Showing posts with label 2017 at 10:28AM. Show all posts
Showing posts with label 2017 at 10:28AM. Show all posts
Ujerumani waisulubu San Marino, huku Lewandoski akifunga hattrick.
Kikosi cha timu ya taifa ya Ujerumani kikiwa nyumbani waliikaribisha timu ya taifa ya San Marino katika mchezo ambao San Marino waliishia kudhalilika baada ya kupewa zigo la mabao saba kwa nunge kutoka kwa vijana hao wa Joachiem Low.
Alianza Julian Draxler dakika ya 11 kuishushia kipondo San Marino na baadae Sandro Wagner akfunga mara mbili na Amin Younes akafunga mara moja na kuufanya mchezo huo kwenda mapumziko Ujerumani wakiongoza mabao manne kwa sifuri.
Kipindi cha pili mlinzi wa klabu ya Arsenal Shkordan Mustafi alifunga bao la 5, Julian Brandit akafunga la 6 kabla ya Sandro Wegner kufunga bao lake la 3 katika mchezo huo na la 7 kwa timu ya taifa ya Ujerumani, lakini kule Norway nako timu yao ya taifa ilitoka sare ya moja moja na Czech Republic.
Montenegro nao walikuwa nyumbani kuikaribisha Armenia ambapo Montenegro waliibuka kidedea kwa kuibamiza Armenia jumla ya mabao manne kwa huku Steven Jovetic akiifungia Montenegro hat trick na lile lingine likiwekwa kambani na Fatos Beciraj na la Armenia likifungwa na Rusian Koryan.
Poland nao wakiwa nyumbani waliikaribisha Romania ambapo katika mchezo huo mshambuliaji wa klabu ya Bayern Munich Robert Lewandoski aliibuka shujaa wa Poland baada ya kufunga mabao yote matatu na lile la kufutia ,achozi la Romania likifungwa na Bogdan Stancu.
ASANTE KWA KUTEMBELEA MTANDAO WETU!!
from Blogger http://ift.tt/2sPFRQP
via IFTTT
Stars imeanza safari ya AFCON 2019 kwa sare
Timu ya taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ imeshindwa kupata ushindi kwenye mechi ya kwanza dhidi ya Lesotho kuwania kufuzu kucheza fainali za mataifa ya Afrika mwaka 2019.
Stars ilitangulia kupata goli la kuongoza dakika ya 27 kipindi cha kwanza likifungwa na mshambuliaji tegemeo Mbwana Samatta kwa mpira wa adhabu ndogo baada ya beki wa kushoto Gadiel Michael kufanyiwa madhambi nje kidogo ya eneo la penati box.
Samatta alipiga mkwaju wa moja kwa moja uliomshinda golikipa wa Lesotho Likano Mphuti na kujaa nyavuni kulia kwa golikipa huyo.
Haikuchukua dakika nyingi, Lesotho wakasawazisha bao hilo dakika ya 36 kipindi cha kwanza baada ya uzembe wa safu ya ulinzi wa Stars na kutoa nafasi kwa Likano Mphuti kufunga bao.
Lesotho baada ya kupata bao walianza kucheza kwa tahadhari, wakijilinda na kupoteza muda kulinda matokeo ya sare ya 1-1 na kuambulia pointi moja ugenini.
Matokeo hayo yamedumu hadi dakika 90 zinamalizika na Stars imeambulia pointi moja kwenye mchezo huo.
Kikosi cha Stars kiliongozwa na Aishi Manula, Shomari Kapombe, Gadiel Michael, Abdi Banda, Salim Mbonde, Himid Mao, Simon Msuva/Farid Musa Mzamiru Yassin/Salum Abubaka, Thomas Ulimwengu/Mbaraka Yusuph, Mbwana Samatta na Shiza Kichuya.
Wachezaji wa benchi ambao hawakutumika: Said Mohamed, Hassan Ramadhani Kessy, Erasto Nyoni na Nurdin Chona.
ASANTE KWA KUTEMBELEA MTANDAO WETU!!
from Blogger http://ift.tt/2refGGA
via IFTTT
Huwezi amini, Giroud ni hatari kuliko Lukaku, Sanchez, Kane na Ibrahimovich.
Kila mshabiki wa soka akiulizwa kuhusu yupi mshambuliaji hatari zaidi Uingereza baasi jina la Romelu Lukaku, Diego Costa, Zlatan Ibrahimovich na Alexis Sanchez ni lazima yatakuwepo miongoni mwa majina yatakayotajwa.
Lakini sivyo, takwimu zinaonesha washambuliaji hao wako juu tu kutokana na muda mrefu wanaopewa uwanjani na pia kutokana na mipira ya adhabu kama faulu na penati ndio vinawaweka juu sana.
Lakini Olivier Giroud ni hatari zaidi yao, takwimu hazidanganyi. Takwimu zinaonesha Olivier Giroud ndio mshambuliaji ambaye hutumia dakika chache zaidi kucheka na nyavu kwani magoli yake 9 ameyafunga kwa kila baada ya dakika 88.11 alizokuwa uwanjani.
Wakati kinara wa magoli EPL Romelu Lukaku ametumia dakika 125.57 kwa kila goli alilofunga, hii inamaanisha Lukaku anatumia muda mwingi sana kuweza kufunga tofauti na Giroud ambaye humchukua dakika chache tu kucheka na nyavu.
Pengine Giroud angepewa nafasi na dakika sawa za uchezaji kama Lukaku ingekua sasa amempita Mbelgiji huyo kimagoli, Harry Kane yuko nafasi ya pili ya washambuliaji ambao hutumia dakika chache zaidi kucheka na nyavu huku yeye akitumia dakika 99.68.
Sergio Kun Aguero naye yumo katika nafasi ya tatu huku yeye hutumia dakika 124.8 kwa kila goli alilofunga, Lukaku yuko nafasi ya nne lakini chini yake yupo Alexis Sanchez ambaye naye hutumia dakika 136.06 kwa kila goli alilofunga msimu huu.
Zlatan Ibrahimovich yeye hutumia dakika 146.25 kwa kila goli alilofunga, na nafasi ya 6 yuko mshambuliaji wa Chelsea Diego Costa ambaye yeye hutumia dakika 146.29 kwa kila goli alilofunga msimu huu.
from Blogger http://ift.tt/2oHmNoY
via IFTTT
Subscribe to:
Posts (Atom)
