Showing posts with label 2017 at 10:45AM. Show all posts
Showing posts with label 2017 at 10:45AM. Show all posts
Thibaut Courtois akataa kusaini mkataba mpya,Madrid wachekelea.

Thibaut Courtois akataa kusaini mkataba mpya,Madrid wachekelea.

Mazungumzo ya mwanzo kati ya golikipa wa Chelsea Thibaut Courtois na klabu hiyo yamekwama. Taarifa zinasema klabu ya Chelsea ilikuwa na mazungumzo ya mwazo kuhusu mkataba wa golikipa huyo.
Hata hivyo pande zote mbili zinazozungumza zimeshindwa kufikia muafaka na suala kubwa likiwa ni nyongeza ya pesa katika mkataba huo, lakini wakala wa Courtois atakutana tena na Chelsea kufanya mazungumzo mengine ya pili.
Matajiri wa Real Madrid wanafuatilia kwa karibu suala la mkataba wa Courtois na Chelsea ambaye kwa muda sasa wamekuwa wakitaka kumsajili na kama mazungumzo kati ya Chelsea na Courtois yatashindikana baasi inaweza kuwa njema kwao.
Courtois amekataa mazungumzo ya awali kipindi ambacho golikipa wa Ac Millan Gianluigi Donnaruma amekataa kusaini mkataba mpya na anaweza kuchukua nafasi ya Courtois au anaweza kwenda Real Madrid kama Courtois akisaini mkataba mpya.
 ASANTE KWA KUTEMBELEA MTANDAO WETU!!

from Blogger http://ift.tt/2rCE4wJ
via IFTTT


Serikali Yaokoa Bilioni 53 Katika Rushwa…!!!!

Serikali Yaokoa Bilioni 53 Katika Rushwa…!!!!

WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema Serikali imefanikiwa kuokoa Sh bilioni 53.9 kutokana na uchunguzi na operesheni mbalimbali zilizofanywa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) katika mwaka 2016/2017.
Amesema kiasi hicho cha fedha ni kikubwa mno, ikilinganishwa ni Sh bilioni 7 tu zilizookolewa katika mwaka 2015/2016. Alisema hayo jana wakati akifungua semina ya Mtandao wa Wabunge wa Afrika walio katika Mapambano ya Rushwa (APNAC) Tawi la Tanzania kwenye ukumbi wa African Dream mjini Dodoma.
Akizungumzia hatua mbalimbali zinazochukuliwa na Serikali katika mapambano dhidi ya rushwa, alisema Serikali imeanza kupata mrejesho mzuri kwamba watumishi wa umma wanawajibika ipasavyo na vitendo vya rushwa vinaendelea kupungua.
“Baadhi ya hatua tulizochukua ni pamoja na kuimarisha taasisi yetu ya TAKUKURU; kuimarisha matumizi ya mashine za kielektroniki ili kupunguza mianya ya kupoteza mapato; kuanzisha mahakama ya mafisadi; kusimamia nidhamu katika utumishi wa umma na kuchukua hatua za haraka za kinidhamu na za kisheria dhidi ya watuhumiwa wote wa rushwa na ufisadi,” alisema.
Aliwaomba wabunge waendelee kuiunga mkono Serikali, kwani haina mzaha kwenye mapambano hayo. “Serikali haina mzaha kwenye mapambano dhidi ya rushwa na tutaendelea na mapambano hayo.
Hivyo, ninaomba waheshimiwa wabunge muendelee kutuunga mkono katika mapambano haya, twende kwa wananchi tukatoe wito kwao watuunge mkono kwenye vita hii,” alisisitiza.
“Tayari tumefanya tathmini na kubaini mianya ya rushwa katika sekta za ardhi, uchukuzi, biashara na maji na hivyo kuziba mianya hiyo. Tutaendelea kuiwezesha TAKUKURU ili iendelee na kazi nzuri waliyoianza ya kubaini mianya na kutoa ushauri wa kuziba mianya hiyo ya rushwa.
Lengo letu ni kuwekeza zaidi kwenye kuzuia, kwa kuwa kinga ni bora kuliko tiba”. Mapema, akizungumza katika semina hiyo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais anayeshughulikia Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Angellah Kairuki alisema Takukuru kwa kushirikiana na taasisi zilizo chini yake, wako njiani kuanzisha mtaala wa somo la rushwa ili ifundishwe tangu shuleni.
“Napenda kuwahakikishia waheshimiwa wabunge kwamba Serikali ya awamu ya tano haitakubali kuona rushwa ikiota mizizi. Tunaamini wanafunzi wakijengewa uwezo tangu utotoni, watachukia rushwa na hatimaye tutakuwa na Taifa lenye watu waadilifu,” amesema.
Alisema kutokana na kazi ya kupunguza watumishi hewa, hadi kufikia Aprili mwaka huu, Serikali imekwishapokea Sh bilioni 1.2 kwenye akaunti maalumu ya Takukuru iliyoko Hazina ambazo zinatokana na makusanyo kutoka kwa waliokuwa watumishi hewa.
Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkazi wa UNDP, Godfrey Mulisa alisema wataendelea kushirikiana na Bunge katika miradi mbalimbali ikiwemo shughuli zinazofanywa na APNAC.
Awali, Mwenyekti wa APNAC tawi la Tanzania, George Mkuchika alisema hadi sasa wabunge wapatao 148 wamekwishajiunga na mtandao huo. Kwamba anaamini hadi Bunge hili litakapomaliza muda wake, zaidi ya robo tatu ya wabunge watakuwa wamejiunga
ASANTE KWA KUTEMBELEA MTANDAO WETU!!

from Blogger http://ift.tt/2sdBUbA
via IFTTT


Tundu Lissu Aandika Historia TLS… Ashinda Urais kwa Asilimia 88…!!!

Wajumbe wa Chama cha Wanasheria wa Tanganyika (TLS), jana wamefanya uchaguzi wa kumchagua rais pamoja na wajumbe wa ngazi mbalimbali za uongozi wa chama chao.
Tundu Lissu inaelezwa kwamba ameshinda urais wa Chama cha Wanasheria (TLS) uliokuwa ukifanyika Arusha, jana kwa zaidi ya 88% ya kura zote.
Uchaguzi huo umefanyika mjini Arusha ambako wanachama wa TLS wamekutana kutekeleza ratiba hiyo pamoja na kupanga mipango mbalimbali ya utendaji kazi wa chama hicho.
Matokeo ni kama ifuatavyo:
Urais: Kura zilizopigwa 1682
Tundu Lissu 1411 sawa na asilimia 88
Francis Stolla 64
Victoria Mandari 176
Godwin Mwapongo 64
==>Kwa upande wa nafasi ya Makamu wa Rais (TLS) mshindi ni Godwin Ngwilimi aliyekuwa Mwanasheria wa Tanesco na kutimuliwa kwa kupinga Escrow.
Council Members
Jeremiah Motebesya
Gida Lambaji
Hussein Mtembwa
Aisha Sinda
Steven Axweso
David Shilatu
Daniel Bushele

from Blogger http://ift.tt/2mgyu5v
via IFTTT


Kategori

Kategori