vyama vingi nchini.
Rais wa awamu ya tatu Mzee Benjamin Mkapa akimnadi Mgombea Ubunge Dkt Magufuli, jimbo la Biharamulo (East).
Baada ya kuingia Bungeni mwaka 1995 aliteuliwa kuwa Naibu Waziri wa Wizara ya Ujenzi ambapo alitetea kiti chake cha ubunge mwaka 2000 na kuteuliwa kuwa Waziri wa Wizara ya Ujenzi chini ya Rais wa Awamu ya Tatu, Mzee Benjamin William Mkapa.
Tarehe 4 Januari 2006 baada ya Rais wa Awamu ya nne, Dkt Jakaya Kikwete kuingia madarakani, alimteua John Magufuli kuwa Waziri wa ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi. Kuanzia 13 Februari 2008 hadi 6 Novemba 2010, John Magufuli alikuwa Waziri wa Kilimo na Uvuvi, ilipofika 2010 aliteuliwa tena kuwa kuwa Waziri wa Ujenzi.
Mwaka 1995, Mama Anna Abdallah alimpokea na kumfundisha kazi kama Naibu Waziri wake wizara ya Ujenzi John Pombe Magufuli.
Mbio za urais.
Baada ya kuchukua fomu ya kutaka kugombea urais kama ulivyoutaratibu ndani ya CCM, Julai 15, 2015 John Magufuli alitangazwa kuwa mgombea wa urais wa CCM baada ya kuwashinda wapinzani wake akiwemo Asha-Rose Migiro, Amina Salum Ali, Benard Membe.
Katika mbio za urais, John Magufuli alikumbana na upinzani mkubwa kutoka kwa mgombea wa CHADEMA, Edward Lowassa na baada ya wananchi kupiga kura Oktoba 25, Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) ilimtangaza John Magufuli kuwa mshindi Oktoba 29, 2015 baada ya kujizolea kura asilimia 58% ya kura zote halali.
Dkt John Pombe Magufuli akila kiapo kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Novemba 5, 2015.
John Magufuli aliapishwa kuwa Rais wa awamu ya tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Novemba 5, 2015 katika Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.
Urais.
Akitimiza mwaka mmoja tangu aingie madarakani, Rais Dkt. JohnPombe Joseph Magufuli amekuwa akigonga vichwa vya habari vya kitaifa na kimataifa mara kwa mara kutokana na kauli mbiu yake ya Hapa Kazi Tu. Rais Magufuli amejikita katika kupiga rushwa vita, kuhakikisha anabana matumizi ya serikali ili fedha hizo ziweze kutumika katika miradi ya maendeleo ikiwa ni pamoja na ujenzi au ukarabati wa viwanda.
Kutilia mkazo kwenye hilo, Rais Magufuli alifuta sherehe za sikukuu ya Uhuru, sherehe za sikukuu ya Muungano, amezuia viongozi wa umma kusafiri nje ya nchi bila kuwa ni kibali maalum, aliagiza kupunguzwa kwa gharama za sherehe ya ufunguzi wa Bunge, ameagiza mikutano na semina zifanyika katika kumbi za majengo ya umma.
Maisha binafsi.
Rais Magufuli ameoa mke mmoja, Janeth Magufuli ambaye alikuwa Mwalimu katika Shule ya Msingi Mbuyuni jijini Dar es Salaam na wana watoto watatu.
Dkt John Magufuli na mkewe Janeth Magufuli mwanzoni mwa miaka ya tisini.

from Blogger http://ift.tt/2sphQjX
via IFTTT


KUTOA MBEGU ZA KIUME ANGALAU MARA 21 KWA MWEZI HUPUNGUZA HATARI YA KUPATA KANSA YA TEZI DUME

KUTOA MBEGU ZA KIUME ANGALAU MARA 21 KWA MWEZI HUPUNGUZA HATARI YA KUPATA KANSA YA TEZI DUME

Kwa mwanaume unayehofia kuja kupata saratani ya tezi dume, kuna hatua angalau moja rahisi unayoweza kuichukua kukukinga dhidi ya hatari hii, na urahisi wake ni kutokana na kujiondolea hatari ya kupata ugonjwa mkubwa kiasi hiki ukiwa chumbani kwako tu.
Tafiti nyingi zimehusisha utoaji wa mara kwa mara wa mbegu za kiume (manii) — kwa kufanya mapenzi, kupiga punyeto au ukiwa usingizini — na kupunguza kwa kiasi kikubwa hatari za kupata saratani ya tezi dume.
Jambo hili linaweza kuleta tofauti kiasi gani?
Kwa mujibu wa tafiti iliyochapishwa mwaka 2016 kwenye jarida la European Urology, tofauti ya kufanya na kutofanya hivi ni kubwa sana.
Wanaume 32,000 walifanyiwa utafiti kuanzia mwaka 1992 mpaka mwaka 2010 na matokeo waliyoyapata ni kwamba wanaume waliripoti kumwaga mbegu za kiume angalau mara 21 kwa mwezi walipokuwa na umri wa miaka ya 20 (20’s) maishani mwao walikuwa na asilimia 19 zaidi ya kutokutwa na saratani ya tezi dume ikilinganishwa na wale waliokuwa wakimwaga mara saba tu kwa mwezi mzima au chini ya hapo.
Kumwaga mbegu za kiume mara kwa mara ukiwa kati ya miaka ya 40 (40’s) pia inakupunguzia hatari ya kupata saratani ya tezi dume kwa asilimia 22, utafiti huo umeonesha.
“Ingawa matokeo ya utafiti wetu inabidi yathibitishwe na tafiti zinazochambua utendaji kazi wa kibaiolojia, bado matokeo haya yanasema kuwa kutoa mbegu za kiume na kufanya ngono salama katika ujana wako wote yawezekana ikawa ni mbinu yenye manufaa makubwa kwa mwanaume katika kupunguza hatari ya kupata saratani ya tezi dume,” amesema Jennifer Rider, kiongozi wa utafiti huo katika mkutano na waandishi wa habari.
Hakuna idadi maalumu kwa mwezi ambayo mwanaume anatakiwa anamwaga mbegu ili kupunguza hatari hiyo. Kilichobainishwa kutokana na utafiti huu ni kwamba huwa inategemea sana na mahusiano ya kingono kati ya wapenzi ambapo hatari ya kupata saratani hii inapungua sana endapo mwanaume anapata fursa ya kutoa mbegu za kiume mara nyingi zaidi.
Hii si mara ya kwanza kwa watafiti kuendesha utafiti kubaini ni kwa jinsi gani kutoa mbegu za kiume kuna uhusiano na kupunguza hatari za kupata saratani ya tezi dume. Mwaka 2003 timu ya watafiti wa nchini Australia walilinganisha idadi ya mwanaume kumwaga mbegu za kiume kwenye utafiti uliohusisha wanaume 2,300 — ambao nusu yao walibainika kuwa na saratani ya tezi dume. Matokeo yalionesha kuwa wale waliotoa mbegu za kiume mara tano hadi saba kwa wiki walipunguza hatari ya kupata saratani ya tezi dume kwa asilimia 36 wakilinganishwa na wale waliomwaga mara mbili au pungufu ya hapo kwa wiki.
Ingawa tafiti hizi zimekuwa zikileta matokeo yanayofanana, watafiti bado hajapata sababu maalumu ya kwa nini kumwaga mbegu za kiume mara kwa mara kunapunguza kwa kiasi kikubwa hatari za mwanaume kupata saratani hii.
Jennifer Rider aliliambia Shirika la habari la Reuters kuwa timu yake ilikuja na dhana moja inayoelezea uhusiano huo: kwamba “Utoaji wa mbegu za kiume mara kwa mara, kwa kiasi fulani, ni kielelezo cha afya bora kwa mwanaume kwa sababu wanaume waliobainika kumwaga mbegu mara chache zaidi kwenye utafiti wao — ambao hawakumwaga kabisa au walimwaga chini ya mara tatu kwa mwezi mzima — walikuwa na uwezekano mkubwa sana wa kukutwa na magonjwa mengine na pia walikufa mapema kutokana na sababu mbalimbali zaidi ya saratani ya tezi dume. Pamoja na matokeo haya, tafiti zaidi zinatakiwa kufanyika ili kuelezea uhusiano wa kibaiolojia unaohusika kupunguza hatari hii.”
 ASANTE KWA KUTEMBELEA MTANDAO WETU!!

from Blogger http://ift.tt/2rtvzok
via IFTTT


MADHARA YA KIAFYA YA KUVAA NGUO ZA KUBANA

MADHARA YA KIAFYA YA KUVAA NGUO ZA KUBANA

Kwa msaada wa viguo vya kubana na vivazi vyote vinavyochonga shepu ya mwili, wengi mchana huonekana na maumbile mazuri yanayovutia kuangalia na usiku wanarudi kwenye miili yao iliyotepweta baada ya kuzivua nguo zao.
Hatuoni tabu yoyote hata kujipaka mafuta ikibidi mradi tuweke kuingia kwenye jinzi za kubana au hata kuvaa ‘skini taiti’ mbili, vyovyote iwavyo ili mradi tuonekane wembamba kuliko tulivyo, tuonekane wazuri na wenye mvuto kuliko tulivyo na nyakati nyingine kwakuwa tunataka tuonekane vijana kuliko tulivyo.
Kama unaihusudu sana jinzi yako ya kubana, bila shaka ushawahi kupata tatizo la mwili kupatwa na ganzi kuanzia mapajani na kupoteza hisia kabisa kwenye mguu mzima mpaka chini. Madaktari wanaiita hali hii kwa jina la kitaalamu la meralgia paresthetica ambayo hutokea kwa sababu ya kukandamiza kwa muda mrefu mishipa ya neva za fahamu inayotoka kwenye kiunoni ambayo kazi yake ni kuleta hisia kwenye mapaja.
Mwili wa binadamu unatoa ishara fulani kama nguo au mapambo fulani tuliyovaa yanabana sana hata kama tukijidai kudharau tunayoyaona kwa macho yetu kupitia kioo ukiwa unajikagua kama umependeza ama la. Yafuatayo ni baadhi tu ya madhara ya kiafya unayoweza kuyapata kutokana na kuvaa nguo zinazobana mwili:
Ugumba
Dkt. George Bwesigye, daktari katika hospitali ya Najeera anatoa maelezo ambayo yanaweza kuwatisha wanaume wengi. “Kokwa zinazotengeneza mbegu za kiume zinatakiwa ziwe kwenye joto la chini tofauti na joto la mwili, ndio sababu zikawa nje ya mwili. Kwa hali hii, zinakuwa na uwezo wa kuzalisha mbegu za kiume kwa wingi. Kwahiyo, kuzibana na nguo kunazuia au kupunguza kwa kiasi kikubwa kazi yake hii ya msingi na huweza kusababisha ugumba.”
Maambukizi
Anasema kuwa chupi zinazobana husababisha joto linaloleta unyevu kwenye eneo hilo nyeti. Unyevu katika sehemu hiyo husababisha vjidudu vya fangasi kwa wanaume au utandu wa vijidudu unaosababisha muwasho na maambukizi kwa wanawake.
Mzunguko mdogo wa damu
Nguo za kubana zinazuia mzunguko unaotakiwa wa damu, ikizuia mzunguko wake wa kawaida wa kupeleka damu na kuirudisha kwenye moyo kwa ajili ya kutumika tena mwilini.
Hili linaleta maumivu, uvimbe au kuvimba/kupinda kwa mishipa ya damu ya miguu kutokana na presha kubwa inayopelekwa sehemu ya chini ya mwili. Kama una tatizo la kuwa na mafuta mengi mwilini, kuvaa nguo za kubana kunaliongeza tatizo hilo kwakuwa mzunguko wako wa damu utaathirika zaidi.
Matatizo ya mmeng’enyo wa chakula
Bwesigye anaendelea kueleza kuwa suruali na mikanda ambavyo vinabana sana tumbo vinakuwa vinalizuia tumbo kutanuka jambo ambalo ni la muhimu sana kwa ajili ya usagaji wa chakula ulichokula.
“Kwakuwa mfumo wa usagaji chakula haufanyi kazi sawa sawa, mtu atajikuta anapata viungulia na kujaa kwa kemikali tumboni, na matatizo mengine mengi,” amesema.
Maambukizo ya njia ya mkojo (UTI)
Mbunifu wa mavazi kwa watu mashuhuri, Solomon Tazibone amesema kuwa wanawake wanaovaa nguo za kubana mara nyingi sana hukwepa kutumia vyoo vya kadamnasi, ambavyo vinahatarisha wanawake wengi sana kupata maambukizi ya njia ya mkojo.
“Si rahisi kutua nguo zilizokubana sana hasa kwenye vyoo vinavyotumiwa na watu wengi. Kwahiyo wanawake wengi hujikuta wakizuia haja ndogo kwa saa kadhaa wakisubiri kwenda sehemu walizozizoea na salama kwao kama majumbani mwao,” anasema.
“Tatizo kubwa zaidi ni pale nguo hizi zinapovaliwa na mabinti wadogo. Tunaweza tukabisha lakini hali halisi ni kwamba wanaume wanapenda kuona vitu vinavyowavutia na hawatasita kumuita mtoto wa miaka 11 aliyevaa kaptura au hata kumuangalia kwa matamanio.
Kama wazazi ni jukumu lenu kuwalinda watoto wenu hata kama utaitwa mshamba au mkoloni.
 ASANTE KWA KUTEMBELEA MTANDAO WETU!!

from Blogger http://ift.tt/2sDCO0G
via IFTTT


SEHEMU 9 ZA KUTALII UKIWA JIJINI DAR ES SALAAM

SEHEMU 9 ZA KUTALII UKIWA JIJINI DAR ES SALAAM

Umaarufu wa Dar es Salaam kwenye shughuli za kibiashara umelifanya jiji hili kuwa vigumu kwa watu kuvizingatia vivutio vyake vya kitalii. Watu wengi huvifahamu kwa kuviona tu lakini bila ya kujua kihistoria sehemu hizo zina maana sana na wageni huja wakitokea nchi mbalimbali kujifunza.
Ukiachana na ufukwe wa Coco Beach unaopatikana pembezeni mwa bahari ya hindi eneo la Oyster Bay, Jumia Travel ingependa kukufahamisha kwamba unaweza kujifunza na kufurahia mambo mengi pindi utakapotembelea maeneo yafuatayo.
Makumbusho ya Taifa na Nyumba ya Utamaduni. Makumbusho haya awali yalifunguliwa mwaka 1940 kama kumbukumbu ya Mfalme George wa tano ambapo kihistoria huwarudisha watanzania nyuma walipotokea. Makumbusho haya huonyesha mabaki muhimu ya binadamu wa kale yaliyogunduliwa na Dkt. Leakey aliyoyachimbua kwenye bonde la Olduvai. Wageni wanaweza kujifunza urithi wa kitamaduni kutoka kwa makabila mbalimbali Tanzania pamoja na athari za biashara ya utumwa kipindi cha utawala wa kikoloni. Baadhi ya vitu vingine vinavyopatikana katika makumbusho haya yaliyopo mtaa wa Shaaban Roberts ni zana za jadi, desturi, mapambo na vyombo vya muziki.
Kijiji cha Makumbusho. Takribani maili 6 kutokea katikati ya jiji, kuna kijiji cha makumbusho ambacho kimehifadhi tamaduni za makabila zaidi ya 120 yanayopatikana Tanzania. Wageni wanaweza kuzunguka kwenye vibanda kadhaa vya nyasi vinavyopatikana pale kwenye ukbwa wa takribani hekari 15 na kujionea ufundi wa kijadi katika kuchora, ufumaji na uchongaji. Kijiji hiki kinachopatikana eneo la Kijitonyama, barabara ya Bagamoyo pia huwa na ngoma na michezo ya jadi pamoja shughuli nyingize za kitamaduni.
Sanamu la Askari. Likiwa limetengenezwa kwa shaba sanamu hili ya Askari huonyesha askari akiwa amevalia vazi rasmi lililotumika kipindi cha vita ya Kwanza ya Dunia huku ncha ya mbele ya bunduki (kama kisu) ikiwa imeelekezwa karibu na bandari iliyopo jirani. Sanamu hili huonyesha kama kumbukumbu ya majeshi ya waafrika walioshiriki kupigana kwenye vita ya Kwanza ya Dunia na linapatikana mtaa wa Azikiwe na Samora.
Boma la Kale. Likiwa limejengwa mnamo mwaka 1866 mpaka 1867 na Majid Bin Said, Sultani wa Zanzibar, Boma hili la kale ni jengo lenye umri zaidi ambalo linapatikana kwa sasa jijini Dar es Salaam. Jengo hili lilitumika kuwakarabisha wageni wa Sultani ambaye alikuwa na kasri lake pembeni yake. Vitu vya kuvutia kwenye jengo hili lililopo mtaa wa barabara ya Sokoine ni namna lilivyojengwa kwa ndani vikiwemo mlango wa mbao kutokea Zanzibar na kuta zilizojengwa kutokana na matumbawe.
Kanisa la Mtakatifu Joseph. Jengo hili la Kanisa la Kiroma lilijengwa na wamisionari wa Kijerumani mnamo mwaka 1897 mpaka 1902, kwa kiasi kikubwa ni kivutio kinachoweza kuonekana eneo la karibu na bandarini. Jengo hili kwa ndani limejengwa kwa ufundi na ubunifu wa hali ya juu na kutumia stadi halisi kabiza za kijerumani. Jengo hili ndio Makao Makuu ya kanisa hilo na liinapatikana katika barabara ya Sokoine.
Kanisa la KKKT Azania Front. Wajerumani walilijenga kanisa la KKKT Azania Front mnamo mwaka 1898. Namna jengo hili lilivyojengwa hususani paa lake kunalifanya kuwa ni nembo ya kivutio jijini Dar es Salaam. Kuna kipindi kanisa hili ndilo lilikuwa kituo kikuu cha shughuli za kimisionari mnamo karne ya 19, kwa sasa ndio makao makuu ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania.
Ikulu. Ikiwa imejengwa kwenye miaka ya 1890, jengo la Ikulu ndilo lilikuwa ni makazi ya mwanzo kabisa ya Gavana wa Ujerumani. Mnamo mwaka 1922, Waingereza walifanya maboresho ya jengo hilo maeneo mbalimbali kufuatia kuliharibu katika kipindi cha vita ya Kwanza ya Dunia. Ingawa raia wa kawaida hawawezi kuingia ndani lakini bado linabaki kuwa kivutio kikubwa mtu akipita karibu nalo. Jengo hili linapatikana mtaa wa Luthuli barabara ya kuelekea Kivukoni.
Kisiwa cha Mbudya. Kisiwa hiki kinapatikana umbali wa dakika kumi kwa mwendo wa boti kutokea Kunduchi kikiwa ni hifadhi ya majinii jijini Dar es Salaam. Ukiwa kisiwani hapa utasahau kabisa pilikapilika za katikati mwa jiji hili kwa kufurahia fukwe safi, michezo ya kwenye maji na kuogelea. Kisiwani haoa kuna vibanda vya kukodisha karibu na ufukwe huku vyakula vya baharini pamoja vinywaji vikipatikana pia. Sehemu hii ni maarufu sana kwa watu wanaopenda kutalii kwa siku moja wakitokea katikati ya jiji.
Kisiwa cha Bongoyo. Takribani maili 4 Kaskazini mwa jiji la Dar es Salaam eneo la Msasani kinapatikana kisiwa cha Bongoyo. Kwa wale wanaopenda kusafiri kwa siku moja na kurudi hii sehemu pekee na ya kuvutia ambayo unaweza kufurahia mambo mengi. Kisiwa kina fukwe safi, michezo ya kwenye maji, pamoja na kujionea aina kadhaa za samaki wa baharini. Nyuma ya kisiwa hiki kuna mibuyu mikubwa ambayo huleta hewa safi kwenye fukwe za kisiwa hiko huku vyakula vya baharini na vinywaji hupatikana kwa ajili ya wanaotembelea. Bongoyo kwa sasa inawezekana kuwa ni miongoni mwa visiwa vinne vinavyotembelewa zaidi kwenye hifadhi za maji jijini Dar es Salaam.
Dar es Salaam ina mambo mengi ya kujifunza ingawa mengi yamezingwa na shughuli za kibiashara zilizotapakaa kila kona. Jumia Travel inaamini kuwa inawezekana unaishi na vivutio vya kitalii karibu nawe lakini ulikuwa haufahamu. Hivyo basi kabla ya kufikiria kwenda mbali kutalii vivutio vingine anza na vilivyomo jijini hapa kwani vipo karibu nawe na haikugharimu sana kuvitembelea.
 ASANTE KWA KUTEMBELEA MTANDAO WETU!!

from Blogger http://ift.tt/2rsG8bv
via IFTTT


Kategori

Kategori