Wakulima wa Chai kupatiwa ufumbuzi wa Migogoro


WAKULIMA wa chai Nyanda za juu kusini na Tanzania kwa Ujumla wanatarajiwa kunufaika na mfumo wa kuweka kumbumbu zao katika mtandao na kuwa wazi kwa kila mkulima na bodi ya chai.



Akizungumza na Waandishi wa habari  wakati wa kutoa mafunzo kwa wawakilishi wa viwanda vya chai, wawakilishi wa wakulima, na vyama vya wakulima kuhusiana na mfumo huo, afisa mkaguzi mkuu, Bodi ya Chai, Fahari Marwa, amesema kuwa mfumo huo utapunguza matatizo mbalimbali yaliyo kuwa yakitokea baina ya wakulima na viwanda.



Marwa amesema kuwa Bodi ya Chai imeamua kufungua mfumo huo ili kupambana na viwanda na wanunuzi wanao waibia wakulima na kuwa mfumo huo utasaidia kuweka wazi taarifa za wakulima kwa bodi hiyo na kutatua migogoro ya maripo kwa urahisi.



Amesema kuwa mfumo huo inatarajiwa kutatua migogoro ambayo imekuwa ikijitokeza baina ya wakulima na viwanda hasa makato ya mikopo ya pembejeo, na malipo ya pili kwa mkulima.



Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya Njombe Sarah Dumba amesema kuwa mfumo huo utasaidia kuondoa matatizo ambayo yamekuwa yakitokea mara kwa mara na utaepusa manungu’uniko kwa wakulima.



Amesema kuwa wakulima wamekuwa wakiyakosa malipoi ya pili ambapo malipo hayo yamekuwa wakiliwa na wajanja ambao wapo katikati ya wakulima na viwanda katika vikundi vyao.