Showing posts with label 2017 at 05:12PM. Show all posts
Showing posts with label 2017 at 05:12PM. Show all posts
‘Uthibiti wa uhalifu mitandaoni bado ni TATIZO’

‘Uthibiti wa uhalifu mitandaoni bado ni TATIZO’

Tanzania haina uwezo wa kudhibiti uhalifu wa kimtandao kutokana na mitandao inayotumika kumilikiwa na watu wa Magharibi.
Kauli hiyo imetolewa wiki hii katika mkutano uliowakutanisha viongozi wa Serikali kutoka Tanzania na China na wawakilishi wa vyombo vya habari jana.
Image result for mitandaoni
Mkutano huo ulikuwa ukidhibiti matumizi mabaya ya mtandao yanayoweza kuleta madhara katika vyombo vya habari.
Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Edwin Ngonyani amesema sheria ya udukuzi wa kimtandao inayotumika nchini haina uwezo wa kuwawajibisha watu wanaotumia vibaya mtandao kutokana na tofauti za tamaduni.
“Sasa tuna watu wanaodhibiti wahalifu wa kimtandao, lakini wanapata wakati mgumu kuthibitisha ushahidi kupitia mitandao ya kijamii kwa sababu mingi inatoka Marekani na kusimamiwa na sheria za nchi hiyo,” amesema Ngonyani.
Balozi wa China nchini, Lu Youqing amesema Tanzania ni moja kati ya nchi barani Afrika ambayo matumizi ya kimtandao yanakua kwa kasi, hivyo ni lazima kuwe na udhibiti wa watumiaji wabaya.
“Kupitia takwimu za TCRA (Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania) zinaonyesha kuna ongezeko la mara 13.7 kwa watumiaji wa simu ndani ya miaka 10 kutoka milioni 2.9 mwaka 2005 hadi kufikia watu milioni 39.8 mwaka 2015, huku watumiaji wa tovuti wakifikia milioni 17.26 mwaka 2015 kutoka milioni 1.01 mwaka 2005,” amesema Balozi Youqing.

from Blogger http://ift.tt/2uJ644O
via IFTTT


‘Dogo’ Harmorapa ampa makavu Diamond soma hapa !!

‘Dogo’ Harmorapa ampa makavu Diamond soma hapa !!

Harmorapa ni kama amemwaga petrol kwenye moto wa gesi. Rapper huyo aliyeteka vichwa vya habari kwa sasa nchini ameonekana kuanza kuununua ugomvi wa Diamond na Alikiba.
Harmo kupitia mtandao wa Instagram, amemtuhumu Diamond kuwa ndio aliyeanza kumchokoza Kiba hivyo anapaswa kumuomba msamaha kupitia vyombo vya habari. Kupitia mtandao huo hitmaker huyo wa Kiboko ya Mabishoo ameandika:


Mimi harmorapa mfalme wa bongoflaver and social network kwa sasa nasema kiukweli kutoka moyoni bwana mdogo #diamondplatnumz wewe ndo ulie anza kumrushia vijembe vya dharau Fundi #alikiba sasa usitafute suluhu kirahisi rahisi wewe platnumz nenda kwenye midia piga goti Muombe msamaa #alikiba kwani mkosefu ni wewe na sio #alikiba .
#now_naitwa_harmo_simba

Matokeo ya alichokiandika si mazuri. Hadi tunaenda mtamboni, bado anachezea mvua ya matusi kutoka kwa Team Diamond.

from Blogger http://ift.tt/2naayjT
via IFTTT


Kategori

Kategori