YANGA YA UTURUKI YAIBUKA NA USHINDI KIDUCHU DHIDI YA ASHANTI UNITED

Mshambuliaji wa Yanga, Didier Kavumbagu (kushoto) akiruka kuwania mpira na kipa wa Ashanti United, Daudi Mwasongwe, wakati wa mchezo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara uliomalizika hivi punde kwenye Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam. Katika mchezo huo Yanga imeibuka na ushindi wa mabao 2-1,yaliyofungwa na Didier Kavumbagu katika dakika ya 51 na la pili likifungwana David Luhende katika dakika ya 79. 
Bao la Ashanti lilifungwa na Bright Obina katika dakika ya 61. 
Katika michezo mingine, huko katika uwanja wa Chamazi Azam 1-Mtibwa Sugar 0, katika uwanja wa Mkwakwani Tanga Coastal Union 1- JKT Oljopro 1, Uwanja wa Kaitaba Kagera Sugar 0-Mbeya City 1 mpira bado unaendelea.
Mshambuliaji wa Yanga, Mrisho Ngassa (katikati) akijaribu kuwatoka mabeki wa Ashanti, Abuu Mtiro (kushoto) na Iddi Seleman (kulia). 
Wachezaji wa Yanga wakimpongeza mwenzao, David Luhende baada ya kufunga bao la pili.
Hussein Javu, akiruka kujaribu kumchambua kipa wa Ashanti.
Mohamed Fakhi na Hussein Javu, wakiwania mpira.
Kocha wa Yanga, Hans Van Der Pluijm, akitoa maelekezo kwa wachezaji wake.
Kocha akizungumza na wachezaji wake baada ya mchezo kumalizika. Simba watashuka dimbani katika uwanja wa Taifa kesho kukipiga na Rhyno.
Na Matukio na Vijana