Vibali vya kuuza mahindi vyatolewa rasimi wauzazi kuomba kwa Katibu tawara wa Mkoa

SERUKALI Mkoani Njombe imewataka wakulima na Wafanyabiashara kuitumia fursa ya kuuza zao la mahindi Nje ya Nchi  baada ya kurahisishwa kwa upatikaniji wa vibali ambavyo kwa sasa vinatolewa na makatibu wa tawala
wa Mikoa tofauti na awali vilikuwa vinatolewa na wizara ya viwanda na biashara.

Akizungumza na East Africa Radio Afisa kilimo Mkoa wa Njombe Awariywa Nnko amesema kuwa kila mfanyabiashara anaruhusiwa kuuza mazao yake nje ya nchi kwa kufuata masharti yaliyoweka wakati wa ukataji wa kibali.



Hatua hii  imekuja kufuatia kuwepo kwa mrundikano wa mavuno ya mahindi yaliyokosa soko wakati hali ya uzalishaji wa mahindi kwa mwaka 2013/14 jumla ya tani 411,802 zilizalishwa katika mkoa wa Njombe.

Aidha Nnko amesema kuwa licha ya Wakala wa Hifadhi ya Chakula ya  Taifa NFRA tawi la makambako  kufanikiwa kununua tani 26,116 za mahindi hadi kufikia Novemba 5 mwaka huu sawa na asilimia 6.3 ya mavuno ya mahindi hivyo kufunguliwa kwa soko hilo kutasaidia wananchi kuuza mazao yao na kusababisha mahidi kupanda bei iliyo kuwa ikitarajiwa na wananchi.