Mjumbe maalumu wa Umoja wa Afrika amesema mbabe wa kivita kutoka
Uganda Joseph Kony huenda akawa mgonjwa sana na anatafuta hifadhi kwa
wapiganaji wake wa kundi la Lord’s Resistance Army.
Fransisco Madeira mjumbe maalum wa Umoja wa Afrika anayehusika na swala la kundi la waasi wa Uganda- LRA, alisema Jumatano kwamba kiongozi wa Jamhuri ya Afrika Kati amewasiliana na Kony na anajaribu kufanya mashauriano naye ili kujisalimisha kwake.
Lakini Madeira anasema inawezekana Kony anaidanganya serikali ya Jamhuri ya Afrika ya Kati ili inapofanya majadiliano, apate muda wa kufanya mkakati wa kuhamisha wapiganaji wake.
Mjumbe huyo hakutoa maelezo zaidi kuhusu kuugua kwa Kony.
Fransisco Madeira mjumbe maalum wa Umoja wa Afrika anayehusika na swala la kundi la waasi wa Uganda- LRA, alisema Jumatano kwamba kiongozi wa Jamhuri ya Afrika Kati amewasiliana na Kony na anajaribu kufanya mashauriano naye ili kujisalimisha kwake.
Lakini Madeira anasema inawezekana Kony anaidanganya serikali ya Jamhuri ya Afrika ya Kati ili inapofanya majadiliano, apate muda wa kufanya mkakati wa kuhamisha wapiganaji wake.
Mjumbe huyo hakutoa maelezo zaidi kuhusu kuugua kwa Kony.