Mweka hazina ajimegea posho Mwanza
Mweka Hazina wa Manispaa ya Ilemela jijini Mwanza anadaiwa kukiuka maadili ya uongozi na kujipatia masurufu na posho za kujikimu zaidi ya milioni nane kwa njia ya udanganyifu.
Habari kutoka ndani ya Manispaa hiyo zilizothibitishwa zinadai kuwa Lainie Kamendu alilipwa fedha hizo kwa awamu tano katika kipindi cha mwaka wa fedha 2013/14.
Alilipwa kwa ajili ya majukumu mbalimbali ikiwemo kwenda jjini Dar es salaam kufunga hesabu za Halmashauri yake kwa siku 50 ambalo aliliacha likiendelea na kurudi Mwanza kuchota fedha nyingine.
Kwamujibu wa chanzo cha habari inadaiwa kuwa mweka hazina huyo alipata milioni3.2 kati ya milioni19.2 zilizolipwa kutoka akaunti ya OC kama posho ya kujikimu kwa siku 40 ambapo kila siku alilipwa 80,000 kwa ajili ya kwenda kufunga hesabu.
By Mzalendo