Askofu Cliopa Azikwa Kanisani Njombe, Ona Picha zaidi ya 20 mazishi yalivyoenda, na sikia alicho zungumza Askofu Malasusa

  • Mamia wamsindikiza Askofu Cliopa.
  • Waongozwa na kiongozi Mkuu wa KKKT Malasusa.
  • Amezikwa maeneo ya kanisa hilo Njombe kwenye viwanja vya makaburi ya viongozi.


Waombolezaji wakiwa katika mazishi

Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Katikati, akiwa katika mazishi ya Askofu mstaafu





mama mjane wa marehemu

Mama mjane wa marehemu akiweka Udongo katika Nyumba ya Milele ya askofu Cliopa







Mama njane akiweka taji la maua




Mwakilishi wa Shehe wa Mkoa aliweka taji nae.

Kiongozi mkuu wa Kanina KKKT akiweka shahada la maua katika Kaburi


Mkuu wa mkoa alipana nafasi ya kutoa neno la faraja kwa wafiwa

Kiongozi wa mkuu wa KKKT Tanzania, Marasusa akizungumza na mamia ya waombilezaji 



KIONGOZI Mkuu wa kanisa la Kiinjili la Kiluteri (KKKT) Alex Malasula amewataka viongozi wa ngazi mbalimbali hapa nchini kuacha mara moja kufanya uovu wa kutumia vibaya mali za Umma na kujitete.

Akihubiri katika madhishi ya Askofu Mstaafu wa kanisha hilo jimbo la Njombe, Askofu Cliopa Lukilo, jana aliye fariki Novemba 13, aliwaambia waombolezaji kuw aviongozi wa sasa wamekuwa wakifanya uovu na kujikinga kwa kujitetea kwa wepesi.

Alisema kuwa viongozi wa miaka ya sasa wamekuwa wakifanya maovu ya kutumia vibaya pesa za umma na kuwa wepesi wa kujitetea kwa kucheleweza kudaiwa wakati wakitafuta namna ya kukepa tuhuma.

Alisema kuwa kufanya hivyo si vizuri na kuwasii viongozi kufanya kazi bila kuharibu mali za wananchi kwa kuzitumia vizuri.

Alisema kuwa viongozi wengi hawapendi kutubu na wamekuwa mafundi wa kujitetea kwa kusingizia katiba na kuwa wanasema jambi lipo mahakamani halijadiliki.

“Watu wengi sasa hivi ukiwaambia kutubu hawakuelewe wanatishia watu kuwashitaki, wansema jambo hili lipo mahakamani halijadiliki, mara umenichafua, dawa ya zambi ni kutubu na sio kujitetea,” alisema Malasula Sikiliza sauti hapa......


Alisema ukiona kitu kinacheleweshwa cheleweshwa ujue kinatafutiuwa namna ya kujitetea.
  
Malasusa alisema kuwa Marehemu alikuwa akipigania haki za watoto wakike kwa kufungua shule ili kuwaondoa katika kazi za ndani.

Alisema kuwa ni vyema wanadam wakatambua wakati wowote wanaweza kuitwa kwani marehemu aliwahi kuugua lakini sasa amefariki kuugua bila.

Alisema kuwa marehemu alifariki siku nne baadae baada ya kusema kuwa yeye amejiandaa kufa wakati akifungua mkutano wa umoja wa wanawake wa makanisa mkoani Njombe.

Alisema kuwa marehemu alitaja mara nne kuwa anejiandaa kuwa akisema “Mimi nimejiandaa kufa, mini nimejiandaa kufa vizuru” alisema wakati wa kufungua mkutano huo na kufa siku nne baadae.

Aidha kanisani hapo zilizomwa salamu za rambilambi kutoka katika viongozi mbalimbali kutika hapa nchini na nje ya nchi huku kwa hapa nchini Waziri mkuu mstaafu Edward Lowassa salamu zake zilisomwa kanisani hapo.

Viongozi wa serikali katika mazishi hayo alihuzuria mkuu wa Mkoa wa Njombe Dr Rehema Nchimbi, ambapo aliomba viongozi wa dini kuwaombea viongozi wa Umma ili kuepuka na maovu.



Dr. Nchimbi alisema kuwa viongozi waombewe ili wasiweze kutafuna mali za umma na kuwa watiifu wanavyo ongoza wananchi mpaka wanamaliza mda wao wa kuongoza kwani viongozi hao ni moja ya kondoo wanao wachunga.