MECY: Waandishi muwe waangalifu

WAANDISHI  wa habari hapa nchini wametakiwa kuwa makiti katika kipindi hiki cha uchaguzi kwa kufanya kazi zao kwa taharadhari kwani wanakazi wakati wa uchaguzi na wataendelea kuwa na kazi baada wa uchaguzi.

Wito huo umetolewa na mwenyekiti wa chama cha waandishi wa habari Mkoani hapa, Njombe Press Club, Mecy Sekabogo, katika mkutamo mkuu wa waandishi wa habari Mkoani humo.
  
Alisema kuwa waandishi wa habari wamekuwa wakifanyakazi bira tahadhari na kupata na madhara ya majeraha, kuharibiwa vifaa vyao na wengine kuuwawa kusha vyombo vyao kuwakana.

Alisema kuwa waandishi katika kipindi hiki wanatakiwa wasijiweke katika siasa bali wafanye kazi za siasa kwa kuto pendelea upande wowote wala kuvaa nguo za baadhi ya vyama.

Alisema kuwa waandishi wapo kila siku lakini kipindi cha uchaguzi kina pita na kuwa waandishi wataendelea kufanya kazi hata baada ya uchaguzi kupita.
Sekabogo (Pichani Mwanamama) alisema kuwa uandishi wa mtu utaendelea hata baada ya uchaguzi kwani wanasiasa wamekuwa wakiwatumia watu kwa kujinufaisha wenyewe na baada ya kushindwa huwaacha waandishi na kuangalia mamboyao.

Alisema kuwa hatarajii kuona makaburi baada ya uchaguzi mkuu anatarajia kuendeleza kuona waandishi wapo na kuendeleza na kazi yao ya kuandika habari za kijamii.

“Katika kipindi hiki waandishi hamtakiwi kuwa upande wowote kwa kuwa utwtwkiwa kwenda kuandika habari za chama kingigine hauta andika vizuri kwa kuwa upo katika chama kingine,” alisema Sekabogo


Aidha kwa baadhi ya waandishi wamesema kuwa wamefurahia kukumbushwa juu ya tahadhari wanazo takiwa kuzichukua wakati wa kipindi hiki cha uchaguzi na kuwa watakuwa makini na kuto kuwa makaburi baada ya uchaguzi mkuu.