Showing posts with label June 15. Show all posts
Showing posts with label June 15. Show all posts
Picha hizi,Manchester United imekamilisha usajili wa beki Victor Lindelof kutoka Benfica…

Picha hizi,Manchester United imekamilisha usajili wa beki Victor Lindelof kutoka Benfica…

Klabu ya Manchester United imekamilisha usajili wa beki Victor Lindelof ,22 kutoka klabu ya Benfica kwa ada ya Pauni milioni 30.7.
Victor Lindelof ameshawasili Carrington leo kwa ajili ya vipimo vya afya na kukamilisha usajili wa kujiunga na Man United.
Victor amekuwa target ya meneja Jose Mourinho toka January mwaka huu.
 ASANTE KWA KUTEMBELEA MTANDAO WETU!!

from Blogger http://ift.tt/2s4WVUv
via IFTTT


Exclusivee…Alichokisema Irine Uwoya Baada ya Dogo Janja Kumtaka Awe Mpenzi Wake..!!!

Exclusivee…Alichokisema Irine Uwoya Baada ya Dogo Janja Kumtaka Awe Mpenzi Wake..!!!

Wiki kadhaa baada ya Dogo Janja aka Janjaro kuweka wazi kwenye vyombo vya habari kuwa muigizaji Irine Uwoya ndiye anayemkosesha usingizi na angependa siku moja awe barafu wa moyo wake, Uwoya amemfungukia.
Janjaro aliwahi kusema kuwa, “Irene Uwoya nampenda tangu nikiwa mtoto, nimeshabandika sana picha yake maghetoni. Nampendaga sana na ni mtu ambaye nammezeaga mate.”
Muigizaji huyo ambaye amekuwa akitajwa mara kwa mara kwenye nyimbo za wasanii wa Bongo Flava akihusishwa na mfano wa uzuri na mvuto, amekejeli ombi la Janjaro ambaye amedai ni mdogo wake mwenye matatizo yake binafsi.
“Yaani kale jamani… ni mdogo wangu, naongeaga naye tunapiga story. Kananifurahisha lakini, hivyo tu,” Uwoya alisema
Hata hivyo, Uwoya aliweka wazi kuwa katika kumchagua mwandani yake, umri sio kigezo cha kumpima mwanaume anayetaka kuwa naye.
 ASANTE KWA KUTEMBELEA MTANDAO WETU!!

from Blogger http://ift.tt/2seN5hh
via IFTTT


HII NDIYO SHULE YA MSINGI ANAYOFUNDISHA MSANII ROMA MKATOLIKI

HII NDIYO SHULE YA MSINGI ANAYOFUNDISHA MSANII ROMA MKATOLIKI

Msanii wa muziki wa Hip Hop nchini Tanzania, Ibrahim Mussa (Roma Mkatoliki) amegeukiwa kufundisha ambapo jana aliibukia katika Shule ya Msingi Mchikichini iliyopo Mbagala Rangi Tatu jijini Dar es Salaam na kufundisha wanafunzi wa darasa la saba somo la hisabati.
Msanii huyo akiongea na gazeti la MTANZANIA alisema kuwa anafundisha somo hilo kwa wanafunzi wa darasa la saba kwani wengi hufeli kutokana na kuwa na walimu.
  • “Mimi kitaaluma ni mwalimu wa hisabati, kutokana na kufeli mno somo hilo nimeanza kampeni ya kufundisha na kugawa vitabu kwa kuanza na shule hii kwa sababu pia nitakuja kufanya onyesho la muziki kwenye sikukuu ya Eid kwa mara ya kwanza,” alisema Roma.
Mwalimu Mkuu wa shule hiyo, Ramadhan Mashaka alisema kuwa msanii huyo amepata kibali cha kufundisha shuleni hapo.


“Nimekagua na kugundua kuwa Roma ni mwalimu mzuri wa hisabati hivyo tumemkaribisha afundishe wanafunzi bila hofu, tukiwa na imani kubwa kuwa wataelewa kwa sababu wanafundishwa na mtu wanayempenda na hii itaongeza morali ya wanafunzi shuleni hapa,” alisema Mwalimu Juma.

Licha ya kufundisha, atafuturisha watoto yatima wa Kituo cha Nira kilichopo Mbagala Chamazi na atatoa zawadi za sikukuu ya Eid.

from Blogger http://ift.tt/2t62JvI
via IFTTT


RASMI IBRAHIM AJIBU NI MALI YA YANGA

RASMI IBRAHIM AJIBU NI MALI YA YANGA

Mshambuliaji wa Simba, Ibrahim Ajibu imefahamika kuwa sasa ni rasmi anajiunga na Yanga baada ya klabu yake ya sasa kushindwa kufikia nae makubaliano ya kumbakiza kwenye kikosi.
Mabosi wa Simba na mchezaji huyo wameshindwa kuafikiana juu ya makubaliano ya mkataba wake mpya na hiyo imewapa nafasi Yanga waweze kumchukua.
Taarifa kutoka ndani ya Simba imeeleza kuwa wameamua kumruhusu aondoke baada ya mchezaji huyo kuonyesha kutokuwa na nia ya kuendelea kubaki klabuni hapo.
“Tumemwacha aende anakotaka kwenda kwa sababu hana ‘spirit’ tunayoihitaji sisi, acha aende tu sisi mbele kwa mbele,” amesema mtoa taarifa.
Ajib ambaye alianza kutamba Simba akitokea kikosi cha vijana, atatua Yanga aliwa mchezaji huyu kutokana na mkataba wake kuelekea mwishoni.
 ASANTE KWA KUTEMBELEA MTANDAO WETU!!

from Blogger http://ift.tt/2t5PLOp
via IFTTT


Mwanamke amtupa mtoto wake ziwani

Mwanamke amtupa mtoto wake ziwani

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza DCP Ahmed Msangi amemtaja mtuhumiwa huyo kuwa ni Nyamisi Bahati (27) anayedaiwa kumuua mtoto wake aitwaye Sakimu Hassani baada ya kumtupa ziwa Victoria na kupelekea mtoto huyo kupoteza maisha, tukio analodaiwa kulifanya majira ya saa 1:00 usiku ya tarehe 13/06/ 2017.
Inadaiwa mtuhumiwa ambaye ni mama wa mtoto huyo alitoka nyumbani kwa mumewe na kwenda kuwasalimia wazazi wake akiwa na mtoto wake, lakini baadaye alitoka nje akiwa na mtoto kama anakwenda kumbembeleza ndipo baada ya muda kupita alirudi akiwa hana mtoto na kupelekea Mama yake mzazi wa binti huyo kumuuliza mtoto amemuweka wapi ndipo mtuhumiwa alionekana na mashaka huku akishindwa kuonyesha mahali mtoto alipo na baadaye akasema amemtupa kwenye Ziwa Victoria.
Kamanda Msangi amesema baada ya mtuhumiwa kusema hivyo, Bibi wa mtoto alipiga yowe akiomba msaada kwa watu ili waweze kuja kumuokoa mtoto na wananchi walipofika waliweza kutoa taarifa kituo cha Polisi na kuweza kufika eneo la tukio ambapo walishirikiana na wananchi na kufanya kazi ya kumtafuta majini na baadaye walifanikiwa kumpata ila alikuwa tayari ameshapoteza maisha.
Kamanda Msangi ameendelea kusema kuwa uchunguzi wa awali unaonyesha mtuhumiwa wa mauaji hayo anasumbuliwa na matatizo ya akili, japokuwa Polisi wapo katika upelelezi na mahojiano na mtuhumiwa pindi uchunguzi ukikamilika mtuhumiwa atafikishwa mahakamani.
 ASANTE KWA KUTEMBELEA MTANDAO WETU!!

from Blogger http://ift.tt/2s4Kecg
via IFTTT


Roma Aamua Kurudi Kufundisha Shule

Roma Aamua Kurudi Kufundisha Shule

MKALI wa Muziki wa Hip Hop Bongo, Ibrahim Musa ‘R.O.M.A Mkatoliki’ anatarajiwa kuwa mwalimu wa muda wa somo la hisabati leo (Juni 15) katika Shule ya Msingi, Mchikichini iliyopo Mbagala-Kibondemaji jijini Dar.
Akizungumza na Showbiz Xtra , Roma anayebamba na ngoma kibao ikiwemo Viva R.O.M.A Viva, K, Ivan na Kaa Tayari alisema kuwa, ameamua kuchukua nafasi hiyo kwanza kujikumbushia kazi yake ya ualimu aliyokuwa akiifanya zamani ambapo alikuwa mwalimu mzuri wa somo la hisabati.

“Somo la hisabati ni miongoni mwa masomo yanayotengwa sana na wanafunzi wengi hivyo basi nikiwa kama mwalimu niliyepitia kufundisha somo hili, nimeona vyema kuhamasisha wanafunzi walipende na kuliamini. “Nitagawa vitabu vya hesabu kwa wanafunzi wa darasa la saba na pia kuwafundisha somo hilo. Kila mmoja nitahakikisha amehamasika na somo hili na kulipenda kama masomo mengine,” alisema R.O.M.A.

Kesho kufutuRisha Mbali na R.O.M.A kutembelea shule hiyo ya Mchikichiki, kesho (Juni 16) mkali huyo ataelekea katika Kituo cha Watoto Yatima cha Nira ambapo atatoa msaada sambamba na kufuturisha.
Shoo ya Dar Live sasa Naye Meneja na Mratibu wa Uwanja wa Taifa wa Burudani, Dar Live uliopo Mbagala-Zakhem jijini Dar, Juma Mbizo alisema baada ya R.O.M.A kufanya yote hayo ya kijamii, mashabiki wake wote waliommis jukwaani watarajie shoo ya nguvu katika Sikukuu ya Idd Mosi.

“Shoo itatambulika kama Nishushe Dar Live ambapo Roma akiwa na wasanii kibao wakiongozwa na Mr. Blue wataliamsha dude ndani ya Dar Live na kugonga nyimbo zake zote zinazobamba. “Nikukumbushe tu mara ya mwisho kwa R.O.M.A kupiga shoo ya kihistoria ilikuwa mwaka jana katika Mkesha wa Mwaka Mpya ambapo alipanda jukwaa moja na mkali, Darassa na kuzoa kijiji. sasa safari hii jibu utatoa mwenyewe akishuka jukwaani,” alisema Mbizo.
WENGINE SASA

Mbizo aliongeza listi kuwa mbali na Mr.Blue na R.O.M.A mashabiki wategemee jukwaa kufunikwa na wakali wa Hip Hop kama Darassa na Stamina huku Snura akiwarushia vyura jukwaani.
Shoo ya watoto nayo ndani Mbizo aliongeza kuwa, mbali na shoo hizo pia pazia la burudani litafunguliwa Sikukuu ya Idd Mosi mapema kuanzia saa 2:00 asubuhi kwa kundi la sarakasi lisilo na mpinzani Bongo, Wakali Dancers pamoja na wakali wa nyimbo za Asili, Makhirikhiri kutoka Tanzania ambao wataliamsha kwa kutoa burudani kwa watoto.


“Kutakuwa na michezo mingi ya watoto kama vile kubembea, kuteleza, kuogelea, kucheza ndani ya ndege na mingine mingi.

“Katika kunogesha burudani kwa watoto, kwa mara ya kwanza mkali wa vichekesho anayebamba katika Kipindi cha Ze Comedy, Bambo atakuwepo kuvunja mbavu za watoto wote watakaojitokeza huku akigawa zawadi ndogondogo kwa watakaotoka chicha.

Zanzibar Stars kuibuka Baada ya kupotea kwa muda, kundi kongwe la Muziki wa Mwambao, Zanzibar Stars linatarajiwa kuibuka kwa mara ya kwanza ndani ya Dar Live likiwa na vichwa hatari kama Bi. Mwanahawa, Sabaha Mchacho, Jokha Kassim, Mosi Suleiman, Ally Jay, Zubeda Mlamali na wengine kibao. Mtonyo sasa! Mbizo alimaliza kwa kutaja kiingilio kwa siku hiyo kuwa, burudani kwa wakubwa itakayoanza saa 2:OO usiku itakwenda kwa shilingi 7,000 huku watoto ikiwa shilingi 3,000 tu!

from Blogger http://ift.tt/2s4KlVp
via IFTTT


Kategori

Kategori