HUYU NDIYE RAIS WA KWANZA WA AFRIKA KUKUTANA NA RAIS DONALD TRUMP

Rais wa Misri, Abdel Fattah al-Sisi yupo, Washington, D.C nchini Marekani ambapo anatarajia kukutana na Rais wa Marekani, Donald Trump na kufanya naye mazungumzo.
Rais Abdel Fattah al-Sisi atakuwa kiongozi wa kwanza kutoka barani Afrika kukutana na Rais Trump. Lakini pia, alikuwa ndiye kiongozi wa kwanza wa Afrika kuzungumza na kumpongeza Trump baada ya kushinda katika uchaguzi mkuu wa Marekani uliofanyika Novemba 8, mwaka jana.
Masuala ya mgogoro kati ya Palestine na Israel yanatarajiwa kutawala sehemu kubwa ya mazungumzo yao, lakini pia masuala ya ugaidi duniani wakiegemea zaidi kupambana na kundi la kigaidi la Dola la Kiislamu (ISIS).
Viongozi hawa walikutana Septemba mwaka jana jijini New York wakati Rais Sisi alipokuwa nchini humo kuhudhuria Mkutano wa Umoja wa Mataifa (UN).

from Blogger http://ift.tt/2otjm54
via IFTTT

from WordPress http://ift.tt/2nAmhVD
via IFTTT

from Blogger http://ift.tt/2nArU6d
via IFTTT

from WordPress http://ift.tt/2nwjrAh
via IFTTT

from Blogger http://ift.tt/2nT6T9t
via IFTTT

from WordPress http://ift.tt/2nwwUrR
via IFTTT

from Blogger http://ift.tt/2nBDe1W
via IFTTT

from WordPress http://ift.tt/2oCqDfS
via IFTTT

from Blogger http://ift.tt/2nQ7Fmb
via IFTTT

from WordPress http://ift.tt/2nxtSUj
via IFTTT

from Blogger http://ift.tt/2ovv7rr
via IFTTT

from Blogger http://ift.tt/2ovsW7V
via IFTTT


Related Posts