Showing posts with label Italia. Show all posts
Showing posts with label Italia. Show all posts

Kanisa Katoliki Sasa Kuvunja Ndoa


KIONGOZI wa Kanisa Katoliki Duniani, Papa Francis jana alieleza mabadiliko mapya yanayolenga kuwarahisishia Wakatoliki kuvunja ndoa zao na kuoa upya.

Dhamira hiyo ni ishara nyingine ya dhamira ya Papa huyo kutaka kulifanya Kanisa Katoliki liwe rafiki zaidi na kuendana matakwa ya walio wengi.

Akizungumza kuhusu mabadiliko hayo, Papa alisema si haki kwa wenzi kuishi muda mrefu ‘wakikandamizwa na wingu la shaka’ kuhusu uhalali wa ndoa zao.

Ikumbukwe kwamba ni msimamo wa Papa kumkatalia Mfalme Henry the VIII wa Uingereza kumtaliki mkewe Catherine wa Aragon katika karne ya 16 uliosababisha England ijitenge na Rome na kushuhudia kuundwa kwa Kanisa la England huku mfalme akiwa mlinzi wa Imani wa kanisa hilo.

Mabadiliko makuu matatu aliyotangaza  Papa jana ni   kuondoa mchakato wa mapitio ya mara ya pili wa uamuzi wa kutoa talaka kupitia mahakama ya kanisa kabla ya ndoa kuvunjwa.

Mengine ni kuwapatia maaskofu uwezo wa kuharakisha na kuvunja ndoa   wenzi wanapoamua wenyewe katika mazingira fulani kama vile ukatili katika ndoa au uasherati na mchakato huo wa talaka kuwa bure, isipokuwa kwa kulipa ada ndogo kwa ajili ya gharama za  utawala.

Kabla ya sheria hiyo, Wakatoliki waliotaka talaka walihitaji kibali kutoka kwa mahakama mbili za kanisa, wakati sheria mpya inabakiza moja ingawa rufaa bado zinaruhusiwa.

Kabla ya sheria hiyo, wanandoa wa Wakatoliki wanaotalikiana bila idhini ya kanisa na kuolewa upya walihesabiwa kama wazinifu na hawakuruhusiwa kupokea komunio.

Lakini kwa mujibu wa  utaratibu mpya, wanaotalikiana wakioa au kuolewa tena watabakia kuwa wafuasi wa kanisa hilo.

Mwaka jana Papa aliunda tume ya wanasheria wa kanisa hilo  kuboresha na kurekebisha taratibu hizo  kurahisisha wanandoa kuachana na kupunguza gharama.

Mageuzi hayo yalikuja katika mfumo wa nyaraka mbili zinazoitwa ‘motu proprio’, neno la kilatini lililobuniwa na Papa mwenyewe.

Taratibu hizo zitakuwa rasmi kama sehemu ya sheria za kanisa (canon law) ifikapo Desemba 8 mwaka huu wakati Papa atakapoanza kutangaza Mwaka wa Jubilee ambao kwa kawaida huhusishwa na msamaha.
Mpekuzi blog
Meli yatelekezwa Italia

Meli yatelekezwa Italia

Walinzi wa Pwani ya Italia wamesema Meli ya Kibiashara iliyokuwa na wahamiaji wapatao 400 inaelekea kwenye Pwani ya nchi hiyo.
Meli hiyo, Ezadeen iliyokuwa ikisafiri kwa bendera ya Sierra Leone haikuwa na wafanyakazi ndani yake na imepoteza mwelekeo kwenye bahari yenye mawimbi makali Kusini Mashariki mwa Italia.
Meli za Italia zimekuwa zikitoa msaada kuwasaidia watu waliokuwa ndani ya Meli hiyo. Zaidi ya wahamiaji elfu moja wameokolewa na kuwekwa kwenye meli nyingine.
Meli hiyo ilitelekezwa bila ya wafanyakazi wala nahodha mapema wiki hii.
 Berlusconi atimuliwa bungeni Italia

Berlusconi atimuliwa bungeni Italia



Silvio Berlusconi

Bunge la seneti nchini Italia limepitisha hoja ya kumtimua Waziri Mkuu mstaafu wa Italia Silvio Berlusconi katika bunge kutokana na kupatikana na hatia ya kukwepa kulipa kodi.
Kufuatia hatua hiyo sasa Berlusconi anaweza kushtakiwa kutokana na kukosa kinga ya bunge.
Kwa upande Berlusconi amewaambia wafuasi wake kuwa leo ni siku ya maombolezo katika demokrasia na kwamba kura hiyo ya bunge la seneti inaonyesha chuki binafsi ya wale wa upande wa kushoto.
Berlusconi alijiondoa siku ya jumanne katika chama cha Forza Italia ambacho kipo ndani ya serikali ya mseto inayotawala nchi hiyo, hata hivyo serikali iliepuka kura ya kutokuwa na imani na kufanikiwa kupitisha bajeti.
Mjadala katika bunge la seneti umekuwa mkali ambapo maseneta kutoka pande zinazopingana wamekuwa wakitupiana maneno makali.
Manuela Ripetti kutoka chama cha Berlusconi cha Forza Italia alisikika akipaza sauti "Tunajua nia yenu ni kumwondoa Silvio Berlusconi".
Awali Berlusconi ambaye ametawala katika siasa kwa miongo miwili nchini Italia amewaomba maseneta kusogeza mbele kura hiyo ya kumwondoa kwa madai kwamba anao ushahidi unaothibitisha kuwa hajafanya kosa la kukwepa kodi.
na BBCSwahili

Kategori

Kategori