Vijana someni katiba ili mfanye uchaguzi sahihi

  • Waaswa kuto ongozwa na wanasiasa


 VIJANA kote nchini wametakiwa kusoma kwa makini rasimu zote mbili za katiba ili kufanya uchaguzi sahihi wa ukifika wakati wa kuipigia kula katiba na kuacha kuongozwa na vyama vya vyama vya siasa.
 
Akizungunza na vijana katika siku ya Nyerere day mkoani hapa Mwenyekiti wa Jukwa la Vijanamkoa wa Njombe, Luka Mhaya, alisema kuwa vijana ili kuchagua rasimu au kuipinga rasimu iliyo pendekezwa ni vema wakapitia kwa makini kipengele hadi kipengele ili kuhakikisha vitu vyenye maslahi kwao kama vipo.

Alisema kuwa vijana wamekuwa wavivu wa kusoma na kupelewa kama bendela fuata upepo na taasisi mbalimbali vikiwemo vyama vya siasa.

“Vijana ili kuhakikisha mnaipitisha Katiba itakayo kuwa ni mstakabali wa maisha yetu ni vima tukaisoma rasimu hii ka kulinganisha na ile ya Tume ya mabadiliko yakatiba Chini ya Jaji Warioba ili kufanya uchaguzi sahihi na kuachana na kusikiliza kutoka vyama vys siasa,” alisema Mgaya.  

Alisema kuwa katika rasimu hiyo kama vijana wenyewe wakasoma na kuona inawafaa ni uamuzi wao au haifai ni uamuzi wako kuliko kama watabaki wakihangaika na kusikiliza wanasiasa wataweza kuchaguliwa kitu ambacho hakiwahusu.

“Vijana licha ya kusoma kwa makini Rasimu hizo mbili bali mjitokeze kujiandikisha katika daftali la kupigia kura ili kupata sifa ya kupiga kula katika rasimu hiyo,” aliongeza Mgaya

Alisema kuwa vijana hawapashwi kulaumu serikali kwa lolote linalo fanyika ni kutokana na serikali kukasimisha madaraka na madaraka kupewa serikali za mitaa na mambo yanayo fanyika ni kutokana na viongozi walio wachagua.


Alisema kuwa ni vema vijana kwa kipindi hiki uchaguzi wa serikali za mitaa wafanye uchaguzi sahihi katika serikali za mitaa na kujitokeza kuchukua nafasi za uongozi ili kufanya mabadiliko na kuondokana ulalamikaji kwa viongozi wasiofaa.

Related Posts