Showing posts with label Bondeni. Show all posts
Showing posts with label Bondeni. Show all posts
Vyuo vikuu zaidi ya 10 vyafungwa kwa muda Afrika kusini

Vyuo vikuu zaidi ya 10 vyafungwa kwa muda Afrika kusini


Makundi ya watu wakiandamana  Johannesburg, South Africa.
Makundi ya watu wakiandamana Johannesburg, South Africa.
Karibu vyuo vikuu 14 vya Afrika kusini vimefungwa kwa muda wakati wa kuongezeka kwa wimbi la malalamiko na maandamano ya wanafunzi   kutokana na mapendekezo ya kuongezwa kwa ada. Maandamano hayo yamepelekea mapambano Jumatano kati ya wanafunzi na polisi nje ya bunge huko Capetown.
Malalamiko yalianza wiki iliyopita katika chuo kikuu cha Witwatersrand huko Johannesburg baada ya mapendekezo ya ongezeko la asilimia 10. Toka wakati huo ujumbe wa Twitter “ada lazima ipungue”umesambaa kwenye mitandao ya kijamii  na malalamiko yametapakaa katika taasisi tofauti ikiwa ni pamoja na chuo kikuu mashuhuri cha Capetown, chuo  kidogo cha kiliberali Rhodes na kile cha nje ya mji Fort Hare.
Maandamano hayo yamelazimisha viongozi wa vyuo vikuu kukutana wiki hii na waziri wa elimu ya juu na mafunzo Blade Nzimande katika jaribio la kutafuta suluhu.
Afrika Kusini yakana kutoa hongo kwa FIFA

Afrika Kusini yakana kutoa hongo kwa FIFA


Afrika kusini
Afrika kusini imekana kwa mara nyengine tena kwamba ilitoa hongo ili kupewa maandalizi ya kombe la dunia la mwaka 2010.
Waziri wa michezo nchini humo Fikile Mbalula, amewaambia wanahabari kwamba Afrika kusini itashirikiana na wachunguzi kutoka Marekani lakini imekataa kuingizwa katikati ya ugomvi kati ya FIFA na Marekani.
Amesema kuwa dola millioni 10 zilizotolewa zilikuwa malipo ya kusaidia soka miongoni mwa raia wa Afrika wanaoishi katika visiwa vya Caribbean na yalilipwa miaka kadhaa baada ya michuano hiyo kuandaliwa na Afrika kusini.
  Historia nyingine kubwa ya Tanzania imeandikwa fainali ya #BBAHotshots 2014

Historia nyingine kubwa ya Tanzania imeandikwa fainali ya #BBAHotshots 2014

IdrisLeo ni siku ya 63 tangu yaanze mashindano ya Big Brother Africa, ndiyo siku ambayo imefanyika fainali ya #BBAHotshots kwa mwaka huu 2014.
Labda nikukumbushe kwamba Tanzania ndiyo nchi pekee iliyokuwa imebakiwa na mshiriki wake ndani ya Jumba la BBA katika ukanda wa Afrika Mashariki na tuliona namna ambavyo mastaa wengi wakitoa support kubwa kwa mshiriki huyo ambaye ni Idris.
Hatimaye usiku huu wa Desemba 07 historia nyingine imeandikwa Afrika, ambapo mwakilishi huyo kafanikiwa kuibuka mshindi.
Nimepita katika kurasa za mastaa mbalimbali Twitter, hiki ndicho kilichoandikwa na mastaa hao;

Kategori

Kategori