MTOTO
Pasto Furaha (11) mwanafuzi wa daraza la pili, mkazi wa kijiji cha Mapinduka
kata ya Igurusi wilayani Mbarali mkoani Mbeya amefariki dunia baada ya kugongwa
na lori.
Kwa
mujibu wa kamanda wa Polisi Diwani Athumani alisema kuwa mtoto huyo aligongwa
na roli hilo Juzi majira ya 12:30 jioni katika maeneo ya Mwapimbuka barabara ya
Mbeya- Iruinga mkoani Mbeya.
Alisema
Marehemu huyo alifariki wakati akipatiwa matibabu katika kituo cha afya cha
Igurusi na mwili wake umehifadhiwa kituoni hapo.
Alisema
kuwa mtoto huyo alikuwa mwanafunzi wa daraza la Pili katika shule ya msingi
Igurusi ya wilayani humo.
Athumani
alisema kuwa gari hiyo ilikuwa ikiendeshwa na Habibu Hassan (28) likiwa na
namba za usajili T 877 CLX na trela namba T 242 CLV aina na Iveco.
Alisema
kuwa gari hiyo inashikiliwa na Polisi na lipo katika kituo cha polisi cha kata
ya Igurusi.
Aliongeza
kuwa chanzo cha ajali hiyo ni mwengo kasi wa dereva wa roli hilo la mizigo na
akasababisha ajali hiyo.
Athumani
alisema kuwa jeshi la Polisi linatoa wito kwa watumiaji wa barabara kuwa makini
na madereva kuwajali watembea kwa miguu.