Showing posts with label 2017 at 10:10AM. Show all posts
Showing posts with label 2017 at 10:10AM. Show all posts
RAIS MAGUFULI APIGA TOP UTOAJI WA URAIA KWA WAKIMBIZI WA BURUNDI

RAIS MAGUFULI APIGA TOP UTOAJI WA URAIA KWA WAKIMBIZI WA BURUNDI

Rais wa Jamhuri ya Burundi Mhe. Pierre Nkurunziza leo tarehe 20 Julai, 2017 amefanya ziara ya Rasmi ya Kiserikali ya siku moja hapa nchini kwa mwaliko wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli.
Ziara hiyo imefanyika katika Wilaya ya Ngara Mkoani Kagera ambapo Mhe. Rais Nkurunziza amepokelewa rasmi kwa kupigiwa mizinga 21 na kukagua gwaride rasmi lililoandaliwa na Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) kwa heshima yake katika eneo la Lemela na baadaye mazungumzo rasmi na dhifa ya kitaifa iliyofanyika Mjini Ngara.
Baadaye viongozi hao wamezungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika uwanja wa Posta ya zamani Mjini Ngara.
Akizungumza katika mkutano huo, Mhe. Rais Magufuli aliyeongozana na Mkewe Mama Janeth Magufuli amemshukuru Mhe. Rais Nkurunziza kwa kukubali mwaliko wake na amemhakikishia kuwa Serikali yake ya Awamu ya Tano itaendeleza na kuimarisha zaidi uhusiano na ushirikiano wa kihistoria na kidugu na nchi ya Burundi hususani katika kukuza biashara na uwekezaji.
“Tanzania ni ndugu zako na Watanzania ni ndugu wa watu wa Burundi, umekuja kwa mazungumzo ya kiuchumi, tumezungumza mambo mengi ya kuimarisha biashara kati Tanzania na Burundi, katika takwimu za mwaka 2016 biashara kati ya Tanzania na Burundi ilikuwa na thamani ya Shilingi Bilioni 116.5, kiwango hiki ni kidogo kwa nchi ya Burudni ambayo ina watu zaidi ya Milioni 10 na Tanzania ambayo ina watu zaidi ya Milioni 52” amesema Mhe. Rais Magufuli.
Halikadhalika Mhe. Rais Magufuli amesema Serikali ya Tanzania inaendelea na juhudi zake za kujenga reli ya kati kwa kiwango cha kisasa (Standard Gauge) ambayo itaunganisha bandari ya Dar es Salaam na nchi za Burundi na Rwanda na hivyo amemhakikishia Mhe. Rais Nkurunziza kuwa reli hiyo itakuwa kichocheo kikubwa cha uchumi wa Tanzania na nchi hizo.
Aidha, Mhe. Rais Magufuli amempongeza Mhe. Rais Nkurunziza kwa juhudi zake za kusimamia amani nchini mwake na ametoa wito kwa wakimbizi wa Burundi ambao bado wapo nchini Tanzania kuitikia wito wa Rais wao aliyewataka warudi nchini Burundi ili wakaendelee kujenga Taifa lao kwa kuwa hali ni shwari.
Pia Mhe. Rais Magufuli amemuagiza Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Mwigulu Lameck Nchemba kusitisha utoaji wa uraia kwa wakimbizi hao ili utaratibu huo usitumiwe kama kigezo cha watu kuzikimbia nchi zao.
Kwa upande wake Mhe. Rais Nkurunziza amemshukuru Mhe. Rais Magufuli kwa mwaliko wake na amesema Tanzania na Burundi ni ndugu na majirani ambao uhusiano na ushirikiano wake ulianza hata kabla ya uhuru.
Mhe. Rais Nkurunziza ametoa wito kwa wafanyabiashara wa Tanzania kwenda kufanya biashara Burundi na wafanyabisahara wa Burundi kuja Tanzania bila wasiwasi na amebainisha kuwa hali ya Burundi ni shwari kwani hata wakimbizi waliokimbilia Tanzania miaka miwili iliyopita wameanza kurejea nchini Burundi kwa hiari yao na wanaendelea na shughuli zao kama kawaida.
“Tunataka kuwajulisha wenzetu Watanzania na Warundi wenzetu ambao walikimbilia Tanzania, Burundi ya leo ni nchi yenye amani, tunawaalika Warundi wenzetu, kaka zetu na dada zetu ambao walikimbilia hapa Tanzania, warudi nchi kwao tujenge nchi yetu iwe na amani ya kudumu.
Tunapata faraja kwamba Warundi wenzetu ambao walikimbilia Tanzania miaka miwili iliyopita ambao wanafikia idadi ya 150,000 wameanza kurudi Burundi bila ya kupitia Shirika la Wakimbizi Duniani (UNHCR), kwa hiyo tunasema wote rudini nyumbani” amesema Mhe. Rais Nkurunziza.
Katika ziara hii Mhe. Rais Magufuli ameongozana na Mawaziri watano na Mhe. Rais Nkurunziza ameongozana na Mawaziri watano ambao pamoja na viongozi wengine wa taasisi na vyombo vya ulinzi na usalama wameshiriki mazungumzo rasmi.
Mhe. Rais Nkurunziza amemaliza ziara yake rasmi ya kiserikali ya siku moja hapa nchini na amerejea nchini Burundi.
Kesho tarehe 21 Julai, 2017 Mhe. Rais Magufuli ataendelea na ziara yake Mkoani Kigoma ambapo ataweka jiwe la msingi la ujenzi wa barabara ya Nyakanazi – Kibondo na barabara ya Kidahwe – Kasulu pamoja na kuzungumza na wananchi.
Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Ngara, Kagera
20 Julai, 2017

from Blogger http://ift.tt/2tlQF98
via IFTTT


Mbowe Naye Avunja Ukimya..Ampa Makavu Live Rais Magufuli ..Afunguka Jini Wapinzani Wanavyoteswa na Kunyanyaswa na Serikali..!!!!

Mbowe Naye Avunja Ukimya..Ampa Makavu Live Rais Magufuli ..Afunguka Jini Wapinzani Wanavyoteswa na Kunyanyaswa na Serikali..!!!!

KIONGOZI wa Kambi Rasmi ya Upinzani bungeni, Freeman Mbowe amesema mwaka mmoja na nusu wa utawala wa Serikali ya Awamu ya Tano umekuwa ni wa manyanyaso na uonevu kwa baadhi ya viongozi na watendaji wao kuuwawa au kupotea na Serikali ikiwa kimya.
Mbowe aliyasema hayo katika hotuba ya kambi hiyo bungeni kwa Ofisi ya Waziri Mkuu, mwishoni mwa wiki ambapo alitolea mfano mauaji na kesi zinazowakumba wapinzani kila kukicha.
Alisema katika kipindi hicho wameshuhudia mauji ya wanachama, kutekwa, kukamatwa kwa wabunge na wanachama na kesi mbalimbali ambazo hazina msingi zikiwa na lengo la kuwakatisha tamaa.
Alitolea mfano kifo cha aliyekuwa Mwenyekiti wa Chadema, Mkoa wa Geita Alphonce Mawazo na kusema aliuawa mchana kweupe, huku watu wakishuhudia na kwamba waliohusika wanajulikana, lakini hakuna hatua ambazo zilichukuliwa.
“Msaidizi wangu Ben Saanane alipotea baada ya kupokea vitisho kadhaa vyenye asili ya kisiasa na hadi sasa vyombo vya dola havijatoa maelezo ya kina ya Ben kapelekwa wapi,” alisema.
Mbowe alisema pamoja na changamoto hizo, Mwenyezi Mungu ameendelea kuwa upande wao na hila hizo za baadhi ya wenye mamlaka, hazijawaondoa kwenye lengo kubwa la kuwavusha wananchi wa Tanzania kuifikia ndoto zao.
Alisema wabunge wa upinzani hawajawa salama kwa kile alichodai kuwa kifungo cha Mbunge wa Kilombero Peter Lijualikali kilikuwa cha uonevu mkubwa na Mbunge wa Arusha Godbless Lema kunyimwa dhamana kwa zaidi ya miezi minne kwa shtaka lenye dhamana.
Mbowe ambaye pia ni Mbunge wa Hai alisema katika kipindi hicho pia wameshuhudia Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu akikamatwa mara kwa mara na vyombo vya dola na kufunguliwa mashtaka mbalimbali yasiyo na nia njema wala afya kwa ujenzi wa demokrasia katika nchi yetu.
“Tunaamini mapito haya mazito ya kisiasa katika nchi yetu yanalenga kujaribu kufifisha ndoto ya Taifa ndoto ya kuwa taifa huru linalosimamia misingi ya haki za binadamu, uhuru wa maoni ya kila raia, demokrasia ya kweli, kuwa taifa linaloheshimu Katiba ya Nchi na taifa lenye uchumi unaomnufaisha kila mwananchi,” alisema.
Mbowe alisema tangu Serikali ya Awamu ya Tano iingie madarakani, zimeonekana dalili za wazi za Serikali hiyo kuvunja Katiba ya Nchi kwa kutupilia mbali misingi ya utawala wa sheria, demokrasia na uhuru wa kupata habari jambo ambalo linaweza kuitumbukiza nchi yetu kwenye dola la ki- dikteta.
Alibainisha matukio mahsusi ya ukandamizaji wa haki na demokrasia yaliyofanywa na serikali kinyume cha Katiba na Sheria za nchi kuwa ni pamoja na kupiga marufuku mikutano ya vyama vya siasa.
Serikali kupitia Waziri Mkuu na Rais, ilitangaza kwamba ni marufuku kwa vyama vya siasa kufanya mikutano ya kisiasa mpaka mwaka 2020 ili kuipa Serikali nafasi ya kufanya kazi.
”Huu ni uvunjaji wa Ibara ya 20 (1) ya Katiba aidha, katazo la mikutano ya siasa linakiuka Sheria namba 5 ya Vyama vya Siasa ya 1992 ambayo imetoa haki kwa vyama vya siasa kufanya kazi ya siasa,” alisema.
Mwenyekiti huyo wa Chadema alisema kupiga marufuku urushwaji wa moja kwa moja wa Mijadala ya Bunge ni kinyume na Ibara ya 18 ya Katiba inayotoa uhuru wa maoni na uhuru wa kupata habari kwa kila mwananchi.
Alisema pia bungeni yamekuwapo matukio kadhaa yanayoashiria kutaka kuwadhibiti wabunge wa upinzani kwa lengo la kuwanyamazisha wasiikosoe Serikali.
Kiongozi huyo alisema jambo hilo limefanyika kwa namna mbalimbali, ikiwamo kuwazushia kesi wabunge wa upinzani na kuwapeleka kwenye Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge ambako hukumu ya kuwaadhibu inakuwa imeshaandaliwa.
Alibainisha kuwa changamoto nyingine ni Serikali kuingilia muhimili wa Mahakama, kupuuza utawala wa Sheria, uonevu aliodai kufanywa na vyombo vya Dola dhidi ya Wananchi wa Visiwa vya Unguja na Pemba.

from Blogger http://ift.tt/2nSQtL9
via IFTTT


Kategori

Kategori