Mafuriko yasomba basi la abiria Mandera


Basi lasombwa na mafuriko
Maafisa wa shirika la msalaba mwekundu kaunti ya Mandera kazkazini mwa Kenya wanasema kuwa takriban watu 16 wametoweka baada ya basi kusombwa na mafuriko kilomita chache kutoka mji huo.
Mvua kubwa iliripotiwa kunyesha katika eneo la mji huo na viunga vyake mapema Alhamisi.
Katibu mkuu wa shirika la msalaba mwekundu Abbas Gulet anasema kuwa wamewaokoa watu 42 kufikia sasa.
Basi hilo liliondoka mjini Mandera likielekea jijini Nairobi mapema siku ya jumatatu kabla ya kukwama katika matope.
Baadaye mvua kubwa ilinyesha na mafuriko kulisomba basi hilo.
Maafisa wa msalaba mwekundu wanasema kuwa wameanza kuwasaka watu waliotoweka katika mto mmoja uliopo ambapo mafuriko hayo yanaelekea.