Showing posts with label Kitaifa. Show all posts
Showing posts with label Kitaifa. Show all posts

Waziri Mkuu aendelea na ziara yake mkoani njombe hii ni taarifa siku yake ya tano ona video

 Waziri mkuu wa tanzania Mhe. Kassm Majaliwa (Katikati) akizungumza na baadhi ya viongozi mkoani Njombe katika eneo la Liganga nyuma yake ni Mawe yanayo daiwa kuwa na Chuma Cha liganga
 Waziri Mkuu Wa Tanzania Kassm Majaliwa Akizungumza na wakazi wa Ludewa Mkoani Njombe ambako anatoa onyo wa wanao jifanya wananchi na kuvamia migodi la Liganga
 Ngomba ya Kinyakyusa ikimpokea waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa katika viwanya vya shule ya mpira Ludewa Mjini ambako amezingunza na wananchi
SERIKALI imesema kuwa itahakikisha kuwa wananchi wanao zunguka mradi wa Machimbo ya Liganga machimbo ya chuma ambao unatarajia kuanza hivi karibuni ambapo kunatarajiwa wananchi hao kulipwa na kuanza Machimbo katika eneo hilo ambapo onyo kwa wale ambao wameanza kuanza kujichomeka na kupata fidia.

Waziri Mkuu ametembelea eneo la machimbo ya Liganga wilayani Ludewa ambapo mbunge wa jimbo la Ludewa anaomba kwa waziri wananchi wake kulipwa fidia na kuwekwa kwa lami barabara ya kutoka Mkiu kuingia mpaka katika mladi wa Liganga.

Waziri akielekea wilayani ludewa anakutana na wananchi wanao msimamisha katika kijiji cha Lusitu ambapo wananchi wanamfikishia kilio chao kwa kutumia nyimbo.

Kabla ya kuingia ludewa mjini waziri anaingia Liganga ambako chuma litachimbwa kwenye mlima wa mawe ya chuma lenye ukubwa wa kilomita kumi ambapo akiwa hapa anazungumza na viongozi wa mkoa wa Njombe.

Baada ya kumaliza kutembelea mradi huu waziri mkuu anakutanan ana wananchi ambapo suala ya fidia mbunge analisema mele ya mkutano wa hadhana huku barabara nayo ikiombwa kuwa ya lami kutoka Mkiu hadi Liganga.

Na haya ndio majibu ya waziri mkuu huhusu umeme, fidia na huduma zinginde za za kijamii.
Kuhusu kukamilika  kwa kulipa fidia na kuanza kwa mradio huo waziri anaongeza.

Baada ya kutoka eneo la mgodiwaziri mkuu anaelekea mjini  Ludewa kwaajili ya Mkutano wa Hadhara   na kuzungumza na wakazi wa  mjini Ludewa ambapo suala la maji na barabara linaibuka tena.


TAZAMA VIDEO HAPO CHINI ALICHO KISEWA WAZIRI MKUU KUZITO KUHUSU LIGANGA

Ziara ya waziri mkuu Njombe Yaahirishwa kuendelea Jumatano wiki hii

 Baadhi ya wakazi wa Njombe Mjini wamiwa wanamsikiliza waziri Mkuu Kassm Majaliwa katika maeneo ya Wikichi Mjini Njombe
 Waziri mkuu Majaliwa akizungumza na wakazi wa njombe Maeneo ya Hospitali ya Mkoa wa njombe Mtaa wa Wikichi Njombe Mjini.
Wziriri Mkuu Mh. Kassim Majaliwa wakitembelea maeneo mbalimbali ya kiwanda cha chai cha Kibena 
WAZIRI  Mkuu wa Tanzania, Mhe Kassim Majaliwa ameahirisha ziara yake mkoani Njombe ambapo ameelekea jijini Dar es salaam ambako anatarajia kumpokea Rais wa Uturuki ambaye anakuja hapa nchini kwa ziara ya kikazi Ziara yake inatarajiwa kuendelea januari 25 kwa siku tatu.
Waziri mkuu amekuwa mkoani Njombe kwa siku tatu ambapo amepita katika halmashauri tatu za mkoa huo kabla ya kuahirisha ziara hiyo na kurejea jijini Dar es Salaam kwa majukumu mengine ya kiutendaji ziara yake mkoani Njombe ilikuwa ya siku sita na kuzitembelea halmashauri zote za mkoa huo.
Waziri mkuu Juzi aliwaaga viongozi wa mkoa wa Njombe na kuelekea jijini Dar Es Salaam katika viwanja vya ndege mkoani Iringa huku akitarajia kulejea tena mkoani humo Januari 25 na kumaliza ziara yake baada ya siku tatu.

Akirejea Njombe atatembelea halmashauri ya wilaya ya Njombe na kutembelea kiwanda cha chai na kuzungumza na wakulimqa wa zao hilo, kasha kuzungumza na wakazi wa Mji wa Njombe baadaye kwenda wilayani Ludewa ambako pia atakutaa na wakazi wa Mundini na Liganga kutako tarajiwa kuwa na migodo ya makaa yam awe na Chuma.
Mkuu wa mkoa wa Njombe Christopher Olesendeka akizungumza na Nipashe kuhusiana na kuahirishwa kwa ziara hiyo alisema kuwa waziri mkuu alikuwa mkoani humo kwa siku tatu ambapo ameahilisha kuendelea na ziara na kasha kulejea tena Januari 25.

Alisema kuwa waziri mkuu anaelekea jijini Dar es Salaam kwa kuwa nchi itakuwa ikipokea ugeni wa Rais wa Uturuki ambaye anafanya ziara yake hapa nchini ambapo baada ya ziara ya Rais Huyo Waziri mkuu watalejea Mkoani Njombe.
 
Mwishoni mwa wiki jana Waziri mkuu alikuwa mkoani Njombe na kuzungumza na wakazi wa maeneo mbalimbali ya halmashauri za wilaya Makete, Wangingombe, na mji wa Makambako ambako ndio alianzia ziara yake.

Akiwa Wangingombe alifungua jingo la Halimashauri ya Wangingombe na kuzungumza na wananchi wa Mjia huo kasha kuwataka watumishi wa halmashauri na wilaya kuhamia halmashauri hiyo ifikapo mwezi februari.

Waziri hakusika kuwaeleza wananchi adhima ya serikali kuwaletea maendeleo ikiwa ni pamoja na kumaliza matatizo ya maji na kufanya wafanye shughuli za kimaendeleo bila Bughuza.

ZANZIBAR INAZIDI KUKUA KWA KASI YA KIMAENDELEO



Balozi wa Korea Kusini Nchini Tanzania Bwana Song Geum Yong amesema Zanzibar inazidi kubadilika Kimaendeleo kutokana na kasi kubwa ya miundombinu inayoendelea kuwekwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ikiungwa mkono na Mataifa na Taasisi washirika wa Maendeleo.

Amesema Taasisi na Makampuni ya Korea yanafurahia mabadiliko hayo na kuamua kusaidia ujenzi wa Miradi ya Kielimu akiutolea mfano ule wa Skuli ya Sekondari ya Kwarara uliomalizika hivi karibuni ili kuipa nguvu zaidi Sekta ya Elimu Zanzibar ambayo ndio kichwa cha maendeleo hayo.

Balozi Song Geum Yong alieleza hayo wakati akizungumza na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi Vuga Mjini Zanzibar aliyekuwepo Visiwani Zanzibar katika uzinduzi wa Skuli hiyo pamoja na kuhudhuria maadhimisho ya sherehe za kutimia miaka 53 ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Alisema anapata faraja kuona kuwa ujenzi wa Skuli hiyo uliopata msaada kutoka Shirika la Maendeleo ya Korea { KOICA }, Good Neighbors, Shirika la Utangazaji la Korea { SBS } na Taasisi ya Wasanifu Majengo ya Korea umekwenda sambamba na ujenzi wa Kituo cha Habari cha Kimataifa cha Tumaini.

Balozi Song alieleza kwamba Kituo hicho cha kurekodia Matangazo ya Redio na Televisheni cha Tumaini kilichoanzishwa kwenye Skuli hiyo ya Sekondari Kwarara kwa kiasi kikubwa kitasaidia kutoa Taaluma kwa Wanafunzi pamoja na Wananchi wa sehemu mbali mbali hapa Zanzibar.

Akitoa shukrani zake kwa misaada mbali mbali inayotolewa na Korea kwa Tanzania na Zanzibar kwa jumla Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif alisema Serikali inakusudia kujenga Bara bara ya lami inayoingia kutoka bara bara Kuu hadi kwenye Skuli hiyo ili kuwaondoshea usumbufu wa Mawasiliano Wananchi na Wanafunzi wa eneo hilo.

Balozi Seif alisema Korea ya Kusini inastahiki kupongezwa kwa jitihada zake za kuunga mkono maendeleo ya Zanzibar, lakini hata hivyo alimshauri Balozi Song kutumia maarifa yake katika kuzishawishi Taasisi na Makampuni ya nchi yake kuendelea kuelekeza nguvu zao katika uwekezaji wa sekta tofauti ikiwemo ile ya usafiri wa Baharini.

Alisema sekta ya Kilimo Zanzibar hasa katika upande wa umwagiliaji pia inastahiki kuungwa mkono zaidi ili kuwaongezea nguvu za uzalishaji Wakulima kwa vile zaidi ya asilima 80 ya Wananchi wa Visiwa vya Zanzibar wanaendesha maisha yao kwa kutegemea sekta hiyo.

Othman Khamis Ame
Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar
Balozi Song Kati kati akielezea faraja yake kwa Balozi Seif kutokana na Makampuni na Taasisi za nchi yake kuonyesha azma ya kutaka kusadia maendeleo ya Wananchi wa Zanzibar na Tanzania kwa ujumla.Balozi Seif Kushoto akisisitiza malengo ya SMZ katika kuimarisha miundombinu ya sekta mbali mbali nchini ili kuwajengea maisha bora wananchi wake.Balozi Seif Kushoto akimpatia zawadi ya vyakula vya viungo Balozi wa Korea Kusini Bwana Song mara baada ya kumaliza mazungumzo yao Oisini kwake Vuga Mjini Zanzibar.Picha na – OPMR – ZNZ.Balozi wa Korea Nchini Tanzania Bwana Song Geum Yong akisalimiana na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Vuga Mjini Zanzibar walipokutana kwa kubadilishana mawazo.
Michuzi 

KATIBU MKUU KIONGOZI BALOZI JOHN KIJAZI


Katibu Mkuu kiongozi Balozi John Kijazi akitangaza uteuzi wa viongozi ya Tume ya Uchaguzi, 
Tume ya Maadili  na Majaji wa Mahakama ya Rufaa Ikulu jijini Dar es salaam leo Desemba 22, 2016


PICHA NA IKULU 

Kategori

Kategori