Tazama Diamond alivyo Copy Na Ku-Paste Video ya Jason Darulo

SOKO la nyimbo katika dunia ya sasa linakuzwa na video za muziki, ubora wa video umekuwa ukichangia kuufanya wimbo kuwa mkubwa hata kama ni wa kawaida.
Kuna vitu vingi vinavyochangia video kuwa bora, baadhi ni ubora wa picha, ubora wa mandhari na ubora wa ubunifu wa kile kinachoonekana katika video husika.
Msanii wa Tanzania, Diamond Platnumz anajulikana kwa kuwekeza nguvu kubwa kwenye kutengeneza video zenye kiwango cha juu, hilo halina ubishi.
Pamoja na sifa hizo, imekuwa ni kawaida kuona Diamond akiiga matukio kadhaa ya video za wasanii wa Marekani na kuziingiza kwenye video za nyimbo zake.
Mfanano wa video au jambo lolote ni kitu cha kawaida lakini kuna mazingira ambayo yanaweza kumfanya mpaka shabiki au mtazamaji wa video akaelewa kuwa hakuna mfanano wa bahati mbaya bali ni makusudi.
ASANTE KWA KUTEMBELEA MTANDAO WETU!!

from Blogger http://ift.tt/2tAxgFs
via IFTTT