ZOEZI LAKAMILIKA WILAYANI WANGING'OMBE

Wanging’ombe

HALMASHAURI ya Wanging’ombe Mkoani Njombe imefanikiwa kuwaandikisha  Zaidi watu 80 Elfu na kuvuka lengo la asilimia 66 za lengo ambapo kulitarajiwa kuandikishwa watu 48,000 mpaka wanapo hitimisha uandikishwaji katika daftari la kudumu la mpiga kura kwa mfumo wa Kierekroniki BVR.

Akizungumza na Elimtaa Blog juu ya uandikishwaji katika afisa Uchaguzi halmashauri ya Wangimbombe, Christopher Masaaka, alisema kuwa katika halmashauri yake wamefanikiwa kuwaandikisha wananchi zaidi ya lengo walikokuwa wamejiwekea.

Alisema kuwa halmashauri hiyo ilikisia kuwaandikisha wananchi 48,866, na kuwa wanawake watitarajia kuwaandikisha 26, 995 na wanaume 21871 na kuwa ongezeo ni sawa na asilimia 66 na kuandikisha kwa alimimia 166.5.

Alisema kuwa zoezi hilo limefanikiwa kwa alisilimia 166 ya lengo ambalo halmashauri ambalo ilikuwa imejiwekea na kusema kuwa hii imetokana na mwitikio wa wananchi katika kujiandikisha.

Masaaka alisema kuwa wanauhakika wa kuwaandikisha wananchi wote katika halmashauri hiyo kwa kuwa kadri siku zilivyo kuwa zikienda watu walikuwa wakipungua na kuwa mpaka siku ya mwisho katika vituo watu walio andikishwa walikuwa hawazidi watano.

Alisema kuwa kwa wale ambao watakuwa hawajajiandikisha itakuwa ni upendo wao kutokan ana zoezi hilo kuendeshwa kwa uhuru na kuto mrazimisha mtu na kuwa watu wote walio pika katika vitua waliandikishwa.

“Kunavituop katika kata ya Igima tulilazimika kuongeza mashine kutokana na idadi ya watu waliyo kuwa wamejitokeza na kumaliza watu wate walio kuwa wamefika katika vituo vya kujiandikisha,” alisema Masaaka.

Alisema kuwa halmashauri hiyo imefanikiwa kuwaandikisha wananchi 81,491 ambapo wanaume wakiwa 36,595 sawa na asilimia 44.91 na wanaume 44896 sawa asilimia 55.09 na kuzidi lengo walilokuwa wamejiwekea.

Zoezi hilo katika halmashauri hiyo lilimalizika juzu na takwimu za watu walio jiandikishwa kwa ujumla kutolewa jana kukiwa na hakuna malalamiko ya mtu kuachwa bila kuandikishwa katika daftari hilo.