
Shirika
la afya duniani limesema kuwa zaidi ya watu elfu tatu sasa wamedaiwa
kufariki kutokana na kuzuka kwa ugonjwa wa Ebola katika eneo la
Afrika Magharibi kati ya visa elfu sita vya ugonjwa huo vilivyoripotiwa.
Liberia imeathiriwa vibaya na ugonjwa huo huku WHO ikisema kuwa kumekuwa na vifo 150 vilivyotokea katika kipindi cha siku mbili pekee.
Idadi hiyo inaweza kupuuzwa kwa kuwa watu wengi wanaogopa kwenda hospitalini.
Hazina
ya Fedha duniani IMF imeahidi dola millioni 130 kama msaada wa dharura kwa mataifa ya Liberia,Guinea na
Sierra Leone.