HALMASHAURI ya mji Njombe imewaweka wadhabuni wawili katika
seka ya usafi ili kuhakikisha usafi unaimarika katika mji huo ambao kuwa sheria
ya utupaji taka imeanza kutekelezwa na faini kwa wanao tupa taka hovyo.
Akizungumza na Nipashe Mkoani Njombe afisa mazingira mji wa Njombe
Dolnald Mwalongo alitoa ufafanuzi huo baada ya wananchi wa mji huo kuibua
malalamiko ya kuchangishwa fedha na mdhabuni bila ya wao kujua na kuhofia
kutapeliwa.
Mwalongo alisema kuwa halmashauri hiyo imeanzakukusanya
fedha kuwa kutumia mdhabuni na kuzizoa taka hizo kwa kutumia mdhabuni wa
kampuni mbili tofauti.
Alisema kuwa kwa kawaida mwananchi au mdau wa uzalishaji wa
taka anatakiwa kuchangia kwa asilimia fulani ili kuzitoa kutoka vizimba vya
taka na kuzipeleka mbali na mji.
Alisema kuwa halmashauri pesa imeamua kuweka wadhabuni
wawili katika seka hiyo ya usafi wa mazingila ili kuboresha usafi wa mazingira.
Alisema kuwa imeweka wadhabuni wawili ili kutekeleza majukumu
ya usafi ya mazingira katika mji huo huku Akieleza kuwa mdhabuni wa kukusanya
pesa anapita kila sehemu anayo takiwa kupita na kukusanya pesa na mdhabuni wa
pili ni kutoa kata katika vizimba vya taka na kuzipeleka katika dampo kuu la
mji huo.
Aidha kwa upande wao wananchi walisema kuwa
hawajatambulishwa na Mkurugenzi kupitia watendaji wao wa mtaa juu ya mzabuni
anaye kusanya pesa.
Baadhi ya wananchi wamedai kuwa wanakwepa kulipa malipo ya
utoaji taka kutokana na mdhabuni hiyo kuto fahamika na kuhofia kutapeliwa.
Felix Mwabile ni mmoja wa wafanyabiuashara kwa ufahamu wake
anasema kuwa kazi ya kukurugenzi ni pamoja na kutoa taka katika vizimba na kuwa
kazi za wananchi ni kuzipeleka katika maeneo ya vizimba vya taka.
Hata hivyo licha ya wananchi kutokuwa na taarifa za mdhabuni
huyo mwenyekiti wa mtaa wa National Housing mjini Njombe Malaki Chaula alisema
kuwa ofisi yake imepokea barua ya uwepo wa mdhabuni atakaye kuwa anahusika na
ukusanyaji wa taka kutoka kwa Mkurugenzi.
