BABA mdogo wa marehemu
anayedaiwa kuuwawa kwa kupigwa na kuuwawa kwa risasi na askari Polisi amesema
chanzo cha kifo cha mwanae Basil Mwalongo ni kuwa alikuwa anamdai askari huyo na
kuitaka serikali ihakikishe inambana mtuhumiwa ili aeleze chanzo.
Alisema kuwa licha ya jeshi la Polisi
kumuweka mahabusu mshitakiwa ihakikishe inamuhoji na kuhakikisha haki za
marehemu zinapatikana.
Akizungumza na Elimtaa baada ya
mazishi ya mwanae ambayo yalitakiwa kufanyika Alhamisi ya wiki jana na
kushindwa kufanyika siku hiyo kutokana na kibali cha mazishi kuto kuwa na muhuri
na kuto eleza sababu ya kifo na kuzikwa Ijumaa.
Baba wa marehemu, Joseph
Mwalongo alisema kuwa chanzo cha kifo cha mwanae ambaye alikuwa ni fundi
kujenga inadaiwa kuwa alijenga nyumba ya askari anayedaiwa kufanya mauaji na
alikuwa anamdai pesa za ujenzi huo wa nyumba.
Alisema kuwa askari huyo alipopata
kazi ya kufanya doria usiku inadaiwa alimuona Basil mahari na kuanza
kumfuatilia na kisha kumpiga risasi na kusababisha kifo chake.
“Mwanangu hakuwa jambazi, hakuwa
mwizi alikuwa ni fundi kujenga alijenga nyumba ya askari huyo na alikuwa
anamdai pesa nyingi tu za ujenzi wa nyumba hiyo ambazo alikuwa hajalipwa wakati
wa ujenzi huo,” alisema Mwalongo.
Aliongeza kuwa mwanae aliyekuwa
fundi kujenga alikuwa ni tegemeo kwa mama yake mzazi ambaye ni mjane hiyo ameiomba
serikali kuhakikisha haki ya marehemu inapatikana na kuwa sheria ifuate mkondo
wake ili kitu kama hicho kisiweze kujitokeza tena.
Licha ya mwili wa marehemu
kuzikwa baada ya siku ya kuwaza kukataliwa kuzikwa bado ndugu za marehemu hawakulizika
na kibali kilichotolewa mara ya pili baada ya mara ya kwanza kutolewa bila
kuandikwa sababu ya kifo.
Walisema kuwa katika kibali cha
pili kilionyesha kuwa marehemu alikufa kwa kuvuja damu nyingi na kufa ambapo
kibali hicho kilikuwa kimetolewa na hospitali ya Kibena huku baada ya kuto
lizika walimfuata mkuu wa wilaya ya Njombe Sarah Dumba kutoa kibali hicho na
mazishi kufanyika.
Aidha inadaiwa kuwa mwili wa
marehemu ulipelekwa kijijini kwao ulipelekwa bila kuwapo kwa taarifa yoyote
kijijini pale na kuutua nyumbani na kuondoka.
Katika mazishi hayo upande wa
serikali kuliwakilisha na mshauri wa mgambo Reonald Mwajombe kwa niaba ya mkuu
wa wilaya ya Njombe alisema kuwa serikali imesikitishwa na msiba huo.
Alisema kuwa serikali itakuwa
bega kwa bega na upande wa marehemu na wakazi wa kijiji cha Lugenge na
kuhakikisha sheria fuata mkondo wake na haki kupatikana.
Kwa upande wa jeshi la mpaka
siku ya ijumaa hakukuwa na kauli yoyote huku kamana akisema kuwa anavikao na
siku ja Ijumaa Elimtaa ilipo fika katika ofisi za kamanda wa polisi alikuwa na
kikao na makamanda wa polisi wa wilaya na kuahidi kuzingumza mpaka jioni
hakukuwa na chochote alichiozongumza.
Marehemu Basil Mwalongo aliuwawa
siku ya Jumanne wiki iliyopita kwa kudaiwa kupigwa na risasi kichwani wiki
iliyopita na siku ya jumatano kusababisha maandamano ya wananchi kutoka katika
mtaa aliokuwa anaishi wa Nzengelentete ambao walitaka kutoa mwili wa marehemu
katika hospitali ya Kibena na kuupeleka katika kituo cha Polisi.
Marehemu alifia katika kilabu ya
pombe ya Nyondo katika mtaa wa Kambalage mjini Njombe ambapo siku hiyo Fred
Sanga alijeruhiwa ambapo askari hao walikuwa doria na kufanya vurugu kilabuni
hapo.
