Showing posts with label 2017 at 06:00PM. Show all posts
Showing posts with label 2017 at 06:00PM. Show all posts
Hivi Ndivyo Gwajima Alivyotua Kilimanjaro kwa Ajili ya Kazi ya Kuuaga Mwili wa Ndesamburo..!!!

Hivi Ndivyo Gwajima Alivyotua Kilimanjaro kwa Ajili ya Kazi ya Kuuaga Mwili wa Ndesamburo..!!!

Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima amewasili katika viwanja vya Majengo, Moshi kwa ajili ya kuuaga mwili wa aliyekuwa Mbunge wa Chadema, Phillemon Ndesamburo.
Tayari mwili wa Ndesamburo umewasili katika viwanja vya Majengo na kupokelewa na baadhi ya viongozi wa Chadema.
Mwili wa Ndesamburo ambaye pia aliwahi kuwa mbunge wa Moshi Mjini,utaagwa katika viwanja hivyo na leo saa 10 jioni utapelekwa nyumbani kwake kwa ajili ya taratibu za mazishi.
Wabunge na Viongozi mbalimbali wa Chadema, akiwamo muasisi wa chama hicho, Edwin Mtei, Frederick Sumaye wapo uwanjani hapo kwa ajili ya kumuaga Ndesamburo

from Blogger http://ift.tt/2s9e9RK
via IFTTT


Zitto: NECTA Limesema hawana rekodi ya Albert Bashite wala Paul Makonda

Tumejulishwa kwenye Kamati kuwa NECTA hawana rekodi ya Albert Bashite wala Paul Makonda.
Yani wote hawapo kwenye kanzidata ya Baraza la Mitihani. Kwamba Tanzania haijawahi kuwa na wanafunzi wenye majina hayo 
TAZAMA HARMORAPA ALIVYO TIMUA MBIO BAADA YA KUIONA BASTOLA

from Blogger http://ift.tt/2o7s4pg
via IFTTT


Majambazi wateka Magari matano na Kupora Fedha Kibiti

Watu sita wanaosadikiwa kuwa majambazi wakiwa na silaha wameteka magari matano na kupora Sh920, 000 na simu saba za mkononi katika eneo la Kitembo nje kidogo ya mji wa Kibiti.
Image result for bus car
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, Onesmo Lyanga alisema tukio hilo lilitokea juzi saa moja usiku na kwamba abiria walioporwa walikuwa wakisafiri kwenye barabara itokayo Dar es Salaam kwenda Mtwara.
Aliwataja waliojeruhiwa kuwa ni Issa Juma, Nassoro Mohammed, Kassim Omari, Issa Juma na Khalifa Mohammed, wote wakazi wa Dar es Salaam. Wengine waliojeruhiwa ni Badru Uwesu mkazi wa Kisemvule, Mkuranga na Edward Safari, mkazi wa Morogoro.
Kaimu Mganga Mkuu wa Hospitali ya Mchukwi walikopelekwa majeruhi, Dk Japhet Guzuye alisema walikuwa na majeraha shavuni, migongoni na shingoni na walitibiwa na kuruhusiwa kuondoka.
TAZAMA JAMAA HUYU ALIVYOKOSWA KOSWA NA KIFO KWA AJARI MTONI

from Blogger http://ift.tt/2nM9ItJ
via IFTTT


Wananchi waandamana na Maiti Kahama, Wachimba Kaburi Ofisini kwa Diwani

Kahama. 
Wananchi wa Kata ya Mhongolo mjini hapa jana waliandamana bila kibali wakiwa na jeneza la mtoto aliyefariki mtaani hapo kwa lengo la kwenda kuuzika mwili huo kwenye Ofisi ya kata hiyo wakidai diwani wa kata hiyo, Michael Mizubo ameuza eneo la makaburi kwa maslahi yake binafsi.
Mmoja wa wananchi hao aliyejulikana kwa jina moja la Paulina ambaye alikuwa akiongoza maandamano hayo, amesema waliamua kwenda kuzika mwili huo wa mtoto huyo aliyejulikana kwa jina moja la Rosemary aliyefariki kwa ugojwa wa kawaida kwenye ofisi hiyo ya kata, kwa sababu hakuna eneo la kuzika.
Hata hivyo wakati wanachimba kaburi hilo kwenye mlango wa ofisi ya diwani huyo kwa lengo la kuuzika mwili huo polisi walifika na kuwatawanya kwenye eneo hilo kwa madai ni ukiukwaji wa taratibu.
Kwa upande wake diwani wa kata hiyo Mizubo anayedaiwa kuuza eneo la maziko amesema wananchi hao walikuwa na sababu zao za kisiasa kwani pamoja na eneo hilo la makaburi kuuzwa tayari kuna eneo jingine limetengwa kwa ajili ya maziko hayo.


DOWNLOAD APPS YA TZTOWN HAPA

http://ift.tt/2ms2574
WANANCHI WAOMBA SERIKALI KUODOA TAKA KIZIMBANI MAKAMBAKO MKOANI NJOMBE


from Blogger http://ift.tt/2msRrhd
via IFTTT


Kategori

Kategori