Israel yasema imeidungua ndege ya kivita ya Syria


Jeshi la Israel limesema limeiangusha ndege ya kivita ya Syria katika milima ya Golan, ikisema ilikuwa imevuka mpaka wa usitishaji mapigano katika eneo linalokaliwa na Israel.  Hili ni tukio kubwa zaidi kutokea katika eneo hilo tangu kuanza vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini Syria mwaka wa 2011.
Image result for Israel Pix 

Taarifa iliotolewa na jeshi la Israel ambayo haikuwa na maelezo zaidi ilisema ndege hiyo iliyoingia eneo la Israel ilifanikiwa kudunguliwa muda mchache kwa mfumo wa kujilinda wa angani karibu na mpaka wa Syria. Kudunguliwa kwa ndege hiyo kunakuja wiki tatu baada ya Israel kuiangusha ndege nyengine isokuwa na rubani iliokuwa katika anga ya milima ya Golan wakati mapigano yakipamba moto upande wa Syria, ambapo eneo kubwa linashikiliwa na waasi wanaopigana kuuangusha utawala wa Bashar Al Assad. Syria imethibitisha kuangushwa kwa ndege yake ya kivita na kukielezea kitendo hicho kuwa cha uchokozi.