Showing posts with label Arusha. Show all posts
Showing posts with label Arusha. Show all posts

CHADEMA Jimbo la Moshi Mjini Yatangaza Wagombea.Wake.



Mkutano wa Hadhara wa Kampeni wa Utamburisho wa wagombea wa Udiwani katika jimbo la Moshi mjini.

Mgombea wa nafasi ya Udiwani kwa tiketi ya Chadema na UKAWA katika kata ya Korongoni ,manispaa ya Moshi,Ally Mwamba akiomba kura mbele ya wakazi wa mji wa Moshi wanaoishi Korongoni (hawapo pichani).

Mgombea wa nafasi ya Udiwani kwa tiketi ya Chadema na UKAWA katika kata ya Rau ,manispaa ya Moshi,Peter Kimaro akiomba kura mbele ya wakazi wa mji wa Moshi wanaoishi Rau (hawapo pichani)

Mgombea wa nafasi ya Udiwani kwa tiketi ya Chadema na UKAWA katika kata ya Ng'ambo ,manispaa ya Moshi,Genesis Kiwelu akiomba kura mbele ya wakazi wa mji wa Moshi wanaoishi Ng'ambo (hawapo pichani)

Mgombea wa nafasi ya Udiwani kwa tiketi ya Chadema na UKAWA katika kata ya Miembeni,manispaa ya Moshi,Mbonea Mshana akiomba kura mbele ya wakazi wa mji wa Moshi wanaoishi Miembeni (hawapo pichani)

Mgombea wa nafasi ya Udiwani kwa tiketi ya Chadema na UKAWA katika kata ya Msaranga ,manispaa ya Moshi,Anna Mushi akiomba kura mbele ya wakazi wa mji wa Moshi wanaoishi Msaranga.(hawapo pichani).

Mgombea wa nafasi ya Udiwani kwa tiketi ya Chadema na UKAWA katika kata ya Bomambuzi ,manispaa ya Moshi,Ludos Tarimo  akiomba kura mbele ya wakazi wa mji wa Moshi wanaoishi Bomambuzi(hawapo pichani)

Mgombea wa nafasi ya Udiwani kwa tiketi ya Chadema na UKAWA katika kata ya Majengo,manispaa ya Moshi,Peter Minja akiomba kura mbele ya wakazi wa mji wa Moshi wanaoishi Majengo (hawapo pichani)
Mgombea wa nafasi ya Udiwani kwa tiketi ya Chadema na UKAWA katika kata ya Kilimanjaro ,manispaa ya Moshi,Afrikan Mlay  akiomba kura mbele ya wakazi wa mji wa Moshi wanaoishi kata ya Kilimanjaro (hawapo pichani)

Mgombea wa nafasi ya Udiwani kwa tiketi ya Chadema na UKAWA katika kata ya Korongoni ,manispaa ya Moshi,Charles Mkome Mkalakala akiomba kura mbele ya wakazi wa mji wa Moshi wanaoishi Pasua (hawapo pichani)

Mgombea wa nafasi ya Udiwani kwa tiketi ya Chadema na UKAWA katika kata ya Kaloleni ,manispaa ya Moshi,Francis Shio akiomba kura mbele ya wakazi wa mji wa Moshi wanaoishi Kaloleni (hawapo pichani)

Mgombea wa nafasi ya Udiwani kwa tiketi ya Chadema na UKAWA katika kata ya Kiusa ,manispaa ya Moshi,Stephen Ngasa akiomba kura mbele ya wakazi wa mji wa Moshi wanaoishi Kiusa .
Mgombea wa nafasi ya Udiwani kwa tiketi ya Chadema na UKAWA katika kata ya Kaloleni ,Manispaa ya Moshi,Reward Shelukindo akiomba kura mbele ya wakazi wa mji wa Moshi wanaoishi Kaloleni  (hawapo pichani)

Mgombea wa nafasi ya Udiwani kwa tiketi ya Chadema na UKAWA katika kata ya Shirimatunda,manispaa ya Moshi,Makupa Jonathan akiomba kura mbele ya wakazi wa mji wa Moshi wanaoishi Shirimatunda. (hawapo pichani)

Mgombea wa nafasi ya Udiwani kwa tiketi ya Chadema na UKAWA katika kata ya Mawenzi ,manispaa ya Moshi,Hawa Mushi  akiomba kura mbele ya wakazi wa mji wa Moshi wanaoishi Mawenzi (hawapo pichani)

Mgombea wa nafasi ya Udiwani kwa tiketi ya Chadema na UKAWA katika kata ya Mji Mpya ,manispaa ya Moshi,Abuu Shayo akiomba kura mbele ya wakazi wa mji wa Moshi wanaoishi Mji Mpya .

Mgombea wa nafasi ya Udiwani kwa tiketi ya Chadema na UKAWA katika kata ya Nganga mfumuni ,manispaa ya Moshi,Anthony Lyimo  akiomba kura mbele ya wakazi wa mji wa Moshi wanaoishi Mfumuni(hawapo pichani

Mgombea wa nafasi ya Udiwani kwa tiketi ya Chadema na UKAWA katika kata ya Soweto ,manispaa ya Moshi,Collins Tamimu akiomba kura mbele ya wakazi wa mji wa Moshi wanaoishi Soweto.
Mgombea wa nafasi ya Udiwani kwa tiketi ya Chadema na UKAWA katika kata ya Njoro ,manispaa ya Moshi,Jomba Koi akiomba kura mbele ya wakazi wa mji wa Moshi wanaoishi Soweto.

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini.

Gola kuondoa watoto wa Mitaani Arusha


Afisa ustawi wa jamii na Maendeleo ya jamii jijini Arusha  Mwantumu Dossiakitembelea mradi wa shamba la mahindi unaoendeshwa na taasisi ya Gola
Foundation jana katika kituo cha Kufikia watoto wa mitaani,katikati ni
Mkurugenzi wa shirika hilo  Elisha Maghembe
Mkurugenzi wa shirika lisilokua la kiserikali la Gola Foundation ,Elisha Maghembe amesema kuwa wameanza zoezi la  kuwaondoa watoto wa mitaani walioko  jijini Arusha na kuwafikisha kwenye vituo maalumu vya malezi lengo ikiwa ni kuwarudisha makwao pamoja na kuwapatia fursa ya elimu waliyoikosa kwa muda mrefu.

Elisha alisema kuwa zoezi hilo limeanza mapema mwaka huu ambapo mpaka sasa wamewakusanya watoto 25 na kuwapeleka katika kituo chao cha malezi kilichopo wilaya ya Arumeru ambapo watoto watano walitambuliwa na kuchukuliwa na wazazi wao.

Amesema kuwa watoto wa mitaani wanapokaa mtaani kwa muda mrefu hujitumbukiza katika majanga ya matumizi ya madawa ya kulevya na kufanya vitendo visivyofaa hivyo ameitaka jamii ishirikiane kutatua tatizo hili ambalo ni janga kwa taifa.

“Tunapofika mtaani kuwaondoa watoto hawa wa mtaani tunakutana na changamoto nyingi ikiwemo kukosa ushirikiano na watoto wenyewe na pia wengine wanatumkishwa na ajira katika umri mdogo na baadhi ya watu hivyo kufanya zoezi hilo kuwa gumu” Alisha Elisha

Afisa ustawi wa jamii na Maendeleo ya jamii jijini Arusha,  Mwantumu Dossi alifika katika kituo cha kufikia cha malezi ya watoto wa mtaani kinachomilikiwa na Gola Foundation amesema kuwa Halmashauri ya jiji itaangalia namna ya kushirikiana kutatua changamoto za watoto wa mitaani.

“Tatizo la watoto wa mitaani ni tatizo sugu nimefika apa kujionea na kama Jiji kuna mkakati Mahususi wa kuwaondoa watoto wa mitaani utakaoanza 2015-2016” alisema Mwantumu 


Mwenyekiti wa Baraza la watoto wilaya ya Arusha Hassan Omari alisema kuwa juhudi za kuwaondoa watoto wa mitaani katika mazingira magumu na hatarishi zinapaswa kuungwa mkono na kila mtu pamoja na serikali kwani watoto ni taifa linalotegemewa kesho. 

WANAHABARI WAHIMIZWA KUWASILISHA MASUALA YAHUSUYO WATOTO YATIMA NA WAISHIO KATIKA MAZINGIRA MAGUMU


SAM_0796
Vyombo vya habari nchini vimehimizwa kuwasilisha masuala yanayowahusu watoto yatima na wale wanaoishi katika mazingira magumu. Akizungumza na wanahabari kutoka vyombo mbalimbali jijini Arusha katika warsha juu ya HAKI ZA WATOTO YATIMA NA WALE WANAOISHI KATIKA MAZINGIRA MAGUMU iliyoendeshwa na shirika liliso la kiserikali la The Foundation For Tomorrow (TFFT).
 
Mkurugenzi Mkuu wa Tanzania wa shirika hilo, Bwa. Kennedy Oulu alisema tatizo la watoto yatima na wale waishio katika mazingira magumu nchini Tanzania ni gumu, hivyo vyombo vya habari havina budi kuifahamisha jamii kuhusu hili suala na matatizo yanayowakabili watoto yatima na waishio katika mazingira magumu ili jamii na wadau mbalimbali waweze kushiriki vema katika kukabiliana na tatizo hili.
 
“Kwa sasa, inakadiriwa kuwa kuna watoto yatima na wale waishio katika mazingira magumu wapatao 1,800,000 hapa Tanzania pekee, huku 1,300,000 kati yao wakiwa wametokana na athari za ugonjwa wa UKIMWI. Mgawanyo wa kifamilia na muundo wa kimsaada kijamii ni moja ya vinavyochangia tatizo hili. 

Vinapoongezwa katika umaskini unaojidhihirisha katika: ukosefu wa upatikanaji wa huduma za elimu ikiwemo elimu ya awali, ukosefu wa upatikanaji wa huduma za afya na uzalishaji kama afya ya uzazi, ukosefu wa stadi za maisha zinazoakisiwa katika mitaala ya shule zenye uwezo unaotakiwa na ubunifu ili kujenga uwezo wa watoto, si kwa yatima na waishio katika magumu pekee”. Alisema Kennedy na kuongeza.
 
“Ni muhimu kutambua kuwa kumekuwa na hatua na mafanikio yaliyofikiwa na wadau mbalimbali ikiwemo serikali katika kuwezesha upatikanaji, kuzijengea uwezo familia za watoto hawa na kubadili mitazamo ya jamii dhidi ya watoto yatima na wale waishio katika mazingira magumu, hii inajenga msingi wa mwitikio endelevu.

WANAHABARI WAHIMIZWA KUWASILISHA MASUALA YAHUSUYO WATOTO YATIMA NA WAISHIO KATIKA MAZINGIRA MAGUMU


SAM_0796
Vyombo vya habari nchini vimehimizwa kuwasilisha masuala yanayowahusu watoto yatima na wale wanaoishi katika mazingira magumu. Akizungumza na wanahabari kutoka vyombo mbalimbali jijini Arusha katika warsha juu ya HAKI ZA WATOTO YATIMA NA WALE WANAOISHI KATIKA MAZINGIRA MAGUMU iliyoendeshwa na shirika liliso la kiserikali la The Foundation For Tomorrow (TFFT).
 
Mkurugenzi Mkuu wa Tanzania wa shirika hilo, Bwa. Kennedy Oulu alisema tatizo la watoto yatima na wale waishio katika mazingira magumu nchini Tanzania ni gumu, hivyo vyombo vya habari havina budi kuifahamisha jamii kuhusu hili suala na matatizo yanayowakabili watoto yatima na waishio katika mazingira magumu ili jamii na wadau mbalimbali waweze kushiriki vema katika kukabiliana na tatizo hili.
 
“Kwa sasa, inakadiriwa kuwa kuna watoto yatima na wale waishio katika mazingira magumu wapatao 1,800,000 hapa Tanzania pekee, huku 1,300,000 kati yao wakiwa wametokana na athari za ugonjwa wa UKIMWI. Mgawanyo wa kifamilia na muundo wa kimsaada kijamii ni moja ya vinavyochangia tatizo hili. 

Vinapoongezwa katika umaskini unaojidhihirisha katika: ukosefu wa upatikanaji wa huduma za elimu ikiwemo elimu ya awali, ukosefu wa upatikanaji wa huduma za afya na uzalishaji kama afya ya uzazi, ukosefu wa stadi za maisha zinazoakisiwa katika mitaala ya shule zenye uwezo unaotakiwa na ubunifu ili kujenga uwezo wa watoto, si kwa yatima na waishio katika magumu pekee”. Alisema Kennedy na kuongeza.
 
“Ni muhimu kutambua kuwa kumekuwa na hatua na mafanikio yaliyofikiwa na wadau mbalimbali ikiwemo serikali katika kuwezesha upatikanaji, kuzijengea uwezo familia za watoto hawa na kubadili mitazamo ya jamii dhidi ya watoto yatima na wale waishio katika mazingira magumu, hii inajenga msingi wa mwitikio endelevu.

VETA WATAKIWA KUSIKILIZA MAONI YA WADAU WAO ILI KUJUA MAHITAJI YAO SANJARI NA KUBADILISHA MITAALA YA ELIMU

 

 

Na Woinde Shizza, Arusha 
 Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (Veta)wametakiwa kuhakikisha wanasikiliza maoni ya wadau ili kujua mahitaji yao sambamba na kubadili mitaala ya elimu ya mafunzo yanayotolewa kwenye vyuo hivyo ili kuendana na soko la ajira lililopo hivi sasa. 
 Hayo yanesemwa leo jijini hapa na Waziri  wa Kazi na Ajira  Mhe Gaudensia Kabaka wakati alipokuwa akizindua kongamano lililoshirikisha wadau kutoka sekta mbalimbali kwaajili ya kujadili changamoto wanazozipata wadau hao na nini chakuongeza kwa vijana wanaopitia Veta na kupata ajira katika sekta mbalimbali sanjari na kuzindua kitabu kinachoanisha mahitaji ya soko la ajira kwa vijana 
 Mhe Kabaka aliwataka vijana kutumia fursa za kujiunga na Veta ili waweze kujiariri badala ya kufanya biashara za kuuza vitu mikononi bali watumie taaluma walizozipata kuzalisha vitu vyenye ubora. Alisema vijana wanaopitia vyuo vya mafunzo Veta si wengi sana huku wimbi la vijana likiwa bado mitaani na kuuza bidhaa zao mabarabarani hivyo ni vyema sasa vijana hao wakaondoka barabarani na kujiunga na vyuo vya ufundi ili waweze kupata mbinu za kutengeneza vitu sambamba na kupata masoko ya uhakika.
Alisema ni vyema sasa Vyuo vya Veta vikaweka mkazo katika sekta ya madini na gesi ili waweze kuangalia mahitaji ya wataalam ni yapi na kutoa elimu hiyo ambayo itawezesha vijana wengi kupata ajira na kukuza uchumi wananchi. 
"Mahitaji ya vijana ni mengi katika sekta rasmi na zisizo rasmi na kia sekta inamtegemea mtu fulani hivyo ni vyema Veta mkasikiliza mahitaji ya wadau sambamba na kutafuta mbinu za kufundisha zaidi ili kuendana na mahitaji ya soko na nyinyi vijana tokeni barabarani mkajiunge na vyuo vya ufundi ili kuweza kuuza biashara zenu kwa ubora badala ya kukimbilia kuuza barabarani ". Alisema Mhe Kabaka
Naye Mkurugenzi wa Veta, Mhandisi Zebadiah Moshi alisema kongamano hilo hufanyika kila mwaka na kushirikisha wadau katika sekta mbalimbali ili kujadili masuala mbalimbali na mahitaji ya wadau hao katika sekta ya ajira sambamba na kuboresha mitaala itakayokwenda na wakati na kuwezesha vijana wanaopitia Veta kuwa bora zaidi kipindi cha kumaliza chuo na kupata ajira. 
Alisema pia Veta inakabiliwa na uhaba wa rasilimali fedha kwenye ujenzi wa vyuo vipya kwenye Wilaya mpya ambazo ni Katavi, Geita, Njombe na Simiu lakini pia kuonaongezeko kubwa la vijana na watu mbalimbali ambao wanajiunga na vyuo hivyo nchini kwaajili ya kupata mafunzo mbalimbali yanayowawezesha kupata ajira. 
 Naye Mwenyekiti wa Bodi ya Veta, Profesa Idrissa Mshoro alisisitiza kuwa Veta inatambua na kuthamini maeneo mbalimbali yanayohitaji soko la ajira ndio maana vijana wanaopata ujuzi kupitia veta wanafanya kazi kwa makini na kujipatia vipato zaidi. 
 Aliongeza kuwa hivi sasa Veta inashirikiana na tasisi na mashirika mbalimbali hususan ya sekta ya madini na gesi na kutoa mafunzo kwaajili ya kuwasaidia vijana kukabiliana na soko la ajira .


WAZIRI wa Kazi na Ajira Mhe.  Gaudensia Kabaka  wakati alipokuwa akizindua kongamano lililoshirikisha wadau kutoka sekta mbalimbali kwa ajili ya kujadili changamoto wanazozipata wadau hao



Waziri wa ajira na kazi  Mhe. Gaudensia Kabaka akiwa katika picha ya pamoja wadau waliouthuria katika  konga mano hilo
Wa kwanza kushoto ni mwakilishi wa BG Tanzania Ms Kate Sullam anaemfatia ni Mr Jean Van Wetter ni mkurugenzi wa VSO Tanzania
Picha ya pamoja ya washiriki wa kongamono hilo wakiwa pamoja na Waziri wa ajira na kazi nje ya ukumbi wa hotel ya Naura Springs iliopo ndani ya jiji la Arusha
 Waziri  kabaka  wa kwanza kulia akifuatiwa na Mwenyekiti wa Bodi ya Veta, Profesa Idrissa Mshoro wakifuatilia kwa makini maelezo yaliyokuwa yanatolewa na Mkurugenzi wa Veta, Mhandisi Zebadiah Moshi (hayupo pichani)  kuhusiana na
Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (Veta)

 WAZIRI wa Kazi na Ajira  Mhe Gaudensia Kabaka  wakati alipokuwa akizindua kongamano
Baadhi ya waandishi  wakiendelea kufatilia kwa makini kongamano hilo
 Washiriki wakifuatilia

Kutoka  kulia ni mwenyekiti wa bodi ya veta Profesa Idrissa Mshoro wa pili kulia ni  Mkurugenzi wa Veta, Mhandisi Zebadiah Moshi wakiwa wanamsikiliza waziri 

washiriki wakiendelea kufuatilia kwa makini


 Mkurugenzi wa Veta, Mhandisi Zebadiah Moshi akiwa anaongea katika kongamano hilo
wadau kutoka sekta ya gesi na petrol wakiwa wanafatilia
Mada ikiwasilishwa

Wadau wakifuatilia mada 
waandishi  wa habari wa Mkoa wa Arusha wakimuoji mwenyekiti wa bodi

NAIBU WAZIRI WA FEDHA AFUNGUA MKUTANO WA WATAALAMU WA UGAVI JIJINI ARUSHA

 

Mwandishi wetu,Arusha

WIZARA ya Fedha, imeitaka Bodi ya Wataalam wa Ugavi na Manunuzi nchni  (PSPTB), kutafuta ufumbuzi wa tatizo la kufanya manunuzi bila kuzingatia thamani halisi ya fedha na kuwataka waajiri kuacha mara moja kuwaajiri watu wasio na sifa kufanya kazi hizo

Naibu Waziri wa Fedha,Adam Malima ametoa kauli hiyo leo wakati akifungua mkutano wa tano wa mwaka wa Siku mbili unaofanyika kwenye jengo la Mikutano la AICC jijini Arusha ambapo aliwataka Wataalamu hao kuzingatia maadili na miiko ya kazi yao.

Amesema katika bajeti ya mwaka 2014/15 serikali imetega bajeti ya Sh trilioni 20 kati ya hizo asilimia 65 hadi za 70 zinatumika kwenye manunuzi ya bidhaa na huduma mbalimbali,hivyo taaluma hiyo kuwa na umuhimu wa kipee katika kudhibiti mapato ya serikali yasitumike vibaya.

Awali Mwenyekiti wa Bodi hiyo, Sr. Dk. Hellen Bandiho, amesema kauli mbiu ya mkutano huo “Thamani halisi ya fedha za Manunuzi” ikilenga kuhakikisha serikali inapata huduma bora kulingana na fedha inazotumia ili kuinua uchumi wa nchi.

Amesema Bodi hiyo imezalisha wataalam zaidi ya 23,000 katika ngazi mbalimbali ambayo ni sawa na asilimia 47 pekee huku waajiri wengi wakiwa wamewajiri watumishi wasiosajiliwa na Bodi hiyo.
Naibu Waziri wa Fedha,Adam Malima akiongoza na maafisa wa Bodi ya Wataalamu wa Ununuzi na Ugavi(PSPTB) katika mkutano wa Siku mbili unaofanyika kwenye kituo cha mikutano cha AICC, jijini Arusha.
Naibu Waziri wa Fedha,Adam Malima akisoma hotuba yake kwenye mkutano wa Siku mbili wa Bodi ya Wataalamu wa Ununuzi na Ugavi(PSPTB)  unaofanyika kwenye kituo cha mikutano cha AICC jijini Arusha.
Baadhi ya Maafisa Ugavi na Ununuzi wakisoma nyaraka mbalimbali za mkutano huo leo jijini Arusha.
Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Wataalamu wa Ununuzi na Ugavi(PSPTB)Clemence Tesha(kulia)akimpongeza Naibu Waziri wa Fedha,Adam Malima kwa hotuba nzuri.
Wataalamu wa Ugavi na Ununuzi nchini wakiwa katika picha ya pamoja na Naibu Wazi wa Fedha (na michuzi na matukio)

Kategori

Kategori