Ashtakiwa kwa kumtia mimba mwanawe


Mahakama ya kenya
Mahakama moja mjini Bungoma nchini Kenya imemshtaki afisa mmoja wa wadi ya Bukembe kwa kulala na mwanawe wa kike mwenye umri wa miaka 14 kwa zaidi ya miaka miwili baada ya mkewe kufariki mwaka 2013.
Kulingana na gazeti la The Standard nchini Kenya,mwathiriwa ambaye ni mjamzito wa miezi minne amesema kuwa mshukiwa huyo ambaye ni babaake amekuwa akimlazimisha kufanya mapenzi naye kila usiku na kumuonya kwamba angemdhuru iwapo angemwambia mtu yeyote.
''Babaangu pia ameninyima fursa ya kwenda katika shule ya upili licha ya mimi kufanya vyema katika mtihani wa KCPE. Mwaka 2013,nilifanya vyema lakini akanilazimisha kurudia darasa. Mwaka jana nilifanya vizuri zaidi lakini anadhani kwamba iwapo nitajiunga na shule ya upili ya bweni,nitamkosesha fursa ya kufanya tendo la ngono nami'',.Mwathiriwa aliiambia mahakama.
Hakimu mwandamizi Peter Ireri alimwachilia mtuhumiwa kwa dhamana ya shilingi laki moja ama pesa taslimu shilingi elfu ishirini.