WIZARA YA AFYA NA USTAWI WA JAMII YAZINDUA DAWA ZA KUTIBU UGONJWA WA KUHARISHA NA NIMONIA JIJINI DAR ES SALAAM





Katibu mkuu wa wizara ya afya na ustawi wa jamii pichani Juu  Dkt. Donnan Mmbando akihutubia washiriki siku ya uzinduzi 

Katibu mkuu wa wizara ya afya na ustawi wa jamii pichani Juu  Dkt. Donnan Mmbando akionyesha dawa iliyozinduliwa  ZINK na ORS octoba,10, 2015 katika ukumbi wa blue pear hotel jijini Dar es Salaam  







Dkt.Benson Bana akisaini kitabu cha wageni kwenye moja ya banda la maonyesho siku ya uzinduzi 

Kaimu Mganga mkuu wa serikali dkt. Magreth Mhando Hapo juu akihojiwa na waandishi wa habari siku ya uzinduzi wa dawa ya ZINK na ORS inayotibu ugonjwa wa kuharisha na  amoxicilini,Inayotibu  ugonjwa wa nimonia   

                   Dkt Jojina Msemo Picha juu kulia akitoa maelezo kwa ufupi kuhusu dawa za kutiu kuharisha na nimonia
Washiriki wa warsha ya uzinduzi wakiwa katika ukumbi wa blue pear hotel jijini Dar es Salaam  

Kaimu mganga mkuu wa serikali dkt.Magreth Mhando akitembelea mabanda ya maonyesho siku ya uzinduzi
Tadashi Yasuda Kutoka unicefu shirika la kuhudumia watoto duniani akionyesha dawa za Kuia kuharisha na nimonia siku ya uzinduzi
Tadashi Yasuda Kutoka Unicef   shirika la kuhudumia watoto duniani  akihutubia waganga wakuu wa mikoa na wilaya Tanzania bara siku ya uzinduzi jijini Dar es Salaam

                                                                             
 washiriki katika semina ya uzinduzi wa dawa za kutibu ugonjwa kuharisha na nimoni ZINKI ORS na AMOXILIN


                            Baadhi ya maonyesho yaliyofanyika siku hiyo ni pamoja na onyesho la kunawa mikono kwa usasahihi kabala ya kumpa huduma mgonjwa wa kuhara  

 
Uzinduzi wa ziora ulifanyika September,10 2015 katika hotel ya blue pear jijin Dar es salaam ulihusisha washiriki kutoa mikoa ya Tanzania bara ambao ni waganga wakuu wa mikoa na wilaya ambapo mgeni rasmi alikuwa ni katibu mkuu wizazara ya afya na ustawi wa jamii dkt.Donnan Mmbando 

Akihutubia siku ya uzinduzi dkt Mmbando alisema  sababu kubwa ya kuzindua dawa hizo ni licha ya kuwa zimekuwa zikitumika kwa muda mrefu ni kutokana na kuwa kwa sasa zimeboreshwa kwa kiwango kikubwa baada ya maendeleo ya ugunduzi yaliyotokana na tafiti za kisayansi 

Aliwaagiza  watendaji wakuu wa idara ya afya, kuhakikisha upatikanaji usambazaji na matumizi sahihi ya dawa za zinki ors na amoxilin ziora katika maeneo yao ya kazi 

Alisema Amoxicillin iliyozinduliwa leo ni aina ya kidonge kinachoyeyuka haraka na ni rahisi kuihifadhi na kusafirisha pia, ukilinganisha na dawa ya zamani iliyokuwa katika chupa na ORS na Zinki zimefungashwa pamoja Aliongeza Utafiti wa hivi karibuni, umeonyesha kuwa watoto wanaoharisha wanaopata ORS ni asilimia 47; wakati idadi ya watoto wanaopata zinki iko chini kwa asilimia 4.7 pekee.

Mmbando pia alisema kuwa Tanzania imepata mafanikio makubwa katika kupunguza vifo vya watoto chini ya miaka mitano licha ya kueleza kuwa kwa sasa changamoto ni magonjwa ya nimonia na kuharisha

Dr jojina msemo kaimu mkurugezi wa kinga wizara afya na ustawi wa jamii aliwasisitiza watendaji wa afya  kuhakikisha wanafanikisha upatikanaji wa dawa hizo katika maeneo yao kwa kuomba dawa hizi kwa mfamasia

Naye mkurugenzi msaidizi kitengo cha elimu ya wizara ya na ustawi wa jamii Helen semu alieza na njia inayotumika kufikisha elimu kwa jamii kuhusina na upatikanaji na matumizi ya dawa hizo kuwa ni pamoja na kutmia vyombo vya habari na njia ya simu za mkononi


Tadashi yasuda Kutoka unicefu shirika la kuhudumia watoto duniani  alizungumzia ukubwa wa tatizo la ugonjwa wa nimonia na kuharisha na kubainisha mikakati ya   kupunguza vifo vya watoto chini ya miaka mitano kimataifa kuwa ni kuendelea kusisitiza matumizi ya dawa

kila mtoto mwenye nimonia anapashwa kupata dawa ya amoxicilini, nakila mtoto anayeharisha anapaswa kupata ORS na Zinki. Dkt. Thomas Lyimo, wa shirika la kuhudumia watoto UNICEF Alieleza namna wadau mbalimbali wakiwemo UNICEF, watakavyoshiriki katika kuhakikisha dawa hizi zinamfikia kila mtoto anayestahili