MWANAPAZI "KATIBA HII SIO CHAMA WALA DINI"



















Haya ni matokeo kwa waliopiga kura ya kupendekeza muundo wa serikali tatu
KATIKA uchangiaji na kutoa maoni katika rasimu ya katiba Mpya wananchi wametakiwa kutoingiza itikadi za kisiasa wakati wa kuchangia.

Akifungua baraza la Katiba lililoandaliwa na Asasi ya Hope for Deprived Action in Deveropment (HDPAD) ya Mji mdogo wa Mbalizi jana Afisa Mtendaji wa Kata ya Usongwe, halmashauri ya Mbeya, John Mwanapazi alisema kuwa wajumbe katika katiba hilo wasionyeshe itikadi yoyote.

Alisema kuwa wanao changia katika baraza hilo wasipinge kile kilichopo katika Rasimu hiyo kwa kuonyesha itikadi ya aina yoyote iwe ya kidini ama kisiasa.

“Katiba hii ni ya Tanzania sio ya kanisa ama dini yeyote na sio katiba ya chama chochote cha kisiasa maoni yako yasiwe kamelenga katika chama Fulani au kanisa unalotokea,” Alisema Mwanapazi

Aliongeza Katiba hii siyo ya Chadema, CCM wala CUF katiba hii ni yawatanzania wote ya kizazi cha sasa na kijacho.

Alisema kuwa katika mapitio hao wasije wakaingiza chuki binafsi kwa kuwa watu wanaugomvi wao wakapingana  katika maoni yao.

Aliongeza kuwa katika maoni yao waangalie kuwa wanatoa maoni ambayo ni ya taifa na sio ya kwao binafsi na kulenga kila kona ya nchi yetu.

“Ndugu washiriki hakikisheni maoni unayo yatoa yawe yamelenga katika mrengo wa kitaifa zaidi na sio kuangalia kwa upanda wa kikata,” Alisema Mwanapazi