Baraka The Prince – Ben Pol Kaimba Upumbavu ..!!!

Baraka The Prince amemchana msanii mwenzake, Ben Pol kwa kumwambia hakuna chochote alichokifanya katika kazi yake mpya inayokwenda kwa jina la ‘Tatu’ licha ya kutengeneza kiki kubwa mitandaoni.
Baraka amesema hayo kupitia ukurasa wake wa kijamii Istagram huku akilalamika kwa kusema hakutegemea kuona kazi hiyo kwa jinsi alivyojitoa msanii huyo kwa kuweka picha zenye utata katika mitandao na kuwafanya watu kuwa na shauku kubwa kujua ni jambo lilipelekea vile.
“Nimekuwa ‘disappointed’ sana huu wimbo…Kwa jamaa alivyojitoa nilidhani ni kitu kikubwa kumbe upumbavu..’Save our music”.Ameandika Baraka

from Blogger http://ift.tt/2rD1PbY
via IFTTT