MALINZI NA VIGOGO WENGINE WA TFF WAKWAMA TENA MAHAKAMANI

Kesi inayowakabili Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi na Katibu Mkuu wa shirikisho hilo Selestine Mwesigwa imeahirishwa hadi Julai 31 mwaka huu na watuhumiwa hao kurejeshwa rumande kwa kile mahakama ilichosema kuwa ni kutokamilika kwa upelelezi.
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam imetoa uamuzi huo leo asubuhi baada ya watuhumiwa hao wanaokabiliwa na jumla ya mashtaka 28 yakiwemo ya kughushi nyaraka, uhujumu uchumi na matumizi mabaya ya ofisi.
Malinzi na vigogo wengine wa TFF walikamatwa mwezi Juni na kupandishwa kizimbani kwa mara ya kwanza Juni 29 kujibu tuhuma hizo zinazowakabili.

from Blogger http://ift.tt/2uzR2kZ
via IFTTT