Msafara wa Mgombea Ubunge Jimbo La Chumbuni CCM

Msafara wa wapanda Pikipiki wakimsindikiza Mgombea Ubunge Jimbo la Chumbuni Zanzibar Ndg Ussi Salum Pondeza ukiondoka katika Tawi la CCM Muembemakumbi kuelekea Afisi za Tume ya Uchaguzi ya Taifa NEC katika majengo ya Skuli ya Rahaleo. 
Mgombea Ubunge kupitia Chama cha Mapinduzi CCM Ussi Salum Pondeza (HAMJAD) akiwapungia mikoni wananchi wakati akiupita katika mitaa ya barabara ya muembeladu kuelekea Afisi za Tume kuchukua Fomu ya kugombea Ubunge Jimbo la Chumbuni Zanzibar 
Msafara wa Mgombea Ubunge Jimbo la Chumbuni ukipita katika mitaa ya barabara ya beziredi kuelekea Afisi za Tume ya Uchaguzi ya Taifa (NEC) kumshindikiza Mgombea kuchukua Fomu ya Ubunge leo mchana.
Mgombea Ubunge wac Jimbo la Chumbuni Zanzibar Ndh Hamjad akisindikizwa na Familia yake akiwasili katika viwanja vya Afisi ya Tume ya Uchaguzi ya Taifa (NEC) katika majengo ya Skuli ya Rahaleo zilioko Afisi za Tume ya Uchaguzi ya Taifa Wilaya ya Mjini (NEC) kuchukua Fomu ya kugombea Ubunge wa Jimbo la Chumbuni Zanzibar kupitia Chama cha Mapinduzi.
Afisi wa Msimamizi Tume ya Uchaguzu ya Uchaguzi Wilaya ya Mjini (NEC) Ndg Seif Adam Muhuzi akitowa maelezo kwa Mgombea Ubunge wa Jimbo la Chumbuni kuhusiana na masharti ya Uchaguzi na jinsi ya kujaza famo hiyo wakati alipofika kuchukua Fomu ya kugombea Ubunge Jimbo la Chumbuni katika Afisi za Tume.  
 

Mgombea Ubunge Jimbo la Chumbuni Ndg Ussi Salum Pondeza akikabidhiwa Fomu ya Kugombea Ubunge Jimbo la Chumbuni na Afisi wa Tume ya Uchaguzi Wilaya ya Mjini Ndg Seif Adam Muhuzi   
Mgombea Ubunge Jimbo la Chumbuni Zanzibar Ussi Salum Pondeza HAMJAD akizungumza na waaandishi wa habari baada ya kuchukua Fomu ya kugombea Ubunge kupitia Chama cha Mapainduzi  katika Afisi za Tume zilioko Skuli ya Rahaleo, akitangaza sera zake  alizozipa kipaumbele katka Uongozi wake wa Ubunge katika Jimbo la Chumbuni