Showing posts with label 2017 at 01:52PM. Show all posts
Showing posts with label 2017 at 01:52PM. Show all posts
Mimi na Diamond Tuna Mahusiano zaidi ya Kimapenzi – Jackline Wolper

Mimi na Diamond Tuna Mahusiano zaidi ya Kimapenzi – Jackline Wolper

Muigizaji Jackline Wolper amesema yeye na msanii Diamond Platnumz wana uhusiano wao ambao ni kiwango cha juu kwani wamekuwa wakishirikiana katika mambo mengi.
Katika segment ya kikaongoni inayorushwa na EATV (facebook) inayotoa fursa kwa watu kumuuliza mgeni maswali, moja ya swali lilitaka kujua ni iwapo Wolper alishakuwa na uhusiano wa kimapenzi na Alikiba, Jux, Ray Kigosi na Diamond Platnumz.
“Alikiba ndiyo, Jux alikuwa rafiki yangu wa karibu, Ray Kigosi yule ni kaka yangu namuheshimu sana, Diamond tuna mahusiano zaidi ya kimapenzi, yaani kikazi.
“Diamond tuna mahusiano mengi sana zaidi hata ya kimapenzi, ni bosi wangu, rafiki yangu, mshauri wangu, yaani na mahusiano nae mengi, umenielewa?, kikazi na vitu vingi,” amejibu Wolper.
Katika hatua nyingine muugizaji huyo amesema kinachomzuia kufanya movie na wasanii wa nje ni kutojua kingereza kwa ufasaha zaidi kitu ambacho ameanza kukifanyia kazi.
“Na wish kufanya hivyo lakini kidogo lugha gongano, ndio maana kuna mwalimu wangu huwa anakujaa kila saa 10 pale ofisini kwa hiyo sasa hivi kidogo naprove, kujua lugha kikweli hiyo ndio dream yangu sana kwa sababu kuna wasanii wa nje nawapenda na ninaamini naweza kufanya nao kazi, kwa hiyo nikiwa kwenye zile level zile za juu nitafanya,” ameleeza Wolper.

from Blogger http://ift.tt/2qfzUiq
via IFTTT


Simba Yahaha Kutafuta Point Tatu za Bure…Yamkatia Rufaa Mchezaji wa Kagera Sugar

Simba Yahaha Kutafuta Point Tatu za Bure…Yamkatia Rufaa Mchezaji wa Kagera Sugar

Uongozi wa mabingwa wa kihistoria Simba Sc imewasilisha rufaa Kwa Bodi ya ligi shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kudai pointi za mchezo dhidi ya Kagera Sugar uliochezwa Jumapili ya wiki iliyopita Kaitaba Bukoba na Simba kufungwa kwa magoli mawili kwa moja (2-1) na Kagera Sugar.
Katika Barua ya Simba imedai Kagera Sugar ilimtumia mchezaji Mohamed Fakhi mwenye kadi tatu za njano ambazo ni kukiuka kanuni na taratibu za ligi kuu ya Vodacom .
Kamati ya masaa 72 leo itakaa kupitia rufaa mbalimbali zilizowasilishwa kwenye kamati mojawapo ni hii rufaa ya Simba Kwa Kagera Sugar
Wakati haya yakifukuta uongozi wa Kagera Sugar umejitokeza na kukana rufaa hiyo, kocha wa Kagera sugar Mecky Maxime alisema: “Mimi niko makini sana na masuala ya kadi za wachezaji wangu, kila mchezaji wangu anapoonyeshwa kadi naandika na pia namkumbusha meneja wangu naye kuandika kadi, Simba kama wameshindwa kutafuta pointi uwanjani wasitafute sababu ya kupata pointi za mezani”
Pia Meneja wa kikosi hicho ambaye amesema Fakhi ana kadi mbili tu za njano na si tatu Kama wanavyosema

from Blogger http://ift.tt/2nROnfb
via IFTTT


BREAKING News: Mahakama kuu yaamuru Mbunge wa Chadema aliyefungwa miezi 6 jela aachiwe huru

Mahakama Kuu Dar es Salaam imetengua hukumu iliyotolewa na Mahakama ya W/Kilombero dhidi ya Mbunge Peter Lijualikali, amekutwa hana hatia.
Mahakama Kuu kanda ya Dar ES Salaam imetengua hukumu iliyotolewa na Mahakama ya Wilaya Kilombero dhidi ya Mbunge Peter Lijualikali baada ya kukubaliana na warufani kwamba hati ya mashtaka iliyomtia hatiani ilikuwa na upungufu.
Uamuzi huo umetolewa leo mbele ya Jaji Ama- Isaria Munisi baada ya kupitia sababu za kupinga mbunge huyo kutiwa hatiani na kuhukumiwa kifungo cha miezi sita jela.
Peter aliwakilishwa mahakamani na Wakili Tundu Lissu na Fred Kiwelo wakati Jamhuri ilikuwa ikiwakikishwa na Wakili wa Serikali, Faraja Nchimbi.
Mshtakiwa mwingine aliyehukumiwa kifungo cha nje, Stephani Mgatta adhabu yake pia imetenguliwa.
January 2017, Mahakama ya wilaya ya Kilombero ilimuhukumu kwenda jela miezi sita Mbunge wa jimbo la Kilombero, Peter Lijualikali (30) kwa kosa la kufanya fujo na kusababisha taharuki katika maeneo ya ukumbi Wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero.
Mwendesha mashtaka inspekta wa Polisi Dotto Ngimbwa aliiambia Mahakama kuwa mshtakiwa, akiwa mshtakiwa namba moja pamoja na mwenzie Stephano Mgata (35) walitenda kosa hilo machi mosi mwaka 2016 kwenye kikao cha Baraza la Madiwani katika eneo la Kibaoni ukumbi wa Halmashauri ya wilaya ya Kilombero.
Kufuatia ushahidi uliotolewa mahakamani hapo, Hakimu mkazi katika mahakama ya wilaya ya Kilombero Timothy Lyon aliwatia hatiani washtakiwa hao walipatikana na makosa. Aidha, Hakimu alisema kuwa mshtakiwa wa kwanza ambaye ni Mbunge ambaye alikuwa na kesi tatu huko nyuma atatumika kifungo cha miezi sita jela kwa kuwa anaonekana kuwa mkosaji mzoefu.
Hata hivyo Mahakama hiyo iliona kwa kuwa mshtakiwa wa pili Stephano Mgata (35), hili ni kosa lake la kwanza amehukumiwa kifungo cha miezi sita nje ambapo ndani ya kipindi hicho cha miezi sita hatotakiwa kutenda kosa lolote la jinai.
Tazama video Mtoto amvua kofia Papa Francis

from Blogger http://ift.tt/2okompp
via IFTTT


Hatarii..Prof Lipumba Azidi Kumganda Maalim Seif,Adai ni Msaliti..!!!

Mwenyekiti wa CUF anayetambulia na Ofisi ya Msajili wa Vyama Siasa, Profesa Ibrahim Lipumba amemlalamikia Katibu Mkuu wa chama hicho, Maalim Seif Sharrif Hamad kufungia akaunti zote za chama hicho za wilaya.
Akizungumza kwenye kikao cha baraza la uongozi linaloongozwa na upande wake, Profesa Lipumba amesema kutokana na uamuzi huo ruzuku ya chama kutoka serikalini wameikosa.
Mwanasiasa huyo amesema CUF ipo katika mtihani kwa sasa, hivyo uwapo wa Maalim katika kikao hicho ungesaidia kuiimarisha.
“Wajumbe nawashukuru kwa kuja ili kupata fursa ya kujenga chama. Chama chetu kipo ndani ya mtihani ambao kwa kweli chanzo chake ni katibu mkuu wetu kutoheshimu katiba yetu na kutoheshimu taratibu za kidemokrasia,” amelalamika Profesa Lipumba.
Amesema kuwa Maalim Seif alitakiwa kuhudhuria kikao hicho na alipewa taarifa lakini hakuweza kufika, hali iliyosababisha majukumu yake kusimamiwa na Naibu Katibu Mkuu wa CUF (Tanzania Bara), Magdalena Sakaya kama katiba yao inavyoelekeza.
“Fedha zimekwama kwenye mabenki hasa NMB kwa sababu akaunti za wilaya zinafunguliwa na kamati za utendaji za wilaya, hazifunguliwi na makao makuu, lakini wenzetu wametumia mitandao ya wapambe wao kutoa shinikizo zifungwe,” amesema.
Akijibu tuhuma hizo, Naibu Katibu Mkuu wa CUF (Zanzibar), Nassor Mazrui amesema kuwa hatua ya kufunga akaunti za benki imelenga kulinda fedha ya chama ili zisitumiwe vibaya na upande wa Profesa Lipumba.
Profesa Lipumba yupo kwenye mgogoro na CUF baada ya kuandika barua ya kujiuzulu na baadaye kuifuta, lakini mkutano mkuu ulikubali kujiuzulu kwake na kuteua kamati ya uongozi chini ya Julius Mtatiro.
Hata hivyo, Msajili wa Vyama vya Siasa bado anamtambua kwa madai kuwa hakutaarifiwa kuhusu uamuzi huo na kwamba, baadhi ya taratibu hazikufuatwa, msimamo ambao CUF chini ya Maalim Seif imeukataa.
TAZAMA HARMORAPA ALIVYO TIMUA MBIO BAADA YA KUIONA BASTOLA

from Blogger http://ift.tt/2noZcaK
via IFTTT


Kategori

Kategori