Showing posts with label 2017 at 11:10AM. Show all posts
Showing posts with label 2017 at 11:10AM. Show all posts
Washauri wakuu wa waziri mkuu wa Uingereza wajiuzulu

Washauri wakuu wa waziri mkuu wa Uingereza wajiuzulu

Washauri wawili muhimu wa waziri mkuu wa Uingereza, Theresa May wamejiuzulu.
Pia kuna ripoti kwamba wanachama wakuu wa chama tawala cha Uingereza, cha Conservative, wametishia kuanza kutafuta kiongozi mpya, endapo washauri hao hawatotolewa kazini.
Mpambe wake, Nick Timothy, alisema anabeba dhamana kwa mchango wake katika kampeni ya chama, lakini alisema bado anaamini manifesto ilikuwa sawa, manifesto ambayo mwanachama mmoja maarufu alisema ni mbaya kabisa katika historia.
Msemaji wa chama amesema, mwenzake Bwana Timothy, Fiona Hill, piya amejiuzulu.
Bibi May anajaribu kuunda serikali ambayo haina wingi wa viti bungeni, kwa kutegemea chama kimoja cha Ireland Kaskazini.
ASANTE KWA KUTEMBELEA MTANDAO WETU!!

from Blogger http://ift.tt/2r6U9vm
via IFTTT


Wanahabari toka Ubelgiji wapo nchini kumfuatilia Samatta

Wanahabari toka Ubelgiji wapo nchini kumfuatilia Samatta

Waandishi wawili wa habari wamesafiri kutoka Ubelgiji kuja nchini kwa ajaili ya kumfuatilia mshambuliaji wa kimataifa Mbwana Samatta anaecheza kwenye klabu ya KRC Genk ya nchini Ubelgiji.
Gauyentie Bogouet pamoja na Marc Cornelissen ambao wanaandikia gazeti la Het Belang van Limburg na website ya http://www.HBVL.BE wana siku tatu tangu wafike Tanzania na leo watatembelea familia ya Mbwana Samatta.
Lengo kuu la safari yao ni kutaka kujua kwa undani alipotoka Samatta njia alizopita kabla ya kutua Genk maisha na tamaduni za taifa anakotokea.
“Tupo hapa kwa siku mbili sasa (jana) tumekuja kwa ajili ya kutaka kujua zaidi kuhusu Samatta alipotoka alikopita na namna alivyofanikiwa kufika Genk. Kesho (leo) tutatembelea nyumbani kwao kwa ajili ya kukutana na familia yake,” alisema Cornelissen mara baada ya kumalizika kwa mechi ya Tanzania vs Lesotho.
Waandishi hao walikuwepo kwenye mechi kati ya Stars dhidi ya Lesotho na walishuhudia Mbwana Samatta akifunga goli katika mchezo huo uliomalizika kwa sare ya kufungana bao 1-1.
Huenda ziara yao ikawa na faida kwa wachezaji wa Tanzania kwa sababu wamepata fursa ya kushuhudia mechi na kuwaona baadhi ya wachezaji wakiwa katika kiwango bora katika mchezo huo hivyo huenda katika ripoti yao wakashauri vilabu vya Ubelgiji kuja Tanzania kusaka vipaji.
ASANTE KWA KUTEMBELEA MTANDAO WETU!!

from Blogger http://ift.tt/2t8wivC
via IFTTT


Barnaba Asema Haya kwa Diamond Baada ya Kuanzisha Website ya Wasafi.com,Adai Amechoka na Kuibiwaโ€ฆ!!!

Barnaba Asema Haya kwa Diamond Baada ya Kuanzisha Website ya Wasafi.com,Adai Amechoka na Kuibiwa…!!!

Barnaba amedai kuwa ni bora fedha zao za muziki ziibiwe na Diamond kupitia tovuti yake ya kuuza muziki ya Wasafi.com kuliko watu wengine.
Muimbaji huyo ameiambia Dizzim Online, “Tumeibiwa sana wasanii, tumedhulumiwa sana. Mungu anisamehe kidogo, bora atuibie msanii mwenzetu, tunajua msanii mwenzetu anakula yupo kwenye soko letu kuliko atuibie mtu binafsi.”
“Na yeye akiwa kama CEO [Diamond] alichukua uamuzi wa busara kama heshima kutupigia simu wasanii wenzake mwenyewe kuliko kuwatuma menejimenti. Mimi naona jambo zuri la bahati alilolifanya na nilienda nikachukuwa contract yangu na kiukweli nimeusaini lakini bado kuurudisha,” ameongeza.
Katika hatua nyingine hitmaker huyo wa ‘Lover Boy’ amewataja wasanii ambao watasikika kwenye albamu yake mpya. Wasanii hao ni pamoja na Baraka The Prince, Linex, Dela, H_art The Band, Bahati wa Kenya, Vanessa Mdee kuna Jux, Maua Sama, G Nako na wengine.

from Blogger http://ift.tt/2myREik
via IFTTT


Kategori

Kategori