Showing posts with label Israel kuishawishi Marekani. Show all posts
Showing posts with label Israel kuishawishi Marekani. Show all posts
 Mkutano wa mabadiliko ya hewa waanza hii leo Marekani

Mkutano wa mabadiliko ya hewa waanza hii leo Marekani

Mkutano mkubwa wa viongozi duniani kuhusu mabadiliko ya tabia nchi unafunguliwa leo katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa mjini New York Marekani, huku kukiwa na wito wa kupunguza hali ya joto duniani. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki Moon ndiye mwenyeji wa mkutano huo atakayewaongoza viongozi takriban 120, huu ukiwa mkutano wa kwanza wa ngazi ya juu tokea ule
Image result for hali ya hewa Pix
uliofanyika Copenhagen mwaka wa 2009 
 na kumalizika  bila ya mafikiano. Wanadiplomasia na wanaharakati wa mabadiliko ya tabia nchi wanauona mkutano huu kuwa  muhimu na kuelekea mkutano mwengine uliopangwa kufanyika mjini Paris mwishoni mwa mwaka wa 2015 ambao unatarajiwa kuweka mipango ya kupunguza utoaji wa gesi chafu inayoharibu mazingira,baada ya mwaka 2020.

HIVI NDIVYO WAZIRI WA ZAMANI WA ISRAEL "ARIEL SHARON" ALIVYOZIKWA LEO




Ibaada maalum ya aliyekuwa waziri mkuu nchini Israel Ariel Sharon imefanyika nje ya majengo ya bunge la Israel.
Bwana Sharon atakumbukwa kwa kuwa miongoni mwa waanzilishi wa taifa la Israel lakini pia alikuwa mwanajeshi na mwanasiasa jasiri aliyechukiwa na wapalestina wengi.








Waliohutubia umati,wamemtaja Sharon kama mtu aliyejitolea kuhakikisha kuna usalama kwa watu wake.
Waziri mkuu Benjamin Netanyahu alisema kuwa Sharon alikuwa mmoja wa makamanda wakuu wa wayahudi na ambaye atakumbukwa zaidi ya wote.
Licha ya sifa hizo Bwana Sharon anachukiwa sana na waarabu hasa wapalestina kwa dhuluma alizowatendea chini ya utawala wake.


Kiongozi huyo aliaga dunia siku ya Jumamaosi akiwa na umri wa miaka 85 baada ya kuwa hali mahututi kwa takriban miaka minane.
Atazikwa baadaye leo katika shamba la familia yake jangwani Negev.
Maelfu ya waombolezaji walitoa heshima zao za mwisho kwa Sharon siku ya Jumapili wakati ambapo mwili wake ulikuwa umelazwa nje ya majengo ya bunge mjini Jerusalem.
Na TheChoice

ISRAEL KUSHAWISHI BUNGE LA MAREKANI DHIDI YA MAKUBALIANO YA NUKLEA

Waziri wa Uchumi wa Israel Naftali Benett amesema leo hii nchi hiyo inapanga kulishawishi bunge la Marekani kuzuwiya kufikiwa makubaliano kuhusu mpango wa nuklea wa Iran.
Naftali Benett


Ameiambia radio ya jeshi kwamba kabla ya kuanza tena kwa mazungumzo hayo watawashawishi wabunge kadhaa wa Marekani ambao yeye mwenyewe binafsi atazungumza nao wakati wa ziara yake inayoanza Jumanne kwamba usalama wa Israel uko hatarini.

Benett alikuwa akizungumza baada ya Iran na mataifa yenye nguvu duniani kushindwa kufikia makubaliano kuhusu mpango wa nuklea wa Iran licha ya kuwa na mazungumzo ya siku tatu na kuvunja matumaini ya kufikiwa makubaliano yaliokuwa yakitafutwa kwa muda mrefu kuhusu mzozo huo wa muongo mzima.

Hata hivyo wanadiplomasia wanasema kwamba hatua kubwa za maendeleo zimefikiwa katika mazungumzo hayo na kwamba mazungumzo yataanza tena mjini Geneva tarehe 20 Novemba.

Kategori

Kategori