Showing posts with label June 11. Show all posts
Showing posts with label June 11. Show all posts
Vincent Bossou: Timu 4 zimempa Ofa,Ikiwemo Hii Moja kutoka Tanzania

Vincent Bossou: Timu 4 zimempa Ofa,Ikiwemo Hii Moja kutoka Tanzania

Bossou ambaye anatarajia kwenda Dubai kwa mapumziko ya Siku 10, amethibitisha kuwa kuna Timu 4 zinamwitaji ikiwemo Singida United na Timu 3 Ulaya.
“Nimepata ofa nchi tatu, kama mambo yataenda vizuri nikitoka Dubai nitaunganisha kwenda Uturuki kufanya mazungumzo ila kwa sasa siwezi kukutajia kwa sababu bado mapema sana,” alisema Bossou.
“Kwa Tanzania nimepata ofa Singida United, wenyewe wako tayari kunipa fedha nzuri, ikiwemo dau la usajili na mshahara mnono, hivyo mambo yakiwa magumu nitarudi kuwasikiliza,”
ASANTE KWA KUTEMBELEA MTANDAO WETU!!

from Blogger http://ift.tt/2sheGBs
via IFTTT


Bajeti 2017/18 inaenda kuwagusa wengi -Dkt Kigwangalla

Bajeti 2017/18 inaenda kuwagusa wengi -Dkt Kigwangalla

Naibu waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na watoto, Dkt Hamisi Kigwangalla amesema katika miaka yake 7 ya uwakilishi bungeni hajawahi kushuhudia bajeti ikishangiliwa kama ya Wizara ya Fedha huku akisema bajeti hiyo inaenda kuwagusa watu wengi.
Dkt Kigwangalla ametumia ukurasa wake wa Instagram kuisifia bajeti hiyo.
Katika miaka yangu saba ya uwakilishi #Bungeni sijawahi kushuhudia bajeti ikishangiliwa na wabunge kama ya jana. Kwa hakika bajeti ya 2017/18 inaenda kuwagusa watu wengi, kuanzia wakulima wetu wadogo wadogo hadi wakubwa hadi wenye viwanda vyenye fungamanisho na kilimo; wachimbaji wadogo hadi wakubwa. Kila mtu ameguswa. Dr. Mpango amekuja akiwa amejipanga haswa, kwa niaba ya Serikali yetu nzima. Michango mingi ya Wabunge na Mawaziri ameizingatia sana. Naamini huu usikivu ndiyo sababu ya bajeti kupendwa na kushangiliwa kiasi hicho. Kwa hakika itapita bila shida. Tutabaki na kazi ya kufanya kazi kwa bidii kuitekeleza. #bajeti #Bajeti2017 #HK #HamisiKigwangalla #Dr_Kigwangalla #SiasaNiVitendo
Juzi Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Philip Mpango aliwasilisha bungeni mapendekezo ya makadirio ya bajeti ya serikali kwa mwaka 2017/18.
ASANTE KWA KUTEMBELEA MTANDAO WETU!!

from Blogger http://ift.tt/2rZZJAU
via IFTTT


Mtoto naye akawa kwenye hali mbaya, tukamkimbiza kituoni, akafa siku tunazika akaanza mama naye akafa

Mtoto naye akawa kwenye hali mbaya, tukamkimbiza kituoni, akafa siku tunazika akaanza mama naye akafa

Watu watatu wa familia moja wakazi wa Kijiji cha Nyantira wilayani hapa mkoani Mara wanadaiwa kufariki katika mazingira ya kutatanisha huku wanannchi wakihusisha vifo hivyo na ulaji wa asali.
Kaimu Kamanda wa Mkoa wa Polisi Tarime, Rorya, Sweetbert Njewike akizungumza kwa simu akiwa Shirati wilayani Rorya, amesema hana taarifa hiyo ofisini kwake.
Mwenyekiti wa kijiji cha Nyantira, James Chacha amesema tukio hilo lilitokea kati ya Juni 7, 8 na 9 na kuzua taharuki kijijini hapo kutokana na aina ya vifo vya wanafamilia hao watatu kufariki kwa kufuatana.
Amewataja waliofariki kuwa ni Kerato Nyangerela (70), Regina Kerato (50) na Samwel Kerato (12) ambaye ni mwanafunzi wa darasa la tatu Shule ya Msingi Nyantira.
Chacha amesema, “Juni 7 tulizika mzee baada ya kumkimbiza Kituo cha Afya, Muriba, baada ya saa 12 akafariki, tukamleta nyumbani kuzika, tulipomaliza maziko mtoto naye akawa kwenye hali mbaya, tukamkimbiza kituoni, akafa siku tunazika akaanza mama naye akafa pia,” alisema.
Ameongeza kuwa kufariki kwa watu hao kwa mfuatano kijiji kumeibua hali ya wasiwasi na huzuni hasa kwa kuwa wameacha watoto wadogo.
Akizungumzia vifo hivyo, Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Tarime, Mkumbo Odari alisema,”asali kama asali haina madhara kwenye mwili wa binadamu isipokuwa pale inapokuwa imechanganyika na sumu ndipo inapoweza kuleta madhara, na ndiyo maana asali inatumiwa kama dawa, kwenye chakula na kupaka kwenye mikate,” alibainisha Odari.
Naye Diwani wa Kata ya Nyansicha, Sunday Magacha alisema hadi sasa chanzo cha vifo vya wanafamilia hao hakijajulikana na uchunguzi bado unaendelea ili kufahamu chanzo licha ya kuwa uchunguzi wa awali uliofanywa na kituo cha afya Muriba ulionyesha kuwa walikuwa wamekula sumu.
Alisema tukio hilo lilikuwa la kwanza na la aina yake ambalo limewaacha wananchi wakiwa wameathirika kisaikolojia.
ASANTE KWA KUTEMBELEA MTANDAO WETU!!

from Blogger http://ift.tt/2sbfWoQ
via IFTTT


Watuhumiwa wa kesi za udhalilishaji sasa kunyimwa dhamana

Watuhumiwa wa kesi za udhalilishaji sasa kunyimwa dhamana

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Katiba Sheria Utumishi wa Umma na Utawala bora Mhe. Haroun Ali Suleiman amesema kutokana na kuongezeka vitendo vya udhalilishaji Zanzibar kwa wanawake na watoto, endapo serikali kupitia taasisi zake zinazoshughulikia kesi za udhalilishaji itamkamata mtu yoyote na kesi za udhalilishaji haitampa dhamana mtuhumiwa wa vitendo vya udhalilishaji.
Akizungumza na Waandishi wa Habari huko ofisini kwake mazizini wakati akitaja vipaumbele vya wizara yake kwa mwaka 2017/2018 amesema jitihada mbalimbali zinachukuliwa kuhakikisha kesi za udhalilishaji zinapungua Zanzibar na moja wapo ni ya kuwanyima dhamana watuhumiwa ili kutoa fundisho kwa wengine na kuimarisha utowaji wa haki.
ASANTE KWA KUTEMBELEA MTANDAO WETU!!

from Blogger http://ift.tt/2r7zC9S
via IFTTT


Kategori

Kategori