Showing posts with label 2017 at 10:43AM. Show all posts
Showing posts with label 2017 at 10:43AM. Show all posts
KWA Anko Magu Hakuna Kuremba..Mawaziri Walishwa CHIPSI Mayai Ikulu…

KWA Anko Magu Hakuna Kuremba..Mawaziri Walishwa CHIPSI Mayai Ikulu…

Kwa maisha ya kawaida mtaani, chipsi mayai ni moja ya vyakula vinavyopendwa na watu wengi hasa kutokana na utamu wake lakini pia ni miongoni mwa vyakula vinavyopatikana kwa haraka zaidi.
Mtanzania wa kawaida hujua kuwa Ikulu yalipo makazi na ofisi ya Rais huwa wanakula vyakula vizuri sana, hivyo ukimwambia kuwa pia wanakula chipsi mayai tena siku za sikukuu, anaweza asiamini.
Suala la kubana matumizi kama ilivyo sera ya serikali ya awamu ya tano linafanyika si tu kwa kuzuia safari za nje au mikutano kutofanyikia katika hoteli za nyota tano, ni pamoja na aina ya chakula kinacholiwa n wageni Ikulu wakati wa vikao.
Mara kadhaa tumeona viongozi wa kitaifa wakipewa pipi na juisi au wakati mwingine wakipewa sambusa wanapokuwa wanakwenda kwenye vikao au mikutano, lakini hii ya jana huenda ikawa imetia fora zaidi.
Jana Rais Magufuli aliongoza kikao cha Baraza la Mawaziri Ikulu jijini Dar es Salaam ambapo, kwanza licha ya kuwa siku ya mapumziko, mawaziri hao walikuwa kazini na pili, licha ya kuwa siku kama ya jana watu hula vyakula mbalimbali kama pilau, mawaziri hao waliokuwa Ikulu walikula chipsi mayai.
Ndio, umesoma sawa sawa, chipsi mayai. Si kwamba chakula hiki hakifai kuliwa na viongozi hao, au ni vibaya wao kula, lakini kwa vile walikuwa Ikulu na ilikuwa sikukuu, ungetegemea kuona wamepewa vyakula vinavyoendana na sherehe hiyo. Na hii imewashangaza wengi kwenye mitandao ya kijamii kwani ni kwa mara ya kwanza kuona viongozi wakila chipsi Ikulu.
Kutokana na fedha kuwa ngumu mtaani, nadhani ni wakati muafaka sisi wananchi tuige mtindo huu wa kubana matumizi ili tuweze kuendana na serikali hii ya Magufuli.
ASANTE KWA KUTEMBELEA MTANDAO WETU!!

from Blogger http://ift.tt/2slfDUO
via IFTTT


Mwanafunzi Darasa 6 Abakwa Hadi Kufa,,,!!!

Mwanafunzi Darasa 6 Abakwa Hadi Kufa,,,!!!

MWANAFUNZI wa darasa la sita mwenye umri wa miaka 13 anayesoma Shule ya Msingi Kipanga wilayani Tanganyika mkoa wa Katavi, amebakwa hadi kufa na watu wasiojulikana, ambao waliutupa mwili wake korongoni.
Kaimu Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi, Benedict Mapujila alisema kitendo hicho cha kikatili ni cha juzi ya saa 11:30 kijijini humo juzi. Alisema siku ya tukio hilo, mwanafunzi huyo wa kike aliondoka nyumbani kwao kama kawaida yake kwenda shule.
Hata hivyo, hakurudi tena kwao na kusababisha wasiwasi mkubwa kwa wazazi wake, kwa kuwa hakuwa na tabia ya kuchelewa kurudi nyumbani. Wazazi wake walikuwa na wasiwasi mkubwa kwa binti yao kuchelewa kurudi nyumbani, hivyo waliamua kutoa taarifa kwa uongozi wa kijiji chao.
Viongozi hao wa kijiji na wananchi, walianza kumsaka binti huyo kwenye maeneo mbalimbali bila kukata tamaa. “Ilipofika saa kumi na moja na nusu ya jioni waliukuta mwili wa mwanafunzi huyo ukiwa umetupwa korongoni na kubaini kuwa alikuwa amebakwa huku sehemu zake za siri zikiwa zimeharibika vibaya,“ alisisitiza .
Alisema chanzo cha kifo cha mwanafunzi huyo wa kike, kilisababishwa na kuvuja kwa damu nyingi baada ya kufanyiwa ukatili huo na watu ambao hawajafahamika. Kamanda huyo alisema hakuna aliyekamatwa kuhusu tukio hilo na jeshi la polisi linaendelea kusaka wahalifu hao. Alisema baada ya kuufanyia uchunguzi wa kitabibu, mwili wa marehemu ulikabidhiwa kwa ndugu kwa ajili ya maandalizi ya maziko yake.
ASANTE KWA KUTEMBELEA MTANDAO WETU!!

from Blogger http://ift.tt/2rLrQ8f
via IFTTT


Mlango Wa Exit Umefunguka Kwa James Rodriguez.

Mlango Wa Exit Umefunguka Kwa James Rodriguez.

Inawezekana mchezaji James Rodriguez akawa ni dhahabu kwa vilabu vingine ambavyo bado vinampa nafasi na vinamhesabu kuwa mchezaji bora hasa kwa nafasi yake, lakini kwa Real Madrid anaonekana kuendelea kuwa mchezaji ambaye njia yake ya kutokea ipo wapi.
Baada ya uvumilivu wa muda mrefu hatimaye kiungo James Rodriguez wa Real Madrid ameanza kuonesha hisia zake za kutofurahia maisha katika timu hiyo baada ya kupiga ngumi benchi kufuatia kufanyiwa mabadiliko katika dakika ya 72 kwenye mchezo dhid ya Leganes.
Katika mchezo huo ambao Madrid walipata ushindi wa mabao 4 kwa 2 James alifunga bao moja na kutoa pasi maridhawa ya goli la nne lakini furaha ya nyota huyo iliisha baada ya kuona dalili za kufanyiwa mabadiliko.
Kocha Zinedine Zidane amesema ni kawaida kwa mchezaji kutofurahia kutoka kwani kila mchezaji hutamani kucheza dakika tisini. Tukio hilo limechochea kuongezeka kwa taarifa zinazomuhusisha mchezaji huyo raia wa Colombia huyo kuihama Real Madrid mwishoni mwa simu huu.
Vilabu vingi vimeendelea kuhusishwa na James Rodriguez huku vilabu vya ligi kuu ya Uingereza vikionekana kumtolea macho zaidi hsa Chelsea, Liverpool pamoja na Arsenal wakionekana kuwa mstari wa mbele huku Bayern Munich ikitajwa kuwa klabu inayomvutia zaidi.

from Blogger http://ift.tt/2nKnFUS
via IFTTT


Kategori

Kategori