WANAWAKE NJOMBE WATAKIWA KUWEKEZA KATIKA SHUGHULI ZA UFUGAJI






MKUU wa mkoa wa Njombe Dkt. Rehema Nchimbi wamewataka wadau wa ukuzaji na uendelezaji wa maziwa kuhakikisha wafugaji wa mkoa wa Njombe hasa wanawake wanakuwa wazalishaji wakubwa wa maziwa na kuhakikisha mkoa wa Njombe unakuwa kinala wa uzalishaji wa maziwa hapa nchini na maziowa ya Njombe kusambaa nchi nzima ifikapo mwisho wa mwaka huu.

Akizungumza katika maadhinisho ya siku Wanawake ambapo kwa mkoa wa Njombe zimefanyika katika kijiji cha Lole Kata ya Ikuna halmashauri ya Njombe na maandalizi yake kufanywa na wasimamizi wa mradi ukuzaji wa sekta ya Maziwa Afrika Mashariki (East Africa Dairy Development, EADD), aliwataka  kuhakikisha wanakuza wafugaji wa Ng’ombe wa maziwa na kuhakikisha maziwa ya Njombe ifikapo mwisho wa mwaka huu yanauza nchi nzima.

Nchimbi alisema kuwa katika ukuzaji wa wafugaji wahakikishe wanawake ndio wanakuwa vinala katika ukuzaji na uzalishaji wa maziwa na kwa kuwa
mkoa wa Njombe kunakuja uwekezaji mkubwa wa uchimbaji wa madini ya chuma na makaa yam awe wahakikishe wanawezesha mkoa wa Njombe kuwa ndio unalisha wawekezaji katika machimbo hayo.

“EADD nawataka mhakikishe katika uwekezaji mkubwa unao kuja hapa nchini na hasa kwa mkoa wa Njombe wawekezaji hawapati maziwa kutoka sehemu nyingine zaidi ya hapa Njombe na nakata mkoa huu kufunguliwa soko kubwa la kimataifa la maziwa na liwe ndio la kwanza,” alisema Nchimbi.

Alisema kuwa kufikia mwisho wa mwaka huu mradi huo uwe umeweza kukuza mwafugaji na maziwa ya kutoka mkoani hapa yanakuwa yamesambaa nchi nzima na kuwa siko kwamba maziwa kutoka sehemu nyingine yasimame bali maziwa ya mkoa wa Njombe kwa kuwa yanapenda hivto wahakijishe maziwa haya yanafika kila kona mikoa ya hapa nchini.

“Kufika mwisho wa mwaka huu nataka kuona kila kona ya nchi yanafika kwani mimi maziwa ya Njombe nimeanza kuyafahamu kabla sijafuika hapa Njombe na niliyapenda na maziwa haya yanapendwa na watanzania hivyo wekeni juhudi ili yafike katika kila kona,” aliongeza Nchimbi.

Naye mkurugenzi mkazi wa mradi EADD, Mack Txsaxo, alisema kuwa mradi huo unao lenga mikoa ya nyanda za juu kusini ya Mbeya, Iringa na Njombe kwa tanza nia ni mradia ambao pia upo katika nchi za Uganda, Kenya na Ruanda umelenga kuinua wafugaji kw akupata kipato kupitia maziwa na marisho.
Alisema kuwa wananchi wa mikoa wa nyanda za juu watapatiwa uwezeshwaji wa kuboreshewa afya za mifugo yao, kutafutiwa masoko ya uhakika na kuhakikisha mifigo yao inakuwa yenye manufaa kwao kwa kuboresha ,maisha kutokana na mazoa ya maziwa.

Aidha mradi huo unatarajia kuwasaidia wafugaji 35,000 hapa nchini na kufanya wafugaji kuw ana maisha endelevu katika ufugaji wa ngombe wa maziwa, na kunufaika kimaisha na katika siku ya wanawake mradi huo unatarajiwa kumsaidia mamamremavu wa macho kwa kumpatia kitu atakacho kiweza katika sekta ya maziwa.

“EADD itamsaidia mama Anna Ngimbhuchi atasaidia mradi wowote ambao atakuwa na uwezo nao katika sekta ya maziwa kwa kumpa mtaji wa thamani ya shiringi milioni moja baada ya wataalam wetu kufanyanae tathimini ya nini atakiweza kufanya,” alisema Txsoxo.

Aidha baadhi ya wafugaji walio nufakika na kupitia mradhi huo wameelezea hisia zao na kuwa wamefufaika kuzalisha maziwa mengi zaidi baada ya kuingia kwa mradi huo na sasa nameweza kuwa na kipato cha kutosha kutokana na maziwa na uzalishaji wa marisho.

Daina Mangula ni mmoja wa wakazi walio nufaika na mazao ya Ng’ombe kutokana na maziwa na kuzalisha marisho ambapo akitoa maelezo juu mbele ya mkuu wa mkoa juu ya faida za malisho alisema kuwa kutokana na mauzi ya mbegu za marisho bora ya nhombe amefanikiwa kupata kipato cha zaidi ya milioni moja na kuwa kupitia mauzo ya maziwa ameweza kusomesha watoto na kuwekeza katia miradi mingine mbalimbali.


Naye afisa mahusiano katika mradi huo Rachael Singo alisema kwa katika mradi huo wanategemea kuwawezesha zaidi wanawake kwa kuwa wanawake wakewezeshwa wanaweza kuiinua familia na kuwataka wanawake huhakikisha wanajiweka katika vikundi ili waweze kufikiwa na mradi huo.