Showing posts with label Tanzania kimataifa mawasiliano. Show all posts
Showing posts with label Tanzania kimataifa mawasiliano. Show all posts

Tanzania yaendelea kunufaika na uhusiano mwema ulipo baina yake na Taifa la China.

 Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu – Uwekezaji na Uwezeshaji Dkk. Mary Nagu akizungumza na waandishi wa Habari wakati wa hafla ya kuadhimisha miaka 65 tangu kuanzishwa Jamhuri ya Watu wa China jana jijini Dar es Salaam.
 : Balozi wa China nchini Tanzania Balozi Lui Youqing akigonga glasi ya mvinyo wakati wa hafla ya kuadhimisha miaka 65 tangu kuanzishwa Jamhuri ya Watu wa China jana jijini Dar es Salaam.
 Picha ya Keki kwa ajili ya hafla ya maadhimisho ya miaka 65 tokea kuanzishwa kwa Jamhuri ya Watu wa China hafla hiyo imefanyika jana jijini Dar es Salaam.
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu(Uwekezaji na Uwezeshaji) Dkt. Mary Nagu  na Balozi wa China nchini Tanzania Balozi Lui Youqing wakikata Keki  wakati wa hafla ya kuadhimisha miaka 65 tangu kuanzishwa kwa Jamhuri ya Watu wa China jana jijini Dar es Salaam.
 Balozi wa China nchini Tanzania Balozi Lui Youqing (katikati) akiteta jambo na baadhi ya wageni waalikwa katika hafla ya kuadhimisha miaka 65 tokea kuanzishwa kwa Jamhuri ya Watu wa China jana jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Jordan Rugimbana na Afisa anayeshughulikia masuala ya Menejimenti na Programu wa Aga Khana Development Network Bw. Navroz Lakhani
 Msanii wa Jamhuri ya Watu wa China akicheza mchezo wa Wushu wakati wa hafla ya kuadhimisha miaka 65 tangu kuanzishwa kwa Jamhuri ya Watu wa China jana jijini Dar es Salaam.
 Baadhi ya wageni wakisoma vitabu wakati wa hafla ya kuadhimisha miaka 65 tangu kuanzishwa kwa Jamhuri ya Watu wa China jana jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya wageni wakifuatilia michezo mbalimbali kutoka kwa wasanii wakati wa hafla ya kuadhimisha miaka 65 tangu kuanzishwa kwa Jamhuri ya Watu wa China jana jijini Dar es Salaam. Picha na Frank Shija, WHVUM.
========  ========  =======
Tanzania yaendelea kunufaika na uhusiano mwema ulipo baina yake na Taifa la China.

Na; Daud Manongi,    WHVUM.

Hadi kufikia mwishoni mwa mwaka 2013 China imetoa msaada wa zaidi ya dola za Kimarekani bilioni 1.943 kwa ajili ya kusaidia miradi mbalimbali ya maendeleo nchini Tanzania, ushirikiano wa kibiashara  dola bilioni 3.7 na uwekezaji dola bilioni 2.5 na jumla ya makampuni 500 yamewekeza nchini Tanzania.

Haya yamebainishwa na Waziri wa Nci ofisi ya Waziri Mkuu – Uwekezaji na Uwezeshaji Dkt. Mary Nagu aliyekuwa mgeni rasmi katika hafla ya miaka 65 ya toka kuanzishwa kwa Jamhuri ya Watu wa China jana jijini Dar es Salaam.

Dkt Nagu amesema kuwa msaada huo utasaidia katika kutekeleza miradi ya maendeleo ikiwema Bandari ya Bagamoyo, mradi wa EPZ, usambazaji wa umeme ukanda wa Kaskazini – Mashariki, Elimu kwa njia ya mtandao,Serikali Mtandao kwa ajili ya Zanzibar na Umeme wa upepo katika mkoa wa Singida. Aliongeza kuwa kukamilika kwa miradi hiyo kutafungua njia za uchumi na kusababisha Tanzania kuwa na uchumi imara na endelevu.

“Najisikia faraja kusema kuwama pamoja na mafanikia chanya tunayopata Tanzania bado ina miradi mingi ambayo inahitaji msaada wa kifedha na kitaalam kutoka kwa Jamhuri ya Watu wa China na ni imani kuwa wataendelea kutoa ushirikiano katika kufanikisha miradi hiyo” Alisema Dkt. Nagu.

Kwa upande wake Balozi wa China hapa nchini Balozi Lui Youqing amesema kuwa nchi yake itaendelea kuisaidi Tanzania kwa kuwa kumekuwa na mahusiano mazuri nay a muda mrefu baina ya nchi hizi mbili.

Balozi Youqing ameongeza kuwa Tanzania inavutia wakezaji kwa kuwa na mazingira salama ya kisiasa na kijamii ambapo anashawishika kuunganisha wawekezaji wa China kushirikiana na wawekezaji wengine katika kupunguza umasikini na kuleta maendeleo akitolea mfano ushirikiano katika sekta ya majengo.

“Tanzania ni nchi kubwa yenye maono na inayovutia zaidi kimataifa kutokana na uimara wake katika Nyanja za siasa na uchumi jamii, imekuwa na ushawishi wa hali ya juu katika anga za kikanda na kimataifa, hali inafanya wawekezaji kutoka sehemu kama EU, US, Japana na kwingineko waongeze uwekezaji, ata mimi binafsi nashawishika kuwashawishi wawekezaji wa China kuwekeza zaidi katika nchi hii” Alisema Balozi Youqing.

China inasherehekea miaka 65 toke kuanzishwa kwake mnamo mwaka 1949, wkati huo huo ni miaka 50 sasa tokea Taifa kuanzisha mahusiano ya kidiplomasia kati yake na Tanzania uhusiano ambao umeasisiwa na Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na Hayati Mao Zedong

Ushiriki wa Tanzania Kwenye Kongano la TEHAMA la Dunia La Shirika la Usimamizi wa Mawasiliano Duniani ITU‏


 Katibu Mkuu wa ITU ambalo ni Shirika la Umoja wa Mataifa linalosimamia Mawasiliano Duniani Dr. Hamadoun Toure akisikiliza Maelezo kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu wa TCRA Prof. John Nkoma. Kulia ni Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia Mh. Prof. Makame Mbarawa. Katikati ni Waziri wa ICT wa Thailand.
 Timu ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania katika Maonesho ya ITU Telecom World
 Timu Tanzania I kuifanya mikakati ya kushiriki kikamilifu katika siku mbili zilizobaki. Hapa wakipeana taarifa ya Matukio ya siku ya pili.
 Kauli Mbiu ya Tanzania katika Kongano la ITU Telecom
*******

Tanzania inashiriki katika Kongano la TEHAMA la Dunia linaloandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa linalosimamia Mawasiliano Duniani (ITU-International Telecommunications Union) linalofanyika katika jiji la Bangkok nchini Thailand.

Kongano hilo lenye Kauli Mbiu ya Kuchochea Mabadiliko Katika Ulimwengu wa TEHAMA, unashirikisha nchi wananchama wa ITU na wasio wanachama, Makampuni ya Mawasiliano Duniani, Taasisi na wasimamizi wa sekta ya Mawasiliano Pamoja na Serekali, wanashiriki Kongano hili katika kipindi ambacho mabadiliko makubwa katika Sekta ya Mawasiliano.

Mabadiliko haya yanapelekea dunia kuwa na Changamoto ya Kuyakubali Mabadiliko hayo na kukabiliana na Changamoto zake kwani faida za mabadiliko ni kubwa kwa Jamii Habari duniani. Akizungumza jijini Bangkok, Waziri wa Mawasiliano Sayansi na Teknolojia Prof. Makame Mbarawa amesema Tanzania iko tayari kwa na imeshapokea mabadiliko na imetekeleza mikakati ya kuhakikisha Tanzania inapokuwa mabadiliko bila tatizo.

Aidha Mheshimiwa Mbarawa amesema Tanzania inatambua umuhimu wa mabadiliko katika TEHAMA hususan kipindi hiki cha dijitali kwani ndio njia pekee ya kuharakisha maendeleo ya watanzania kwa ufanisi.

Nae Mkurugenzi Mkuu wa  Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania Prof. John Nkoma amesema Tanzania tayari  mstari wa mbele kuhakikisha inachochea mabadiliko ya teknolojia ya habari na mawasiliano ili wananchi wafaidike na huduma za Mawasiliano. "Tuna mfumo mzuri wa usimamizi wa leseni za muingiliano wa teknolojia, sheria na kanuni nzuri ambazo zinawezesha mabadiliko katika TEHAMA kunufaisha watanzania. Tayari Tanzania imeingia katika mfumo wa Utangazaji wa digitali na tunaendelea kuweka mazingira mazuri ya kuwepo kwa huduma nyingi zaidi kurahisisha maisha ya watanzania". Amesema Profesa Nkoma.

Taasisi kadhaa toka Tanzania zinashiriki Kongano hili kutoka Tanzania ikiwa ni pamoja na W ziara ya Afya, Kamisheni ya Sayansi na  Teknolojia,  DTBi ya wavumbuzi na wagunduzi, NICTBB inayosimamia mkongo wa Taifa, MaxCom.

Kongano hili linafanyika kwa siku nne kuanzia tarehe 19 - 22 Novemba 2013. Tanzania inashiriki na kauli Mbiu ya nchi "Tanzania: Africa Strategic ICT Hub". Pamoja an Kongano pia yako Maonesho ya ICT yenye nia ya kuonesha jinsi nchi zinavyochochea maendeleo kwa raia wake kupitia TEHAMA. Banda la Maonesho la Tanzania limevutia watu wengi wanafikia kujifunza jinsi Tanzania imeweza kuchochea mabadiliko katika TEHAMA na jinsi wananchi wanafaidika na huduma mbalimbali zinazotolewa nchini.

Aidha Baadhi ya Taasisi zinazoshiriki zinaangalia uwezekano wa kuchochea zaidi upatikanaji wa huduma zao kwa kuwa na washirika katika shughuli zao. Leo asubuhi Ujumbe wa Tanzania ulishiriki katika Mkutano Maalum wa Wawekezaji Katika Sekta ya Mawasiliano ulioendeshwa na Naibu Katibu Mkuu wa ITU Bwana Houlin Zhao.

NA Mbeyayetu

Kategori

Kategori